Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii(SSRA), Dkt. Irene Isaka

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii(SSRA), Dkt. Irene Isaka

Kwa mfano, serikali walipochota Tsh trilion 8.34 za wastaafu, walimwelekeza atoe hizo hela haraka na kama angekataa angefutwa kazi au hata kuzuliwa kesi au kupotezwa na watu wasiojulikana. Kwa hiyo Irene ametolewa kafara ili kuinusuru serikali iliyoifilisi hiyo mifuko.
Yule mama Falaa sanaa...Hata kama unatumwa inabdi uangaliee kipi cha kusema na kutetea..!! Hata wakuu wa polisi ukiwa unatumwa kupiga raia na unaendaa tu siku kikiwakaa Mkuu anakukataaa...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ajabu! Kosa lifanywe na sehemu zote za bunge (Rais na watunga sheria) halafu Irene atolewe kafara. Yajayo ni ya kufikirika.
 
Nyie watu mkoje? Hivi hili swali si lilitetewa bungeni? Yaani sijui hamna akili ama huwa mnajitoa akili. Irene kwani alikuwa anapanga mwenyewe bila ya kupitisha kwa wenye mamlaka ya kutunga kanuni?

Kikokotoo hutengenezwa na Waziri mwenye dhamana, mkurugenzi wa SSRA hahusiki!
Duu

Sent from my TA-1024 using Tapatalk
 
Hilo jambo ni kubwa sana na bila shaka yoyote lilifanyika kwa shinikizo kubwa ya wanasiasa serikalini. Hakuna mtumishi wa umma anayeweza kuwa na mawazo mabaya kiasi kile dhidi ya wenzake na yeye mwenyewe. Na mantiki yake tuliambiwa ni ili kupata fedha za kujenga viwanda!
 
Ndiyo ujuwe ni usanii mtupu baada ya kuanzisha tatizo makusudi na kujifanya tena wanalitatua

Sent using Jamii Forums mobile app
Wakati anaanzisha halikuwa tatizo bali mkakatiti maridhiwa wa serikali kupata mtaji kwa miradi yake.limegeuka kuwa tatizo baada ya kila mwenye pumzi kulaani. Ndani ya Jf, mbali na yule Mbunge wa Singida sidhani kama kuna watu walitetea uamuzi huo wa serikali kama ilivyo ada! Watetezi nao walishikwa pabaya! When they came for for the communists I did not bother, for I was not a communist!
 
Viongoz wapenda cfa matatzo ya wananchi ni mitaji yao kisiasa ,wanavuruga ili watengeneze waonekane mashujaaa kwa macho mawili lkn la tatu ni wakupuuzwa kabisa na kudharauliwa,
 
Mawazo yangu yapo tofauti kidogo na wengi, wengi tunaangalia pale tulipodondokea na siyo pale tulipojikwaa. Nazani wote tulimsikia Raisi akisema mifuko haina pesa na ndio maana mamlaka husika(SSRA) ikaja na aina mpya ya kikokotoo ili kuokoa jahazi.

Swali la msingi la kujiuliza, Ilikuwakuwaje mpaka mifuko ikafilisika? Raisi aligusia kidogo kwamba kufilisika huko kulitokana na uwekezaji usio na tija mfano mradi wa Dege Eco village huko kigamboni.
Nilimsikia mhusika mmoja akisema mifuko ya hifadhi ya jamii ilikuwa na kiasi cha trillioni 13 na hivi sasa wamebakia na trillioni 1 point something pekee, kwa kifupi trillioni 12 either zimewekezwa kwenye miradi ambayo haifanyi vizuri au kiasi kikubwa cha hizo fedha zimepigwa.
Hivi inakuingia akilini kweli trillioni 12 ziwekezwe kwenye miradi isiyofanya vizuri au zipigwe ilihali mamlaka zinazosimamia hii mifuko zipo(SSRA), waziri mwenye dhamana yupo, TAKUKURU IPO, CAG yupo, sasa kwa nini imechukua muda mrefu sana mamlaka zote hizi kugundua kwamba haina ya uwekezaji iliyokuwa inafanywa na hii mifuko haina tija?
Kumbuka kwamba hii mifuko inaendeshwa kwa kanuni na sheria, kwa hiyo sizani kama watendaji wa hii mifuko wanaweza kujiamulia tu kuchukua bilioni kadhaa na kuwekeza kwenye miradi kama wa Dege bila kuhusisha mamlaka husika zinazosimamia hii mifuko, na vile vile ndani ya hii mifuko kuna mavaluer na mauditors wakutathimini hii miradi na pia kutoa annual balance sheet kwa mamlaka husika inayoonyesha financial soundness of the fund, inakuwaje sasa hawa wote walishindwa kubaini hayo yote mpaka tunafikia huku?
Wengine wanasema hii mifuko ilikuwa sehemu ya serikali kujichotea pesa, binafsi sijui kama hilo Lina ukweli lakini swali langu, katiba ya hii mifuko inawaruhusu wao kuwakopesha waajiri wanaochangia katika hii mifuko au kuwekeza kwenye miradi ya waajiri?

Kama hayo yote yaliweza kufanyika hadi mifuko ikafilisika na hatujasikia watu kukemea au kupelekwa mahakamani kwa matumizi mabaya ya madaraka au ufisadi sizani kama kutakuwa na maajabu katika hii mifuko simply because Dada Irene kapangiwa majukumu mengine.
Haya maswali uliyouliza Kiongozi yote ni muhimu. Sasa tusogee ngazi moja mbele, Serikali yetu imechukua hatua kwa mshauri ambaye mpango wake (no matter how evil it may sound) ulilenga kuwasaidia watumishi kupata japo kwa udogo wake (mafao) wayapate kwa muda mrefu.
This is lesser evil ukiniuliza Mimi comparing it na other evils mentioned in your article. Swali kuwa ni kama haya yote uliyoyaainisha, ushauri mbaya wa wataalamu, juu ya ufanisi wa miradi, na uwekezaji wa zaidi ya asilimia 85 ya michango ya wachangiaji wa mifuko, ambao najua serikali inaouwezo wa kupata taarifa na kujenga kesi ambayo, basically ndio msingi wa kutatua hili tatizo.

Kwa nn serikali haifanyi hayo, yaliyo ndani ya uwezo wake... Unless yenyewe ndiomkopaji mkubwa zaidi. Na mfilisi wa mifuko?! Just thinking out loudly!!
 
Rais wetu ni msikivu sana. Mungu amlinde na kumpa afya njema. Sent using Jamii Forums mobile app
Rais wetu ni msikivu sana. Mungu amlinde na kumpa afya njema. Sent using Jamii Forums mobile app
Rais wetu ni msikivu sana. Mungu amlinde na kumpa afya njema. Sent using Jamii Forums mobile app
Rais wetu ni msikivu sana. Mungu amlinde na kumpa afya njema. Sent using Jamii Forums mobile app
Siasa za maji taka!!Mama ndiyo alitunga hiyo sheria mbovu??! Sent using Jamii Forums mobile app
Siasa za maji taka!!Mama ndiyo alitunga hiyo sheria mbovu??! Sent using Jamii Forums mobile app
[QUOTEd="Allen Kilewella, post: 29801875, member: 55849"]Hakuwa anatetea jambo binafsi. Ile ndiyo huitwa "Collective Responsibility"[/QUOTE]
Kwa cheo chake angeweza kuzuia hili lakini kwa sabab wanafanya kazi kwa uoga ndio imempelekea kufika pale...na yeye ni dhaifu maana ameshindwa kujenga hoja
Hizo sio hisia? Utaratibu wa kutangaza jambo kubwa kama hilo kwenye taasisi ya umma ukoje?
 
Kama ungekwua ni ushauri wa Jenista si angemvua uwaziri, kwanini atengue uteuzi wa mkurugenzi na sio wa waziri
Strange! Watanzania uelewa wetu ni mdogo sana na labda njaa zinatufanya tuwe makasha matupu! Unasema kama angelikuwa amemshauri Jenesta angeli mvua uwaziri. Kwanini Makonda bado yupo kazini. Ana Jinai ngapi kubwa alizozifanya na bado yuko kazini? Waliofanya makosa kama ya Makonda ni wangapi na wakafukuzwa? Huyu ana selective prosecution and highly biased man of no ryle of law! A dictator!
 
vyama vya wafanyakazi vya tanzania havijawahi kusimamia hata mara moja maslahi ya wafanyakazi wa Tanzania, kwenye swala la kikotoo walishirikishwa mwanzo mwisho sema baada ya kusikia kelel za wafanyakazi ndio na wao wakaibuka ningewaelewa kama wangepiga kelele toka mwanzo lakini iliwachukua muda mrefu kueleza misimamo yao kwa kifupi hawana tofauti na wanasiasa hata matumizi mabovu ya mifuko ya hifadhi ya jamii katika hiyo mifuko kuna wawakilishi wa wafanyakazi kwenye bodi ya hiyo mifuko lakini jiulize kwanini bado mifuko inafuja pesa za wafanyakazi.
Hiyo miradi anayolalamikia rais mingi ilifanyika wakati mkurugenzi mkuu wa NSSF akiwa Ramadhani dau lakini rais amempa ubalozi, tumia kichwa chako kuchambua mambo usisubiri kuchambuliwa

Hapo unabuni huna uhakika na ulisemalo, wawakilishi wa wafanyakazi serikalini kama wangewakilishwa mwanzo, kungekuwazogo kubwa kushushwa kutoka 50% mpaka 25% lump sum hapo hakuna ulicho chambua


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli leo tarehe 28 Desemba, 2018 ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Dkt. Irene Isaka.

Mapema leo Rais Magufuli alifanya kikao cha wazi na Viongozi waTUCTA, watendaji wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (PSSSF na NSSF) na Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii(SSRA) kujadili masuala yahusuyo Mafao ya wafanyakazi hususani KIKOKOTOO na Rais Magufuli alifikia hitimisho kwamba Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika).
Pia soma
> Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika) - JamiiForums

Irene Charles Isaka, Director General, Social Security Regulatory Authority - JamiiForums
 
Sanaaaa! Nilijiuliza anawezaje kujitokezana kutetea kitu kama kile
Mzee alikuwa anaamini kama waliosema ndiooooo kule bungeni ni wa kwa mjomba, sasa hapa anapapase macho. Isitoshe hawa watu sidhani kama wanatolea macho sana vijisenti vya kuchukua uzeeni. Wanapiga mpunga wakutosha angali meno iko.
 
U
Kwa cheo chake angeweza kuzuia hili lakini kwa sabab wanafanya kazi kwa uoga ndio imempelekea kufika pale...na yeye ni dhaifu maana ameshindwa kujenga hoja
Uongo mchana kweupe,yeye anaweza pinga vipi miongozo ya serikali?au haujawahi kuwa mtumishi?
 
Back
Top Bottom