Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii(SSRA), Dkt. Irene Isaka

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii(SSRA), Dkt. Irene Isaka

Kaangushiwa jumba bovu huyu

Sent using Jamii Forums mobile app

Jaribu kuvuta kumbukumbu za aliyewahi kuwa waziri wa nishati Mr Msabaha pale Bungeni aliposema yeye ni "Bangusilo" watu tukatafuta maana yake tukakuta ni kondoo wa kafara, huyu binti naweza sema 100% hana kosa bali ni wana siasa wamemponza ila uzuri very soon watamliwaza
 
Kwenye nchi za wenzetu waliostaarabika ambao sisi tunawaita MABEBERU, J.Mhagama alingejiuzulu mara baada ya kile kikao. Lakini cha kushangaza zaidi nae alijumuika kwa kushikana mikono na rais kwa furaha sijui za kweli au kujifanyisha akaimba
 
Labda na yeye ataona umuhimu wa fao la kujitoa baada ya kutenguliwa🙄
 
Alikuwa anang’ang’ania kunyang’anya mafao ya wafanyakazi as if ni pesa zake binafsi, binafsi nimemchukia kupitiliza, mafao yetu akae nayo mbali, kwa kweli kwenye hili namfagila jiweee ila 2020 simchagui...
 
View attachment 979879
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli leo tarehe 28 Desemba, 2018 ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Dkt. Irene Isaka.

Mapema leo Rais Magufuli alifanya kikao cha wazi na Viongozi waTUCTA, watendaji wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (PSSSF na NSSF) na Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii(SSRA) kujadili masuala yahusuyo Mafao ya wafanyakazi hususani KIKOKOTOO na Rais Magufuli alifikia hitimisho kwamba Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika).
Pia soma
> Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika) - JamiiForums
Amejitahidi maana hicho kikokotoo kilikiwa kinawapa wengi headaches... Ila nasubiri kuona kama kweli huyu mkurugenzi aliyetenguliwa atapangiwa kazi nyingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom