Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii(SSRA), Dkt. Irene Isaka

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii(SSRA), Dkt. Irene Isaka

Great thinkers wameisha kabisa JamiiForums. Mmeambiwa kabisa kwamba atapangiwa kazi nyingine eti watu wanapoongeza ametumbuliwa. Maana yake alifanya kazi yake ipasavyo, ila tu mambo yamehalibika hivyo watampa kazi nyingine. Maslahi yake pale pale. Sisi mazuzu tunadhani ametumbuliwa
 
Narudia tena, rais ni mmojawapo katika hilo tatizo, rais, na wabunge wa ccm ni sehemu ya hiyo sheria mbovu. Kama wabunge walipitisha kitu kibovu rais halazimishwi kusaini, alipaswa kurudisha kabla ya kusaini kuwa sheria. Wabunge wa upinzani walipiga kelele nje na ndani ya bunge. Hapo rais na wabunge wa ccm wanajiteteaje?

Anyway, Rais katengua hiyo sheria, je sheria iliyosainiwa inatenguliwa kwa mdomo tu? Leo hii ukienda mahakamani kudai haki, mahakama watahukumu kwa mujibu wa sheria iliyosainiwa au watafuata busara za rais?
Sheria haijatenguliwa mkuu kilichotenguliwa ni kanuni na kanuni hiyo ni kipengele kimoja cha kikokoto

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli leo tarehe 28 Desemba, 2018 ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Dkt. Irene Isaka.

Mapema leo Rais Magufuli alifanya kikao cha wazi na Viongozi waTUCTA, watendaji wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (PSSSF na NSSF) na Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii(SSRA) kujadili masuala yahusuyo Mafao ya wafanyakazi hususani KIKOKOTOO na Rais Magufuli alifikia hitimisho kwamba Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika).
Pia soma
> Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika) - JamiiForums
Asante mh John Pombe Joseph Magufuli kwa kutuondolea huyu mama "Dr" Irene, ambaye huko nyuma nilitilia wasi wasi sana "Phd" yake.
Huyu mama alishindwa kabisa kelezea 20% wanayochangia wafanyakazi kwenye mfuko wa pendheni, na 25% ambayo mfanyakazi analipwa kutokana na jumla ya makato yote.

Sisikitiki na nilimdharau sana kwa kujaribu kueleza vitu ambavyo ni dhahiri alikuwa havijui kabisa mantiki yake.

Swali langu ninkwamba alifikaje hapo?
Kulikuwepo na due diligence, vetting ya elimu yake na uwezo?
 
Narudia tena, rais ni mmojawapo katika hilo tatizo, rais, na wabunge wa ccm ni sehemu ya hiyo sheria mbovu. Kama wabunge walipitisha kitu kibovu rais halazimishwi kusaini, alipaswa kurudisha kabla ya kusaini kuwa sheria. Wabunge wa upinzani walipiga kelele nje na ndani ya bunge. Hapo rais na wabunge wa ccm wanajiteteaje?

Anyway, Rais katengua hiyo sheria, je sheria iliyosainiwa inatenguliwa kwa mdomo tu? Leo hii ukienda mahakamani kudai haki, mahakama watahukumu kwa mujibu wa sheria iliyosainiwa au watafuata busara za rais?
Mimi siko kwenye hizo complication zenu za kichadema! kudandia kila kinachopita mbele yenu. Ona wenzako mpaka sasa hawaoni kuwa wanatetea suala la fastjet na wanasema bila haya waruhusiwe kurusha ndege na suala la usalama lifumbiwe macho!
 
Magufuli huwa hapendi ujinga na watu kufanya kazi kwa mazoea. kauli ya hapa kazi tu inaendelea kuwa wazi na lazima ieleweke Magufuli anaposema hapa kazi anamaanisha nini anasema.
Wakati yeye ndo mjinga namba moja.No raid gan aliisain hiyo sheria? Mwenyekiti wa baraza la mawaziri ni nani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli leo tarehe 28 Desemba, 2018 ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Dkt. Irene Isaka.

Mapema leo Rais Magufuli alifanya kikao cha wazi na Viongozi waTUCTA, watendaji wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (PSSSF na NSSF) na Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii(SSRA) kujadili masuala yahusuyo Mafao ya wafanyakazi hususani KIKOKOTOO na Rais Magufuli alifikia hitimisho kwamba Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika).
Pia soma
> Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika) - JamiiForums
Irene Charles Isaka, Director General, Social Security Regulatory Authority - JamiiForums

wala tusipoteze muda kuuliza na kubuni sababu za kutengua uteuzi. uzuri Rais wetu anatabirika sana. kwa kuwa hili jambo la kikokotoo limeshafanywa kete ya kisiasa na kujitafutia umaarufu wa kupendwa kama mtetezi wa wafanyakazi, mpeni muda tu.. siku sio nyingi ataropoka kwenye matukio yake sababu za kutengua...hata kama atatengeneza sababu na kuacha ukweli pembeni
 
Nyie watu mkoje? Hivi hili swali si lilitetewa bungeni? Yaani sijui hamna akili ama huwa mnajitoa akili. Irene kwani alikuwa anapanga mwenyewe bila ya kupitisha kwa wenye mamlaka ya kutunga kanuni?

Kikokotoo hutengenezwa na Waziri mwenye dhamana, mkurugenzi wa SSRA hahusiki!
Kwanini asingejiondoa kwenye hiyo nafasi ya ukurugenzi, kuendelea kuwepo hapo ina mana alikubaliana na mambo aliyoletewa kuyasimamia kuhusu mafao ya watumishi.
 
Mmeambiwa kabisa kwamba atapangiwa kazi nyingine..
Hiyo huwa ni statement tu kuua soo. Ninawafahamu vigogo watatu “walioenguliwa” kwa gear ya kupangiwa kazi nyingine tangu mwaka jana. Wapo tu wizarani wanasugua benchi huku wakisoma magazeti.
 
Back
Top Bottom