Rais Magufuli atengua uteuzi wa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Dkt. Ave Maria Semakafu

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Dkt. Ave Maria Semakafu

Wanawake kuweni na akili. Alichofanya Magufuli hapa si tu kutengua uteuzi Bali pia kumdhalilisha Semakafu kwa kumuita mpumbavu hadharani. Wanawake mna jambo na Magufuli 28/10/2020. Mmedhalilishwa mno
Na katika rais asiye na staha ni huyu huwa anatukana watu hadharani sio Mara moja na kwa kuwa ni wa kutoka majalalani wanabakia kukenua tu.

Kwakuwa huwa nawaona hawawezi kuchukua hatua za kulinda heshima za utu wao naona ni sawa tu awatukanage hawana akili, angejitokeza hata mmja ku protest kwa kujiuzulu huyu jamaa angekoma kudharirisha watu. Mimi boss wangu hawezi nitukana ofisini namjibu vizuri tu atakoma sasa hawa kujiuzulu tu kwa kulinda utu wao hawawezi, tukana tu hao Hadi akili ziwajie
 
Kwa nini mambo kama haya hayajadiliwi tena bungeni ? Au ndio bunge limekuwa BUBU?😳
 
Maamuzi mazito kama yale ni ngumu kuwa maamuzi bila Baraka toka juu, anawatumia wenzake kama mpira
Huyo Ave Maria ametolewa kafara tu kwa sababu uamuzi wa kutangaza kufutwa certificate ulitolewa mwaka 2014.

Unless iwe kamfuta kazi kwa sababu nyingine lakini kama sababu ndio hiyo basi kaonewa tu... labda kwavile Magufuli anaona atakosa kura za walimu wenye certificate, ingawaje wao hawataguswa!

In short, awamu ya IV ilisomesha walimu wengi sana tena sana na walikuwa wanaajiriwa!! Kutokana na ile kasi, ndio ikafikia Walimu wa Shahada hususani masomo ya art wamejazana mashuleni kwa sababu walikuwa wengi mno huku serikali ikiendelea kuajiri!

Ndipo hapo likaja suala kwamba walimu wenye shahada (arts subject) wataajiriwa kwenye shule za msingi kwa sababu kule sekondari walishajaa lakini stahiki zao zitabaki kama za walimu wengine wa sekondari!

Lakini kwavile bado kuna changamoto ya walimu wa sayansi, ndipo ikaanzishwa ile 3-Years Special Diploma (Science & Maths) pale UDOM ili baadhi yao wakafundishe secondary schools na wengine primary schools.... lakini JPM akaifuta ile programu

Sasa ikiwa hata Mwalimu wa Shahada anaenda kufundisha primary school hiyo certificate ni ya nini tena?!
 
Kabisa! Huyu mama katolewa kafara. Uamuzi wa kubadili sera usingeweza kufanyika bila ridhaa ya baraza la mawaziri ambapo Rais ni mwenyekiti, wizara inatekeleza tu.

Sasa hapa eti tunaaminishwa kwamba uamuzi huo ulifanya na NAIBU katibu mkuu? Wala sio katibu mkuu au naibu waziri au waziri? Hizi hadaa nyingine hapana..
Huo uamuzi ulipita tangu 2014!
 
Miaka 5 ya tumbua tumbua.

Watu hawashtuki tena.
 
Na nimefurahi ametumbuliwa, ni muda muafaka sasa nae aende akajitolee au akajiajiri.

Wanaropokaga kikuda sana wakipata madaraka.
Screenshot_2020-10-06-05-06-07-1.jpg
 
Duh....ndio maana huyu mzee kupata kura za watu wenye akili ni ngumu sana.
Mambo hayawezi kwenda hivi.
Huyu mama naamini hakuamka mwenyewe na kutoa tangazo hili.
Hivi tujiulize kwa ulimwengu huu bado tunahitaji walimu wa certificate?...
 
Wanyooshe hao mzee baba
Narudia tena wanyooshe hao mzee baba
Mi nipo Hapa Denmark nakula maisha kwanza nikirudi nikute hali shwari
 
Avemaria ni mwanaccm damudamu kabisa. Ni wale ambao wako tayari kuacha kupitia familia wakikimbilia mambo ya chama. Ila ni mkorofi kupindukia. Kuna watu watakuwa wamefurahia sana.
Hili jambo limepangwa. Na ili lipangike vizuri lazima atumiwe kada anayeweza kuelewa mchezo mzima.

Huyo mama anaelewa kila kitu toka tangazo limetoka hadi kutenguliwa sababu ni kumbeba asiye bebeka kwa ahadi kuwa atakumbukwa awamu ifuatayo.

Asichojua Hugo mama ni kuwa AME bet kwa Liverpool dhidi ya Aston villa kwa kufuata jina, kichapo cha Magufuli October ni kile cha Liverpool.

Walimu wote wameshashtuka mchezo wa "tengeneza tatizo kisha litatue upate credits"
 
Na nimefurahi ametmbuliwa,ni muda muafaka sasa nae aende akajitolee au akajiajiri.

Wanaropokaga kikuda sana wakipata madaraka.View attachment 1591683
Suala la kujitolea ni upumbavu, na hata mpango wenyewe ulivyokuwa haukusema wenye certificate wasiajiriwe bali ulisema program ya certificate vyuoni inafutwa... kwamba, serikali isingedahiri wanafunzi wengine kusomea ngazi ya certificate!
 
Hongera sana rais wangu ,tunataka mtu mwenye maamuzi magumu
 
Yaani hii ishu walimtegea kabisa huyo mama

Yaonekana ana kihehrehere sana sana Sasa wakaamua wamuekee mtego[emoji1787][emoji1787]

Magufuli kala kichwa [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Haya sasa. Kwahiyo semakafu anasulubiwa kwanini?
Hakuna sababu ya msingi zaidi ya kuwa ametangaza hadharani wakati ni kipindi cha uchaguzi!! Magu anataka kuhadaa watu kwamba bado yupo na watu wa Form IV Div IV wanaotaka kusomea ualimu wakati ukweli ni kwamba mpango wa kufutwa certificate upo kwa zaidi ya miaka 5 sasa!!
 
Kabisa! Huyu mama katolewa kafara. Uamuzi wa kubadili sera usingeweza kufanyika bila ridhaa ya baraza la mawaziri ambapo Rais ni mwenyekiti, wizara inatekeleza tu.

Sasa hapa eti tunaaminishwa kwamba uamuzi huo ulifanya na NAIBU katibu mkuu? Wala sio katibu mkuu au naibu waziri au waziri? Hizi hadaa nyingine hapana..
Ilani ccm uk 129(n) ipo wazi
 
Hongera sana rais wangu ,tunataka mtu mwenye maamuzi magumu
Kama yapi?! Ya kumfuta mtu kazi kwa sababu ya kutangaza sera ya serikali yake mwenyewe, au?! Hivi kwa akili yenu mnaamini kabisa Naibu Waziri anaweza kuchukua uamuzi mgumu kama huo pasipo na kuridhiwa na serikali?! Pasipo na kupitishwa na Baraza la Mawaziri?!

But this sounds good kwa sababu kina-reflect kile kile ambacho mara kwa mara tumekuwa tukisema hapa endeleeni kushangilia udhalimu wa hii serikali kwa sababu mnadhani mkiwa ni wapiga makofi mtakuwa salama but none is safe!!!
 
Back
Top Bottom