Rais Magufuli atokwa na Chozi la huzuni: Mzee Mkapa alinilea kama mtoto wake, alikuwa ni shujaa wangu, alinionyesha upendo

Yeah kitu muhimu ni kuheshimu madaraka na uwezo wa mwenzie katika uongozi..
Hata Magu yapo anayokosea na yapo anayofanya vyema
Hivyo huwezi judge uongozi wa mwenzako
 
Nakumbuka mwalimu wangu O'level nilipendelea sana kumuita Godfather alikua anapenda kusema fanya yote lakini "what legacy do you leave behind" raisi tumeona ndio imemuuma sana lakini tujiulize vipi familia za kina sanane,Azwory zinapitia maumivu gani?
 
Mimi siangaliagi wala sisikilizagi hizo mambo, naumiaaa
 
nilie [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Pole sana Jpm huu ni msiba mzito sana kwako. Mungu akutie nguvu. Najua huko magetoni hapakaliki ni kilio mwanzo mwisho
Ni msiba mzito halipingiki sote ni yetu njia. Alijitahidi kutufikisha sehemu kama taifa hakuna mkamilifu zaidi ya Muumba kizuri ameacha WOSIA.
 
Kama kweli alikuwa ni shujaa wake amuenzi kwa kulifanyia kazi ombi la Mkapa ili Tume Huru ipatikane kabla ya uchaguzi wa 2020.
Hebu niulize wakuu hapa:

Kwani Tume ya kusimamia uchaguzi inahitaji watu wenye utaalam wa aina gani?

Tukikusanya maaskofu kadhaa na Masheikh wa kutosha na kuwakabidhi jukumu la kusimamia uchaguzi kwa haki, hawa watu hawawezi wakaifanya hiyo kazi kwa ufanisi katika muda huu mfupi uliobaki kabla ya uchaguzi?

Lakini CCM hawataki hata kulisikia hili; na kwa kustaajabisha kabisa, hata wapinzani halionyeshi kuwaumiza vichwa!
 
Ahsante sana Mkuu umekuja na wazo zuri sana la kupata Tume Huru na bado kuna muda wa kutosha tu wa kukamilisha hili.

 
Mbona hili ni rahisi sana mkuu 'Tripo9.'
Kulia au kutolia kunategemea mawazo yako wakati unayasikia hayo maneno na jinsi huyo anayeyasikia maneno anavyomchukulia huyo aliyeyatoa maneno.

Kama msikilizaji hamwamini anayeyasema maneno, nini hasa kitamfanya alie?

Kama msikilizaji alishafanyiwa jambo la kikatili na anayetoa maneno ya kuliza, hayo maneno peke yake ndiyo yamfanye atokwe machozi bila ya kumfikiria mtu anayeyasema hayo maneno?

Kuna pia sehemu ya marehemu katika hili. Kama kulikuwepo na jambo zito sana ambalo msikilizaji hakuwa anakubaliana na marehemu, hiyo nayo inaweza kuwa sababu mhimu ya kutoamsha hisia za kutoa chozi juu yake. Kuna mambo mengine chungu nzima.
 
Hata we ukija kuwa raisi utakuja kuona jinsi ilivyokuwa ngumu kuongoza kila kashfa nzito kwenye nchi utahusishwa wewe...

Hata yeye aliwahi kunyeshwa sumu na hata akakaribia kukata tamaa ya uongozi..
Kwahiyo kalipiza kunyweshwa sumu kwa kutaka kumuua lisu?
 
Huyu mzee alitulea wote kama taifa,sioni hasara kwa mzee magu kumwaga chozi,we ve to learn how to appreciate
 
Aliwahi msifia wakati ule mkapa akizindua kitabu chake my life my purpose
 
Yeye alionyeshwa upendo Leo anawaonyesha chuki wengine JPM u need to change Mr President.
 
Swali zuri sana. Nimesikia kuwa kulikuwa na kodi ya kichwa, baiskeli na mifugo wakati huo! Lakini usishangae wanasiasa wakampamba Mwinyi kuliko Mkapa. Tuombe tu uzima.
Tafuta uzi humu kuhusu legacy ya mzee mwinyi uelewe kwa undani mchango wa mzee mwinyi katika taifa hili.
 
Kwa mujibu wa sifa zilizotolewa katika kipindi hiki ni wazi kuwa Mkapa alipokea taifa toka kwa Mzee Mwinyi likiwa KOPO TUPU. Sasa sijui Mzee Mwinyi sifa zake zitakuwa zipi akifa.
Upo uzi humu ukieleza kwa undani legacy ya mzee mwinyi.

Soma comment baada ya comment utajifunza mengi sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…