Rais Magufuli awatumbua Kitila Mkumbo, Ole Sendeka na Katambi, awateua Jumanne Fhika, Dr. Aloyce Nzuki, Allan Kijazi, Josephat Paulo, Kemikimba

Rais Magufuli awatumbua Kitila Mkumbo, Ole Sendeka na Katambi, awateua Jumanne Fhika, Dr. Aloyce Nzuki, Allan Kijazi, Josephat Paulo, Kemikimba

Huu utaratibu wa RAIS MAGUFULI nauunga mkono kwa 100%.

Tena wakikosa huko walikoenda, asiwateue tena. Ili mtu aweze kuifanya kazi yake vizuri, ni muhimu sana aipende, **** hawa wateule wa Rais, hawapendezwi na nafasi walizo nazo. Kwa nini aendelee kuwa nao?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapana imeandikwa ataendelea kukikalia pia ni kam msemaji wa serikali na wakati huohuo ni katibu mkuu wizara ya Mwakyembe
Mzee ebu nielekeze vizuri 🤪🤦
serikalini hata ukiwa unafanyakazi ofisi kumi huwa unalipwa mshahara mmoja tu. Mfano, waziri huwa ni mbunge, angeweza kulipwa mshahara Wa ubunge na Wa uwaziri Ila ukishakuwa waziri unaondolewa kwenye payroll ya bunge, unabaki kulipwa wizarani tu. Bungeni atakuwa analipwa posho za vikao tu. Kwa ishu ya kijazi itaangaliwa kati ya wizarani na Tanapa wapi analipwa mshahara mkubwa, kama ni Tanapa ataendelea na mshahara Wa huko, kama Wa wizara ni mkubwa atalipwa Wa wizara.
 
Kwani Rais kazuia mtu kugombea? Mbona alisema hadharani kabisa tena kwa moyo mweupe anayetaka kugombea aseme yeye hawezi kumzuia, na ndo watu unaona wa naondoka wenyewe. Tukija kwenye swala la tamaa, kiukweli huo ndio uhalisia, wote wanaoacha teuzi na kwenda kugombea ubunge ni tamaa zao za fedha tu, mana kiutendeji mkuu wa Mkoa, wilaya au katibu wa wizara wana eneo kubwa la utendaji na kumsaidia Rais katika majumu yake kuliko hata ubunge... Kwanza Bunge ni mhimili tofauti... Kiukweli ni Tamaa tu.
Sio tamaa tu, hii inahusu pia kuwa kinyume nae kupitia mhimili mwingine!!
 
Naona watu wame bet [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Ova
 
Katambi hana base yoyoye Shinyanga mjini na hajulikani maana 2015 alibebwa tu na nguvu ya Chadema.
Pale mjini GAKI, Fresho na Kwilasa ndio wanaamua mbunge awe nani
Yani wachaga wawili kutoka Machame wanawaamulia nani awe Mbunge huko Usukumani..

Teh teh teh Wachagga wasumbufu sana..
 
Ndio najuanamaanisha kama waziri akigombe tena ubunģe basi na yeye atenguliww uwaziri wake.

Kama unajua, basi unachanganya mambo... au kwa makusudi!

Waziri lazima awe mbunge kwanza, ukimtengua kisa amechukua fomu manake nini... utateua Waziri mwingine kutoka wapi na bunge limevunjwa!
 
Nahisi wengi wanakimbia kufanya kazi chini ya mkuu yaani wanazikimbia stress pia zile Simu za saa nane usiku pia kutumbuka ni nje nje sasa ni bora wakakae mjengoni dodoma jioni anasaini laki tatu posho za makamati na safari za kutosha.
 
Kama unajua, basi unachanganya mambo... au kwa makusudi!

Waziri lazima awe mbunge kwanza, ukimtengua kisa amechukua fomu manake nini... utateua Waziri mwingine kutoka wapi na bunge limevunjwa!
Naibu si yupo?
 
Sasa kwanini huyo Kijazi amebaki na nafasi ya mwanzo? kumekosekana wataalamu wa kupelekwa huko TANAPA? Ila hawa Kina Kijazi wana kismati?
 
Huu utaratibu wa RAIS MAGUFULI nauunga mkono kwa 100%.

Tena wakikosa huko walikoenda, asiwateue tena. Ili mtu aweze kuifanya kazi yake vizuri, ni muhimu sana aipende, **** hawa wateule wa Rais, hawapendezwi na nafasi walizo nazo. Kwa nini aendelee kuwa nao?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kuna walakini,kawaonya hawasikii,katishia kuwatumbua hawasikii vile vile,kawatumbuwa ndio kwanza wanaongeza kasi ya kutia nia.
Hii mass exodus ya wateule wake ni hatari sana kwa serikali yake.Wako tiyari kukosa ubunge kuliko kumtumikia Magufuli.
 
Nini maoni yenu
IMG-20200717-WA0020.jpg
IMG-20200717-WA0021.jpg
 
Huu ni ujumbe kwa Magufuli kwamba watu hawaogopi vitisho. Alitishia mteule wake akigombea anamtumbua na jina lake analikata kwenye Ubunge lakini watu bado wanafukuzana na ndoto zao.

Na October 25 wananchi wanamchinjia baharini kama walivyofanya wateule wake.
 
Hawa wakichaguliwa kuwania ubunge ina maana kwamba walitumwa na JIWE kuchukua fomu kama hawakutumwa basi itabidi awakate juu kwa juu na wasiingine kabisa kwenye top 3.

Ila inabidi mjiulize inawezekana vipi "MINJINO" aachie ukuu wa wilaya aende Ku BET kwenye ubunge bila kuwa na baraka kutoka kwa aliyemnunua?
 
Back
Top Bottom