Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Ingekuwa rais kawaambia baba askofu na waumini wake wachukue mchanga,kokoto,simenti,mabati,rangi halafu waende kwa ndugu zao waislam waujenge huo msikiti Wala tusingesikia kelele Wala migongano..

Nilichogundua hapa Ni huo mchango kuwa pesa watu wanaona wamedharauliwa au Ni aibu kwa dini Fulani...


Ewe ndugu pesa isiitawale nafsi mpk ikapelekea kuingia kwenye dhambi
 
Nimesoma hadi mwisho sijaruka kipengele chochote, japo sikujua kinachoendelea lakini umeelezea vizuri nikapata mwanga,

Binafsi nakazia kwa msumari yote uliyoyaandika, Dini isichanganywe na Siasa.
Ndugu rais, wewe ni Rais siyo sheikh, wewe ni Mkiristu siyo Muislamu, mambo ya Waislamu waachie Waislamu wenyewe!

Una haki ya kuchangisha fedha kwa ajili ya matendo ya imani yako lakini huna haki ya kusimama ndani ya nyumba ya imani yako kudictate kipi kifanywe kwa niaba ya watu wa imani nyingine.

Waislamu wana taratibu zao za kujenga nyumba za Ibada zao, wanachangia wao wenyewe au wanatafuta mfadhili wa imani yao wao wenyewe, au wanafanya kwa kufuata taratibu za dini yao, kisha wanajenga msikiti wao!

Umewahi kusikia wapi Waislamu nchini wameendesha harambee makanisani kwa ajili ya kupata pesa kwa ajili ya kujenga misikiti yao? Au unafikiri Waislamu hawana marafiki Wakiristo wakiwemo maaskofu na mapadre ambao wangeweza kuwaomba wawafanyie harambee wajenge hizo nyumba?

Au lini umewahi kusikia maaskofu na mapadre wameomba michango kupitia misikitini ili Waislamu wachangie ujenzi wa makanisa?

Kuna mambo ni boundary ya kuheshimiana kiimani, nayo ni kutokuingiliana katika namna kila imani inavyoendesha mambo yake!

Najua pengine kibinadamu uliona aibu kutokana na mihela mirefu unayoimwaga makanisani siku hizi kwa jina la sadaka, ukahisi labda umma wa Waislamu utakuona kama mtu anayetumia mafungu yale ya urais yasiyokaguliwa na yeyote kwa ajili ya sadaka hizo, mimi nasema usihofu, maadamu wewe ni Mkatoliki na Mkiristu basi usiuonee haya Ukiristo wako wewe toa tu, Waislamu wanajiweza, wanaweza kujenga misikiti yao wao wenyewe na infact misikiti nchi hii ni mingi kwelikweli na imejengwa na Waislamu wao wenyewe!

Kuhusu misikiti iliyojengwa na Wafalme na marais, hiyo Waislamu tunajua huwa wanatafuta hao wafadhili wao wenyewe, ila sasa kwa kuwa Kiprotokali jambo linalofanywa na mfalme au rais wa Taifa moja katika jingine lazima mfalme au rais wa taifa husika awe na taarifa ndiyo maana taasisi za dini zinaweza kukujulisha ili usaidie kunyoosha mambo! Hii ni tofauti na kwenda kanisani ukaanzisha harambee ya kujenga misikiti! Ndugu Rais ulitumwa au kuombwa na Muislamu gani kutaka kujenga msikiti kupitia fedha za kanisani?

Wakati mwingine naangalia haya mambo na kuona kuwa yamekaa kisiasa. Hata hivyo mambo ya dini ni sensitive sana si vizuri kuchanganya dini na siasa! Mwalimu alionya sana kuhusu mambo haya!

Ipo namna mtu asiye muislamu anavyoweza kuguswa na kuamua kujenga msikiti, kwa mfano, Mwalimu aliguswa moyoni mwake baada ya kustaafu uraisi akaamua kutafuta fedha za kujenga Msikiti Butiama, Mwalimu alikuwa na connection za Vatican, Makanisa makubwa makubwa lakini hakwenda kutafuta fedha makanisani ili ajenge msikiti, Mwalimu alikwenda kwa Ghadafi ndiye aliyempa pesa za kujenga Msikiti huko Butiama!

Nimkumbushe tu ndugu Magufuli kuwa, dini ya Kiislamu pia imeweka misingi ya aina gani ya misikiti inafaa kuswaliwa ndani yake, Quran inasema ile misikiti iliyojengwa kwa dhamira safi ndiyo misikiti ya Mungu na ndiyo inayofaa kuswaliwa bali ile iliyojengwa kwa dhamira isiyo njema, yenye malengomalengo fulani hivi hiyo haina baraka za Mungu na haifai kuswaliwa ndani yake!

Nashauri Ndugu Rais awe makini sana na haya mambo ya dini, haya ni mazito sana, akiyakosea yataiweka heshima nzima ya taasisi ya urais rehani halafu kuja kurekebisha taswira hiyo inaweza kutumia gharama kubwa.

MAMBO YA WAISLAMU WAACHIWE WAISLAMU WENYEWE. NDUGU RAIS FANYA YALE YA IMANI YAKO AU YALE UTAKAYOOMBWA UFANYE KAMA UKIPENDA!
Mambo ya ngazi kubwa kama hizi nashauri waachiwe viongozi wa Ngazi za juu ambao ndiyo wana mamlaka ya kusema kitu juu ya jambo lolote ndani ya inami zao, Masheikh na Ma-Askofu. Tusiwe tunaibuka tu sisi waumini kisa tuna access na mitandoa ya jamii
Kwani harambee hiyo ameifanya wakiwa wapi, Ikulu? Hivi mtu ukishakuwa Rais haki yako kama muumini wa dhehebu fulani inapotea?

Sikumbuki vizuri lakini nadhani kuna kipindi aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mh. Paul Makonda, aliwahi kupata fedha fulani kwa ajili ya ujenzi wa Msikiti hapa Dar es Salaam.

Kama sikosei Mh. Makonda naye pia ni mkristo, na jambo hilo lilipokewa vizuri sana na watanzania wote kwa ujumla, naamini hivyo
 
Quod scripsi, cripsi ...John 19:22 "what i have written, i have written"

What u going to do about it?[emoji3][emoji3]


.
Ndugu rais, wewe ni Rais siyo sheikh, wewe ni Mkiristu siyo Muislamu, mambo ya Waislamu waachie Waislamu wenyewe!

Una haki ya kuchangisha fedha kwa ajili ya matendo ya imani yako lakini huna haki ya kusimama ndani ya nyumba ya imani yako kudictate kipi kifanywe kwa niaba ya watu wa imani nyingine.

Waislamu wana taratibu zao za kujenga nyumba za Ibada zao, wanachangia wao wenyewe au wanatafuta mfadhili wa imani yao wao wenyewe, au wanafanya kwa kufuata taratibu za dini yao, kisha wanajenga msikiti wao!

Umewahi kusikia wapi Waislamu nchini wameendesha harambee makanisani kwa ajili ya kupata pesa kwa ajili ya kujenga misikiti yao? Au unafikiri Waislamu hawana marafiki Wakiristo wakiwemo maaskofu na mapadre ambao wangeweza kuwaomba wawafanyie harambee wajenge hizo nyumba?

Au lini umewahi kusikia maaskofu na mapadre wameomba michango kupitia misikitini ili Waislamu wachangie ujenzi wa makanisa?

Kuna mambo ni boundary ya kuheshimiana kiimani, nayo ni kutokuingiliana katika namna kila imani inavyoendesha mambo yake!

Najua pengine kibinadamu uliona aibu kutokana na mihela mirefu unayoimwaga makanisani siku hizi kwa jina la sadaka, ukahisi labda umma wa Waislamu utakuona kama mtu anayetumia mafungu yale ya urais yasiyokaguliwa na yeyote kwa ajili ya sadaka hizo, mimi nasema usihofu, maadamu wewe ni Mkatoliki na Mkiristu basi usiuonee haya Ukiristo wako wewe toa tu, Waislamu wanajiweza, wanaweza kujenga misikiti yao wao wenyewe na infact misikiti nchi hii ni mingi kwelikweli na imejengwa na Waislamu wao wenyewe!

Kuhusu misikiti iliyojengwa na Wafalme na marais, hiyo Waislamu tunajua huwa wanatafuta hao wafadhili wao wenyewe, ila sasa kwa kuwa Kiprotokali jambo linalofanywa na mfalme au rais wa Taifa moja katika jingine lazima mfalme au rais wa taifa husika awe na taarifa ndiyo maana taasisi za dini zinaweza kukujulisha ili usaidie kunyoosha mambo! Hii ni tofauti na kwenda kanisani ukaanzisha harambee ya kujenga misikiti! Ndugu Rais ulitumwa au kuombwa na Muislamu gani kutaka kujenga msikiti kupitia fedha za kanisani?

Wakati mwingine naangalia haya mambo na kuona kuwa yamekaa kisiasa. Hata hivyo mambo ya dini ni sensitive sana si vizuri kuchanganya dini na siasa! Mwalimu alionya sana kuhusu mambo haya!

Ipo namna mtu asiye muislamu anavyoweza kuguswa na kuamua kujenga msikiti, kwa mfano, Mwalimu aliguswa moyoni mwake baada ya kustaafu uraisi akaamua kutafuta fedha za kujenga Msikiti Butiama, Mwalimu alikuwa na connection za Vatican, Makanisa makubwa makubwa lakini hakwenda kutafuta fedha makanisani ili ajenge msikiti, Mwalimu alikwenda kwa Ghadafi ndiye aliyempa pesa za kujenga Msikiti huko Butiama!

Nimkumbushe tu ndugu Magufuli kuwa, dini ya Kiislamu pia imeweka misingi ya aina gani ya misikiti inafaa kuswaliwa ndani yake, Quran inasema ile misikiti iliyojengwa kwa dhamira safi ndiyo misikiti ya Mungu na ndiyo inayofaa kuswaliwa bali ile iliyojengwa kwa dhamira isiyo njema, yenye malengomalengo fulani hivi hiyo haina baraka za Mungu na haifai kuswaliwa ndani yake!

Nashauri Ndugu Rais awe makini sana na haya mambo ya dini, haya ni mazito sana, akiyakosea yataiweka heshima nzima ya taasisi ya urais rehani halafu kuja kurekebisha taswira hiyo inaweza kutumia gharama kubwa.

MAMBO YA WAISLAMU WAACHIWE WAISLAMU WENYEWE. NDUGU RAIS FANYA YALE YA IMANI YAKO AU YALE UTAKAYOOMBWA UFANYE KAMA UKIPENDA!
 
Pamoja na Wakristo kulilalamikia hili but ili ionekane sio sawa then zikataeni zile pesa, zikija tu, zipigeni chini, tutaona malalamiko yenu yana maana.
 
Wanadai wamefanya makubwa, wamefanya siasa miaka mitano peke yao lakini bado wanawazuia wanahabar kuripoti habari za wapinzani. Ukweli haujifichi utafanya propaganda lakini watu kama hawakupendi hawakupendi tu
 
Wenye dini yao wala hawana tatizo na hilo suala la michango. Nchi yetu sote hii na wala sio mara ya kwanza kuchangiana ujenzi wa makanisa na misikiti. Tatizo kila jambo linachanganywa na siasa.

Ni juzi tu Joketi Mwogelo Mkuu wa Wilaya Kisarawe amechagua ujenzi wa Msikiti na Waislamu wenyewe wamechagua kuwa mlezi wa kamati ya ujenzi.
Alikuwa kanisani?
 
Ukisoma between lines - mwandishi - Ana chuki isiyopimika dhidi ya wakatoliki.
Mwandishi anaumia sana kumuona Rais anatoa sadaka kanisani.
Hili la kuchangiana si hoja yake ya msingi. Ila imempa upenyo tu kuventi chuki yake dhidi ya wakatoliki.
Rais ni kiongozi wa nchi. Anaongoza wakristo, waislam na hata wasio na dini.
Ana jukumu la kuwaunganisha wote waishi kindugu, kuthaminiana, kuheshimiana na kusaidiana.
Mwandishi asingetumia chuki yake dhidi ya ukatoliki angeweza kuiona dhamira njema ya Rais kutuunganisha na kutufanya tuishi kitanzania - tukipendana na kushirikiana bila kujali tofauti zetu kiimani, kikabila nk.
Sisi ni WATANZANIA na ni NDUGU.
There is no way, again there is no way and never there will be mapenzi ya wakristo kwa waislam

Qur an imeshasema zamani sana mambo haya.

Walipofikia waislam wa Tanzania moja ya chanzo ni chuki ya wakristo hususan wakatoliki dhidi ya waislam.

Mengi sana yashasemwa juu ya hili na hakuna na hakutokuwepo mapenzi haya yanayoonyeshwa isipokuwa ni jambo/mambo tu yanafanywa kwa maslahi flani
 
Mambo ya ngazi kubwa kama hizi nashauri waachiwe viongozi wa Ngazi za juu ambao ndiyo wana mamlaka ya kusema kitu juu ya jambo lolote ndani ya inami zao, Masheikh na Ma-Askofu. Tusiwe tunaibuka tu sisi waumini kisa tuna access na mitandoa ya jamii
Kwani harambee hiyo ameifanya wakiwa wapi, Ikulu? Hivi mtu ukishakuwa Rais haki yako kama muumini wa dhehebu fulani inapotea? Sikumbuki vizuri lakini nadhani kuna kipindi aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mh. Paul Makonda, aliwahi kupata fedha fulani kwa ajili ya ujenzi wa Msikiti hapa Dar es Salaam. Kama sikosei Mh. Makonda naye pia ni mkristo, na jambo hilo lilipokewa vizuri sana na watanzania wote kwa ujumla, naamini hivyo
ELIMU ELIMU ELIMU
 
Back
Top Bottom