Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Natamani ausome huu waraka umeandika fact tupu
 
Hiyo ni 'sunna' siyo 'faradha', Mkuu. Allah ndiye atakaye muhukumu kwa tendo hili. Ila nina imani. Allah amefurahishwa kwa namna 'watu wa kitabu' wanavyomthamini.

Pole kwa kutolijua hili kabla.
Watu wa kitabu??? Hahahahaahahahahaha

Ahlul kitaab ni watu wa zaburi (ya kweli), injili (ya kweli) na tauraat (ya kweli).

Sio watu wa biblia mkuu hahahahaahahahhah
 
Kuna majengo (misikiti) iliharamishwa kuswaliwa bali ilijengwa na waislam (wanafiki) seuze mshirikina? Tupunguzieni maajabu awamu hii wandugu! Mnaona fahari kuvunja recod hata za kutia madoa? Acheni acheni acheni.
Haswaaa
 
We mtoa post umekosea sana na udini unakusumbua,nataka tu kukukumbusha kwamba Rais ni kiongozi wa nchi na nchi haina dini
Rais anaruhusuliwa kuchangia dini yeyote kadri atakavyojisikia .shida ni sehemu aliyotumia kuchangia hiyo pesa .huwezi kusimama Kwenye madhabahu alafu eti ukanzisha harambee yakuwachangia waislamu.sio sawa kabisa.Angekuwa anazo zakumtosha alitakiwa aombe kwa Paroko kuwa ibada ikiisha anaomba waongozane mpk hapo kwa Jirani anataka kufanya harambee kidogo nae Jirani akue. Lkn so kama alvyo fanya kuchangisha ndani ya kanisa tena madhabahuni.
 
Someni ufunuo sura ya Tisa panahistotia ya kiunabii kuhusu uislamu na ukatoriki(jihad and crusade) dini hizi mbili ni mahasimu wa muda mrefu na historia iliyowazi sana.kwa kilchofanyika Islamic wa zamani wasingekubari kabisa,hawa was Leo wanshida sehemu
 
Uko sahihi, hata Dar aliwaombea kwa Mfalme wa Morocco wajengewe msikiti wa kisasa. Na tayari umekamilika!
 
Mkuu,

Unaonekana ni mtu wa maana sana. Sina uhakika na hilo. But yeah at least unaonekana ni mtu!

Unajua mimi sijasema kwamba huu mchukiano ni two way traffic, kaa yupo anaesema hivyo aje atoe hoja zake.

Mimi ninachosema historia ya nchi yetu ni kwamba wakristo hususan wakatoliki wamekuwa wakiwachukia waislam (historically) na labda niseme hili ni tatizo la kimfumo zaidi kuliko individuals maana sote tunaishi vizuri kwa nje.

Hoja ikaja kwamba, aliyoyafanya Mheshimiwa rais magufuli ndio yanapingwa hapa na mimi nikafikia kuelezea kwamba hakutokuwa kamwe na mapenzi hayo ambayo yeye Mheshimiwa rais ametaka kuya portray kwa sababu chuki kutoka kwao (wakristo hususan wakatoliki) kwa uislam au waislam ni kubwa zaidi kuliko mapenzi yao.

Hebu imagine tu brother, katika umri wako na pengine kwa elimu yako eti Leo ndio Unamjua Sheikh Suleiman Takadir?? Sikulaumu mkuu ni mfumo ndio uliopelekea hivyo. Kwa hiyo lililofanyika ni geresha tu au danganya toto na wala si kwa mapenzi ya dhati ya wakristo juu ya uislam. Ukweli ni ule aliousema GWAJIMA juu ya miskiti, kwamba ataugeuza kuwa Sunday schools ile ni chuki ya hali ya juu na yale ni machache tu aliyoyasema ambayo kwa chuki ilimvyomjaa alishindwa kuendelea kukaa nayo moyoni.

Allah anatuambia kwamba ubaya wao (makafiri) waudhihirishao dhidi yetu (waislam) ni mdogo mno ukilinganisha na ule waufichao vifuani mwao.

Ukweli ni ule wa waziri lukuvi juu ya kauli anazozitoa kuhusu Zanzibar na mengine mengi mno mno mno mno.

Kwa hiyo ndugu yangu kimfumo, huu upendo kamwe hautokuwepo. Ile kuchangisha pesa ni geresha tu au nyinyi mnaita siasa tu.
 
Ndani ya miaka 5 hii ndio wahadhiri wakuu na waandamizi na baadhi ya wafanyakazi wa UDOM waliondolewa wote wakiwa ni waislam (kwa chuki za kidini) na kuwa replaced na wote waliokuwa sio waislam (kwa maslahi ya kidini).

Una hoja?
 
Ukiwa kanisani,mtaani au huko msikitini?
Hahaha usichotaka ni nini, pesa yangu au dhehebu langu au kanisa ninalo sali?
Mbona tunapoombwa michango sisi hatujali kiivyo, nyie mna mind nini sasa?!

Jijengeeni misikiti na ofisi zenu msiombe ombe.
 
Nimesoma hadi mwisho sijaruka kipengele chochote, japo sikujua kinachoendelea lakini umeelezea vizuri nikapata mwanga,

Binafsi nakazia kwa msumari yote uliyoyaandika, Dini isichanganywe na Siasa.
Hilo linafanyiwa kazi kwa upinzani lkn ccm kwao ni ruksa kuchanganya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…