Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Sasa kama hajatumwa kipi kilimpelekea kufanya harambee? Washauri wake feki ama? hebu kuweni seriaz hili jambo ni kubwa mno
 
Hujaelewa kinachojadiliwa wewe.kaa pembeni nna kadegree kako ka kudesa huko mwalimu nyerere


Inawezekana ni kweli sijaelewa aisee [emoji3][emoji3]

Sasa Naomba nisaidie kuelewa kwa kifupi hoja ya za msingi ni zipi ?

Je mleta mada msingi wa madai yake ni nini?
 
Sisi waislam ndio hatuna chuki haswa dhidi ya ndugu zetu wasio waislam. Tumekuwa tukifuata mafundisho ya dini yetu juu ya wenzetu wasio waislam ingawaje sasa mara zote tumekuwa victims wa wema wetu huo.

That being said, tunapojitenga na wasio waislam ni huwa tu tunachkuwa tahadhari and nothing more.

Mimi pia naamini wakristo wema wapo wengi tu na nimeishi nao na ni wenzangu mpaka Leo.
 
Serikali inakusanya kodi toka Kwa watu wa dini zote na wasio na dini, sasa iweje wa dini fulani wapewe mali ya serikali?
ukiona hvyo favor upande wa pili umezidi, ngoja nikupe mfano kaskazin huku kuna sehemu hamna hospital ya serikal ni za kanisa tu nisaidie jibu kwanini serikal wasiweke hosptala zao, halaf uje na hyo inshu ya chuo
 
Bibi yangu aliwahi kuniambia ukiwa na roho mbaya kwa watu wasiokua wa familia yako na ukawa unawatendea mabaya ipo siku tabia hiyo itakomaa na utajikuta unawatendea hayohayo wanao. Yaani wapinzani wa nchi hii sijui kwa hizo chuki ni waumini wa dini gani maana hawana jema, hawataki amani, furaha wa utulivu.
Huku mtaani tumekutana na madaftari ya kuchangisha kujengea misikiti kila siku na ukichanga huulizwi dini yako... ila leo rais kuchangisha msikiti wa chamwino ujengwe ishakua nongwa. Mungu atusamehe
 
Kwani Uislamu unasemaje juu ya hili ?
 
Hivi mbona mnapindisha hoja??

Wapinzani ni nani kwanza?? Mimi ni CCM enzi na enzi lakini hili nalipinga. Je ni mpinzani???

Waislam kuchangishiwa hela za kujengea msikiti ndani ya KANISA ndio hoja hapa.

Tena zaidi inasemekana raid hakuombwa na hao waislam akawachangishie nyinyi huko mitaani huwa mnaombwa.

Hebu acheni ukasuku nyie watu
 
Kama wewe ni Mkristo kasome Vizuri Biblia yako na kama ni Mwislam rudia kusoma Quruan uje ulete mrejesho hapa usijibu kimhemko
 
Kuna mtu hapa anaitwa TUJITEGEMEE alikuwa anataka elimu juu ya ahlul kitaab akiwahusisha wakristo wa sasa kuwa ahlul kitaab. Mimi nimemwambia sina elimu nalo kubwa ndio maana nkakuita mkuu

Wakristo na Mayahudi wote ni "ahlul kitaab" hii ndiyo kauli yenye nguvu, japokuwa kuna baadhi ya wasomi wanasema hakuna "ahlul kitaab" zama hizi, ila kwa dalili kadha wa kadha katika Qur'aan a Hadithi zinaonyesha watu hao bado wapo, sababu wanayo yafanya leo ndiyo yale yale yaliyokemewa tangu mtue yuko hao, mfano wa suala la kudai Yesu ni Mungu, kadhalika suala la Utatu mtakatifu.

Kwa maana nyepesi ni kuwa "ahlul kitaab" ni wsle wote wanaojinasibisha na dini hizo mbili yaani Ukristo na Uyahudi.
 
Kumbe hata kwa mujibu wa ukristo ni dhambi ?

Mara nyingi huwa nadhani ukristo hauko na miiko kama uislamu.

hata katika uisamu haifai pia.
Yaani haifai waislamu kuchanga pesa ili kujenga jengo la ibada yeyote ambayo itafanyika kinyume na Allah.

Hofu yangu kuna siku atakuja msikitini kufanya mchango wa kanisa.
 


Msikilize Mufti, au ww unajua uislam kuliko Mufti.? Ww sio msemaji wa Waislam, hivyo sio mtu sahihi kuzungumzia ya waislam hata kidogo.

Mh. Rais Magufuli, songa mbele, supporter wako tuko wengi zaidi ya wanao kupinga, na Mh. Rais nikutie moyo, hata Yesu alikataliwa na binadamu hawa hawa, hivyo hata utende wema kiwango gani bado wako watakao kupinga tu. Hivyo usikate tamaa hata kidogo.






Wivu utawamaliza jamani, Mh. Rais hakuanza jana au juzi kusaidia ujenzi wa misikiti au makanisa...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…