Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Sasa kama hajatumwa kipi kilimpelekea kufanya harambee? Washauri wake feki ama? hebu kuweni seriaz hili jambo ni kubwa mno
 
Hujaelewa kinachojadiliwa wewe.kaa pembeni nna kadegree kako ka kudesa huko mwalimu nyerere


Inawezekana ni kweli sijaelewa aisee [emoji3][emoji3]

Sasa Naomba nisaidie kuelewa kwa kifupi hoja ya za msingi ni zipi ?

Je mleta mada msingi wa madai yake ni nini?
 
Mimi siwezi kuwa na chuki na mtu yeyote Eti sababu dini yake na yangu tofauti hiyo hapana!

Nimejifunza upendo kwa watu wote waloumbwa na Mwenyezi Mungu sababu kwa kufanya hivyo namheshimu aliyewaumba ambaye ni Mungu!

Kwanza mimi mzazi wangu mmoja ni Muislam kwa taarifa yako!

Mimi bado naamini waislam waelewa wapo wengi Ila kuna kundi fulani Ndiyo linataka ubaguzi wa kidini!

Sijui kwanini mnapenda kujiona watakatifu wakati mna yenu kibao [emoji108]

Aso hili ana lile!

Mtu anaweza kuwa hanywi pombe au hali nguruwe n.k lakini mshirikina mkubwa, mchawi, mfuga majini, mzinzi n.k

Siyo siri uzi huu nimejifunza kitu!
Sisi waislam ndio hatuna chuki haswa dhidi ya ndugu zetu wasio waislam. Tumekuwa tukifuata mafundisho ya dini yetu juu ya wenzetu wasio waislam ingawaje sasa mara zote tumekuwa victims wa wema wetu huo.

That being said, tunapojitenga na wasio waislam ni huwa tu tunachkuwa tahadhari and nothing more.

Mimi pia naamini wakristo wema wapo wengi tu na nimeishi nao na ni wenzangu mpaka Leo.
 
Serikali inakusanya kodi toka Kwa watu wa dini zote na wasio na dini, sasa iweje wa dini fulani wapewe mali ya serikali?
ukiona hvyo favor upande wa pili umezidi, ngoja nikupe mfano kaskazin huku kuna sehemu hamna hospital ya serikal ni za kanisa tu nisaidie jibu kwanini serikal wasiweke hosptala zao, halaf uje na hyo inshu ya chuo
 
Bibi yangu aliwahi kuniambia ukiwa na roho mbaya kwa watu wasiokua wa familia yako na ukawa unawatendea mabaya ipo siku tabia hiyo itakomaa na utajikuta unawatendea hayohayo wanao. Yaani wapinzani wa nchi hii sijui kwa hizo chuki ni waumini wa dini gani maana hawana jema, hawataki amani, furaha wa utulivu.
Huku mtaani tumekutana na madaftari ya kuchangisha kujengea misikiti kila siku na ukichanga huulizwi dini yako... ila leo rais kuchangisha msikiti wa chamwino ujengwe ishakua nongwa. Mungu atusamehe
 
Ndugu rais, wewe ni Rais siyo sheikh, wewe ni Mkiristu siyo Muislamu, mambo ya Waislamu waachie Waislamu wenyewe!

Una haki ya kuchangisha fedha kwa ajili ya matendo ya imani yako lakini huna haki ya kusimama ndani ya nyumba ya imani yako kudictate kipi kifanywe kwa niaba ya watu wa imani nyingine.

Waislamu wana taratibu zao za kujenga nyumba za Ibada zao, wanachangia wao wenyewe au wanatafuta mfadhili wa imani yao wao wenyewe, au wanafanya kwa kufuata taratibu za dini yao, kisha wanajenga msikiti wao!

Umewahi kusikia wapi Waislamu nchini wameendesha harambee makanisani kwa ajili ya kupata pesa kwa ajili ya kujenga misikiti yao? Au unafikiri Waislamu hawana marafiki Wakiristo wakiwemo maaskofu na mapadre ambao wangeweza kuwaomba wawafanyie harambee wajenge hizo nyumba?

Au lini umewahi kusikia maaskofu na mapadre wameomba michango kupitia misikitini ili Waislamu wachangie ujenzi wa makanisa?

Kuna mambo ni boundary ya kuheshimiana kiimani, nayo ni kutokuingiliana katika namna kila imani inavyoendesha mambo yake!

Najua pengine kibinadamu uliona aibu kutokana na mihela mirefu unayoimwaga makanisani siku hizi kwa jina la sadaka, ukahisi labda umma wa Waislamu utakuona kama mtu anayetumia mafungu yale ya urais yasiyokaguliwa na yeyote kwa ajili ya sadaka hizo, mimi nasema usihofu, maadamu wewe ni Mkatoliki na Mkiristu basi usiuonee haya Ukiristo wako wewe toa tu, Waislamu wanajiweza, wanaweza kujenga misikiti yao wao wenyewe na infact misikiti nchi hii ni mingi kwelikweli na imejengwa na Waislamu wao wenyewe!

Kuhusu misikiti iliyojengwa na Wafalme na marais, hiyo Waislamu tunajua huwa wanatafuta hao wafadhili wao wenyewe, ila sasa kwa kuwa Kiprotokali jambo linalofanywa na mfalme au rais wa Taifa moja katika jingine lazima mfalme au rais wa taifa husika awe na taarifa ndiyo maana taasisi za dini zinaweza kukujulisha ili usaidie kunyoosha mambo! Hii ni tofauti na kwenda kanisani ukaanzisha harambee ya kujenga misikiti! Ndugu Rais ulitumwa au kuombwa na Muislamu gani kutaka kujenga msikiti kupitia fedha za kanisani?

Wakati mwingine naangalia haya mambo na kuona kuwa yamekaa kisiasa. Hata hivyo mambo ya dini ni sensitive sana si vizuri kuchanganya dini na siasa! Mwalimu alionya sana kuhusu mambo haya!

Ipo namna mtu asiye muislamu anavyoweza kuguswa na kuamua kujenga msikiti, kwa mfano, Mwalimu aliguswa moyoni mwake baada ya kustaafu uraisi akaamua kutafuta fedha za kujenga Msikiti Butiama, Mwalimu alikuwa na connection za Vatican, Makanisa makubwa makubwa lakini hakwenda kutafuta fedha makanisani ili ajenge msikiti, Mwalimu alikwenda kwa Ghadafi ndiye aliyempa pesa za kujenga Msikiti huko Butiama!

Nimkumbushe tu ndugu Magufuli kuwa, dini ya Kiislamu pia imeweka misingi ya aina gani ya misikiti inafaa kuswaliwa ndani yake, Quran inasema ile misikiti iliyojengwa kwa dhamira safi ndiyo misikiti ya Mungu na ndiyo inayofaa kuswaliwa bali ile iliyojengwa kwa dhamira isiyo njema, yenye malengomalengo fulani hivi hiyo haina baraka za Mungu na haifai kuswaliwa ndani yake!

Nashauri Ndugu Rais awe makini sana na haya mambo ya dini, haya ni mazito sana, akiyakosea yataiweka heshima nzima ya taasisi ya urais rehani halafu kuja kurekebisha taswira hiyo inaweza kutumia gharama kubwa.

MAMBO YA WAISLAMU WAACHIWE WAISLAMU WENYEWE. NDUGU RAIS FANYA YALE YA IMANI YAKO AU YALE UTAKAYOOMBWA UFANYE KAMA UKIPENDA!
Kwani Uislamu unasemaje juu ya hili ?
 
Bibi yangu aliwahi kuniambia ukiwa na roho mbaya kwa watu wasiokua wa familia yako na ukawa unawatendea mabaya ipo siku tabia hiyo itakomaa na utajikuta unawatendea hayohayo wanao. Yaani wapinzani wa nchi hii sijui ni waumini wa dini gani maana hawana jema, hawataki amani, furaha wa utulivu.
Huku mtaani tumekutana na madaftari ya kuchangisha kujengea misikiti kila siku na ukichanga huulizwi dini yako... ila leo rais kuchangisha msikiti wa chamwino ujengwe ishakua nongwa. Mungu atusamehe
Hivi mbona mnapindisha hoja??

Wapinzani ni nani kwanza?? Mimi ni CCM enzi na enzi lakini hili nalipinga. Je ni mpinzani???

Waislam kuchangishiwa hela za kujengea msikiti ndani ya KANISA ndio hoja hapa.

Tena zaidi inasemekana raid hakuombwa na hao waislam akawachangishie nyinyi huko mitaani huwa mnaombwa.

Hebu acheni ukasuku nyie watu
 
Bibi yangu aliwahi kuniambia ukiwa na roho mbaya kwa watu wasiokua wa familia yako na ukawa unawatendea mabaya ipo siku tabia hiyo itakomaa na utajikuta unawatendea hayohayo wanao. Yaani wapinzani wa nchi hii sijui kwa hizo chuki ni waumini wa dini gani maana hawana jema, hawataki amani, furaha wa utulivu.
Huku mtaani tumekutana na madaftari ya kuchangisha kujengea misikiti kila siku na ukichanga huulizwi dini yako... ila leo rais kuchangisha msikiti wa chamwino ujengwe ishakua nongwa. Mungu atusamehe
Kama wewe ni Mkristo kasome Vizuri Biblia yako na kama ni Mwislam rudia kusoma Quruan uje ulete mrejesho hapa usijibu kimhemko
 
Kuna mtu hapa anaitwa TUJITEGEMEE alikuwa anataka elimu juu ya ahlul kitaab akiwahusisha wakristo wa sasa kuwa ahlul kitaab. Mimi nimemwambia sina elimu nalo kubwa ndio maana nkakuita mkuu

Wakristo na Mayahudi wote ni "ahlul kitaab" hii ndiyo kauli yenye nguvu, japokuwa kuna baadhi ya wasomi wanasema hakuna "ahlul kitaab" zama hizi, ila kwa dalili kadha wa kadha katika Qur'aan a Hadithi zinaonyesha watu hao bado wapo, sababu wanayo yafanya leo ndiyo yale yale yaliyokemewa tangu mtue yuko hao, mfano wa suala la kudai Yesu ni Mungu, kadhalika suala la Utatu mtakatifu.

Kwa maana nyepesi ni kuwa "ahlul kitaab" ni wsle wote wanaojinasibisha na dini hizo mbili yaani Ukristo na Uyahudi.
 
Kingine sina Hakika kama Mungu wa waislamu ndo Mungu wa Wakristo.

Hapa mtu unaweza ukajikuta unachuma dhambi bila kujua.

Sisi wakristo tunajua Mungu wetu ni Mungu mwenye wivu. Siwezi kuchangia ujenzi wa msikiti au ujenzi wa shaulin temple ili Mungu mwingine aka abudiwe. Kwa imani yangu iyo ni dhambi.
Kumbe hata kwa mujibu wa ukristo ni dhambi ?

Mara nyingi huwa nadhani ukristo hauko na miiko kama uislamu.

hata katika uisamu haifai pia.
Yaani haifai waislamu kuchanga pesa ili kujenga jengo la ibada yeyote ambayo itafanyika kinyume na Allah.

Hofu yangu kuna siku atakuja msikitini kufanya mchango wa kanisa.
 
Ndugu rais, wewe ni Rais siyo sheikh, wewe ni Mkiristu siyo Muislamu, mambo ya Waislamu waachie Waislamu wenyewe!

Una haki ya kuchangisha fedha kwa ajili ya matendo ya imani yako lakini huna haki ya kusimama ndani ya nyumba ya imani yako kudictate kipi kifanywe kwa niaba ya watu wa imani nyingine.

Waislamu wana taratibu zao za kujenga nyumba za Ibada zao, wanachangia wao wenyewe au wanatafuta mfadhili wa imani yao wao wenyewe, au wanafanya kwa kufuata taratibu za dini yao, kisha wanajenga msikiti wao!

Umewahi kusikia wapi Waislamu nchini wameendesha harambee makanisani kwa ajili ya kupata pesa kwa ajili ya kujenga misikiti yao? Au unafikiri Waislamu hawana marafiki Wakiristo wakiwemo maaskofu na mapadre ambao wangeweza kuwaomba wawafanyie harambee wajenge hizo nyumba?

Au lini umewahi kusikia maaskofu na mapadre wameomba michango kupitia misikitini ili Waislamu wachangie ujenzi wa makanisa?

Kuna mambo ni boundary ya kuheshimiana kiimani, nayo ni kutokuingiliana katika namna kila imani inavyoendesha mambo yake!

Najua pengine kibinadamu uliona aibu kutokana na mihela mirefu unayoimwaga makanisani siku hizi kwa jina la sadaka, ukahisi labda umma wa Waislamu utakuona kama mtu anayetumia mafungu yale ya urais yasiyokaguliwa na yeyote kwa ajili ya sadaka hizo, mimi nasema usihofu, maadamu wewe ni Mkatoliki na Mkiristu basi usiuonee haya Ukiristo wako wewe toa tu, Waislamu wanajiweza, wanaweza kujenga misikiti yao wao wenyewe na infact misikiti nchi hii ni mingi kwelikweli na imejengwa na Waislamu wao wenyewe!

Kuhusu misikiti iliyojengwa na Wafalme na marais, hiyo Waislamu tunajua huwa wanatafuta hao wafadhili wao wenyewe, ila sasa kwa kuwa Kiprotokali jambo linalofanywa na mfalme au rais wa Taifa moja katika jingine lazima mfalme au rais wa taifa husika awe na taarifa ndiyo maana taasisi za dini zinaweza kukujulisha ili usaidie kunyoosha mambo! Hii ni tofauti na kwenda kanisani ukaanzisha harambee ya kujenga misikiti! Ndugu Rais ulitumwa au kuombwa na Muislamu gani kutaka kujenga msikiti kupitia fedha za kanisani?

Wakati mwingine naangalia haya mambo na kuona kuwa yamekaa kisiasa. Hata hivyo mambo ya dini ni sensitive sana si vizuri kuchanganya dini na siasa! Mwalimu alionya sana kuhusu mambo haya!

Ipo namna mtu asiye muislamu anavyoweza kuguswa na kuamua kujenga msikiti, kwa mfano, Mwalimu aliguswa moyoni mwake baada ya kustaafu uraisi akaamua kutafuta fedha za kujenga Msikiti Butiama, Mwalimu alikuwa na connection za Vatican, Makanisa makubwa makubwa lakini hakwenda kutafuta fedha makanisani ili ajenge msikiti, Mwalimu alikwenda kwa Ghadafi ndiye aliyempa pesa za kujenga Msikiti huko Butiama!

Nimkumbushe tu ndugu Magufuli kuwa, dini ya Kiislamu pia imeweka misingi ya aina gani ya misikiti inafaa kuswaliwa ndani yake, Quran inasema ile misikiti iliyojengwa kwa dhamira safi ndiyo misikiti ya Mungu na ndiyo inayofaa kuswaliwa bali ile iliyojengwa kwa dhamira isiyo njema, yenye malengomalengo fulani hivi hiyo haina baraka za Mungu na haifai kuswaliwa ndani yake!

Nashauri Ndugu Rais awe makini sana na haya mambo ya dini, haya ni mazito sana, akiyakosea yataiweka heshima nzima ya taasisi ya urais rehani halafu kuja kurekebisha taswira hiyo inaweza kutumia gharama kubwa.

MAMBO YA WAISLAMU WAACHIWE WAISLAMU WENYEWE. NDUGU RAIS FANYA YALE YA IMANI YAKO AU YALE UTAKAYOOMBWA UFANYE KAMA UKIPENDA!


Msikilize Mufti, au ww unajua uislam kuliko Mufti.? Ww sio msemaji wa Waislam, hivyo sio mtu sahihi kuzungumzia ya waislam hata kidogo.

Mh. Rais Magufuli, songa mbele, supporter wako tuko wengi zaidi ya wanao kupinga, na Mh. Rais nikutie moyo, hata Yesu alikataliwa na binadamu hawa hawa, hivyo hata utende wema kiwango gani bado wako watakao kupinga tu. Hivyo usikate tamaa hata kidogo.









Wivu utawamaliza jamani, Mh. Rais hakuanza jana au juzi kusaidia ujenzi wa misikiti au makanisa...
 
Back
Top Bottom