Rais Magufuli: Hakuna Lockdown kwa Dar wala Tanzania, NEVER! Tusiwatishe watanzania, hofu ni ugonjwa mkubwa kuliko Corona

Out of topic: Baada ya TBC kuzingua, naangalia Clouds TV, kuna mtangazaji anasema tunaweza kukata TShirt kutengeza barakoa, ili mradi tu iwe ni kitambaa cha katani (ambayo ameiita cotton kwa kiingereza).

Swali: Katani ndiyo Cotton?
Hahahahahah

Senti bai yuzingi tecno T301
 
Out of topic: Baada ya TBC kuzingua, naangalia Clouds TV, kuna mtangazaji anasema tunaweza kukata TShirt kutengeza barakoa, ili mradi tu iwe ni kitambaa cha katani (ambayo ameiita cotton kwa kiingereza).

Swali: Katani ndiyo Cotton?
Cotton ni pamba mkuu,hiyo TV hakuna "weledi" na wala hawajitambui,huwa nikiwa huko nyumbani Tz nawakataza familia kuiangalia.
 
Watu naona wana chuki tu na raisi wetu wengi hawajui rais anaweza kuhutubia taifa hata akiwa mkoa wowote wa tanzania na mahali popote tanzania mfano kila mkoa kuna ikulu ya rais

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rudini TBC wamerudi tena.

Amesema siyo kununua barakoa kila nchi kuna barakoa zingine zinakuja na corona.

Amesema kuna watu wanataka Dar iwe lockdown "never haifungwi ni senta ya kila kitu

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Corona kiboko mtu kaamua kujichimbia mafichoni. Inawezekana zile cases za TBC ndo zimemtisha mtu akajua haka sio kaugonjwa bali ni liugonjwa
 
Amesema takwimu za wanaopona zitangazwe ,leo wametangaza cases zote 284 lakini zaidi ya 100 wamepona mbona haitangazwi

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…