Rais Magufuli: Hakuna Lockdown kwa Dar wala Tanzania, NEVER! Tusiwatishe watanzania, hofu ni ugonjwa mkubwa kuliko Corona

cheki anachoongea usiteme pumba
 
Magufuli kama Xi Ping kabisa. Anasema wanaoandika kwenye social media kusema watu waliukufa kwa Coronavirus wafatiliwe. IGP kapewa Lungu.
Safi wanunue mtambo wa kisasa wafatilie mpaka huku jf [emoji23][emoji1787][emoji2960]

Sent from my Infinix X624 using Tapatalk
 
Ila hata mimi kwenye suala la lockdown na kuhusu kutishana namuunga mkono mzee baba...vifo vya watu 10 haviwezi kututisha kama taifa...cha muhimu ni tahadhari tu na njia mbadala nyingi zitolewe
 
Rais: Taarifa zitatolewa na Waziri Mkuu, Waziri wa Afya au ... (sijasikia vizuri wa tatu ni nani).
 
Rais: Anasema wizara iseme ukweli, data za wanaopona yeye anazo ni zaidi ya 100, ila eti imetajwa 11 tu.

Rais: Kwenye mitandao inaonekana namba za simu nyingi siyo za Tanzania, zinatumika kutangaza uongo na kuleta taharuki.
Sasa yeye yupo mbali huko,anabishana na walio Jikoni!!!!🤣🤣🤣
 
Ukweli watu wengi wanaongea bila facts, wengi tu ni waropokaji na hawana takwimu zozote. Ilà kwa vile ni nchi huru kila mtu anabwabwaja anavyotaka.

Tahadhari ni lazima kila mtu achukue, the man is right on point. Tusipofanya kazi wengine tutakufa, wengi wanalilia hiyo total lockdown lakini raia wa mataifa makubwa huko duniani wanashawishi serikali zao watoke wakafanye kazi, sisi kwa uvivu wetu tunataka tufungiwe ndani.
 
Don niacheee pliiiiz sitaki kucheka jamani. Tuendelee kumuomba Mwenyezi Munguz atatusaidia sana, hawezi kutuacha, cause anatupenda... scientifically miili yetu itakua resistant tu. Ni mapito!

Sure. Rais anasema anafurahi vyombo vya usalama kupambana na corona kama vita nyingine.

Na wananchi msipokee kitu chochote kinachoweza kuwa chanzo cha corona.

Sasa sijui hapa anawazungumzia wanaotoa misaada ya vifaa.
 
This is very low opinion mkuu. Karne ya 21 unauliza anaongozaje nchi akiwa chato? Viongozi wa un wamekutana via vid wengine wakiwa majikoni mwao. Live na mkutano unaenda!
Ofisi ya Rais Huwezi kuihamishia sebuleni kwako.
 
Rais John Magufuli ameitaka Wizara ya Afya itoe takwimu za kweli kuhusu maambukizi ya corona ikiwa ni pamoja na kutangaza takwimu sahihi za watu wanaopona ili kuondoa hofu kwa Watanzania.

Kwa mujibu wa Rais idadi ya watu waliopona ni ndogo kuliko hali halisi na kwamba, ana taarifa kuwa hadi wakati Waziri Mkuu alipotangaza idadi ya watu walioambukizwa, waliopoteza maisha na waliopona zaidi ya watu 100 walikuwa wamepona.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…