Tanzania ipo kwenye soft lockdown na ndio maana shughuli zingine muhimu za kiuchumi zaendelea kama kawaida.
Pia, katika soft lockdown hiyo mji wa Dar -es-Salaam unapaswa uendelee na shughuli zote za kiuchumi kuingiza mapato ya serikali yetu maskini.
Hiyo ni kutokana na sababu za kijiografia kwani tuna bandari inayopitisha mizigo ya nchi jirani, wataka tuzuie hiyo mizigo na tusipate ushuru?
Hizo nchi utajazo kama Uingereza wao mpaka sasa wana hard lockdown isipokuwa maduka ya mitaani na supermarkets ambapo kanuni zote za usafi mita 2 kati ya mtu na mtu zinafuatwa.
Nch zingine kama Ujerumani, Austria na Italia wameondoa hard Lock-down na kuweka soft lockdown ili shughuli za kiuchumi ziendelee.
Georgia siku ya Ijumaa wanarudisha shughuli kama gym na sehemu za kukata nywele kabisa.
Hard Lockdown inaleta taabu kiuchumi in a long run na ndio maana kule Marekani walianza vurugu siku nyingi huku wakiandamana na silaha wakitaka hard Lock-down iondolewe.
Kuhusu kwamba raisi anajificha huko Chatoi wewe una uhakika gani kama anajificha?
Inawezekana yeye pia yupo kwenye lockdown wewe na mimi hatufahamu.
Isitoshe, huyu ni kiongozi wa nchi hivyo hatua zote za kiusalama, na kiafya kwake na familia yake ni lazima zipewe kipaumbele mbali ya yote, huyu ni raia namba moja wa Tanzania.
Halafu, wewe wasema kwamba anatisha watu ni vipi anatisha? Ikiwa watu wanapotosha ukweli wa habari na kutoziamini taarifa za wizara husika ya afya wewe wataka upotoshaji wa taarifa uendelee ama?
Respect, man.