Rais Magufuli: Hakuna Lockdown kwa Dar wala Tanzania, NEVER! Tusiwatishe watanzania, hofu ni ugonjwa mkubwa kuliko Corona

Jilegezeni na pongezi..wekeni hotuba msikilize kama mziki.

Mazingira yatufanyie wepesi ili shillingi ibaki kwenye pongezi na kusifu.

Corona imezua mijadala kibao huku Africa isiyo na maana.
Kamaa tumeanza visingizio vya Masks kuwa zina Infections.

Kuna mengi sana yatasemwa baada ya matukio mabaya tunayoombewa yatokee kwa lazima kwa kukiuka taratibu za kusifia na kupongeza.


Legeeni na familia zenu kwa kupongeza.Waulizeni wanaozika ndugu zao na walio na ndugu huku walikokimbia nini wanajisikia.
 
Kwanza niwape pole watendaji wote wa Rais waliojitahidi kupamba kadiri ya uwezo wao.
Pole sana Ummy Mwalimu, Faustine Ndugulile na Makonda pia.

Magufuli alishindwa kusema tu tutumie mitishamba badala ya kutegemea hospitali, inasikitisha sana kuona kiongozi mkuu wa nchi ana mawazo kama yale.

Anawaambia wananchi wasihofu corona mboba yeye kakimbia Dar Kajificha Chato?

Swala la kufunguia mikoa nashauri hivi

Mikoa ifungwe kwa wasafiri tu ila magari ya mizigo yaendelee na kazi huku ukaguzi ukiwa mkali sana kwa wanaovuka na magari hayo.

Kitendo cha Rais kuthamini pesa kuliko utu hili linatia hofu. Yaani ni bora watu wafe kuliko kukosa pesa? Kuna tofauti gani na ukoloni hapo?

Kumuongezea muda huyu Rais kwa kipindi kingine ni kijihatarisha maisha.

WIZARA WALIOPONA NI 11
RAIS WALIOPONA NI ZAIDI YA 100

Nani mkweli? Ni kweli Rais anahalalisha uongo kwa manufaa ya kijinga kumbe sasa hivi habari zote zitakuwa za kupika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Return Of Undertaker, Alimyumia rostam kumleta kwake bwana lowasa, alimtumia rostam kununua wabunge wa upinzani alimtumia rostam azizi kwa mambo ya kishetani anatumiwa yeye sasa.

Rostam azizi king maker ni mwana CIA hajawahi kuwa na nia njema na Tanzania amechelewa huyo mshamba wa chato

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata Mimi nilitegemea Barua ya Kujiuzulu Chap. Ummy na Majaliwa Ubunge unawatosha, Uwaziri umekuwa Fedheha!
 
Magufuli amekosea sana na huenda nusu ya population ya Dar es Salaama ikayeyuka kabla ya mwisho wa mwaka, na ardhi ya makaburi ikawa haitoshi. Hili siyo swal la kuangalia kisiasa na kiuchumi tu, ni lazima liangaliwe kitabibu.

Huyu mama Ummy Mwalimu anapigana vizuri sana na amenifurahisha sana kwa approach yake, ila sasa Makonda na Magufuli kuingiza siasa wanataka kuharibu mwelekeo wa mapambano. Corona haina chama, haina cheo, na wala haina mipaka.
 
Hapa Sheria ya TAKWIMU ichukue mkondo wake..
Hapa ndio Sheria ya Takwimu inachukua mkondo wake viongozi wahusika kila mmoja anatoa takwimu zinazomfurahisha.

Tungoje zile za Makamu wa Rais, Waziri wa Afya na za Msemaji Mkuu wa Serkali wote hawa sasa hivi wako mafichoni wakiogopa hili gonjwa linalowamaliza wanyonge wasio na pa kukimbilia.

Tuendelee kujifukiza kwa maji moto tufe haraka bila kuteseka muda mrefu kama kwa Covid-19. ,100 degrees C ni boiling point virus vinakufa, binadamu je?
 
Hakimu Mfawidhi, Mnyonge mnyongeni ila haki yake apewe, JPM analipa bilioni 700 kwa mwezi, analipa mishahara karibu bilion 600 kwa mwezi, ana miradi ya hospitali na Zahanati, kila mkoa, kila Wilaya.

Ana mradi mkubwa wa reli, mradi wa Umeme, Bomba la mafuta, ujenzi wa vivuko na Meli,madaraja, Barabara, ujenzi wa Rada mpya na viwanja vya ndege, Ununuzi wa Ndege Mpya, Ukarabati wa shule na vyuo vya zamani na vingine vingi ambavyo mimi sivikumbuki.

Katika Nchi za Afrika, Hakuna ata nchi mmoja inayoweza kutekeleza miradi iyo yote kwa pamoja, Iyo miradi niliyo ainisha ukiacha ujenzi wa bomba la mafuta iliyobaki yote ipo katika utekelezaji. Kikwete hakufanikiwa kukusanya fedha kama JPM, yeye aliamini katika misaada. Mkapa alibahatika kusamehewa madeni.Mwinyi yeye alikutana na masharti magumu ya IMF na uchumi mmbovu kabisa.

Ninacho msifu JPM analipa izo bilioni 700 kazi zake zinaonekana, mishahara analipa kwa wakati. Upende usi pende miradi yake iki kamilika kwa wakati Nchi itakua imepiga hatua. Swala la kukopa haliepukiki, ata ao Japani, Marekani n.k Wana Madeni makubwa kuliko ata uwezo wao wa kulipa ayo madeni.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tushaambiwa wasemaji wa korona ni DA Ummy na PM, hawa wengine usiwasikilize mkuu, zile ni story za vijiwe vya kahawa viunga vya Chato.
 
Rais Magufuli yuko sahihi kwa 100%
Kama hiyo dawa inayopulizwa mwilini siyo Sanitizer (>65% alcohol).

Kwa wale waliopita kwenye mashine hizo, ambazo pia ziko kwenye baadhi ya hospitali, wamethibitisha unyeevunyevu huo hukauka mara tu unaotoka kwenye hiyo mashine. Hata Ulaya hizo mashine zinatumika. Cha msingi dawa inayowekwa humo lazina iwe na kiwango kikubwa cha "alcohol" kuweza kuyeyusha utando wa mafuta (fat) wa kirusi.
 
Mazishi ya Mama Rwakatare Ni saa ngapi? Yangerusha Kwenye TV kwa faida ya waumini wake.
Umeambiwa watahudhuria watu kumi tu. Unataka kuweka na watu wa TV wakurusha live tena, hizo nafasi 10 waachiwe ndugu wa karibu tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…