Rais Magufuli: Hakuna Lockdown kwa Dar wala Tanzania, NEVER! Tusiwatishe watanzania, hofu ni ugonjwa mkubwa kuliko Corona

Rais Magufuli: Hakuna Lockdown kwa Dar wala Tanzania, NEVER! Tusiwatishe watanzania, hofu ni ugonjwa mkubwa kuliko Corona

SYLLOGIST!,
Hamtaki kucopy na kupaste hatua za kujikinga dhidi ya Corona badala yake mnakuja na za kwenu kujifukiza kwenye 100°C!Acheni utani na masuala ya afya za watu!
 
Wewe ni mpumbavu kabisa na nimekudharau,kwani hao uliowataja ndio nini?aliyekwambia kuwa lazima awaige hao ni nani?
kwahiyo aina ya maisha unayoishi wewe unataka kila mtu aige?
siamini una ujinga wa wa chini kiasi hicho,so sad!
smh!
Yaani mtu anakwambia tusitishane Corona ni kaugonjwa kadogo halafu yeye anakimbia Ikulu anaenda mafichoni,za kuambiwa changanya na zako!
 
Wakuu nawasalimu kwa jina la yeye aishiye milele. Mungu aendelea kuwapa faraja,upendo na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.

Back kwenye mada. Jana mkuu wa kaya kaibuka baada ya wengi kudai kaikimbia kaya. Kaibuka na ungangali wake ule ule wala hajabadilika. Kaibuka akitoa maelekezo ya kidaktari huku hoja hoja zake nyingi zikipingana na wataalamu wetu. Nikajiuliza maswali kadhaa je kabla ya hotuba:

1. alipata ushauri wa wataalamu husika kujua ABC ya hili janga?

2.Mbona hotuba yake inapishana pishana na maelekezo ya wataalamu ambao ushauri wao tayari tulisha uamini na kutuumia,je kauli zake si zitaleta mtafaruku zaidi kwenye kaya?

3. Nimeshangaa mkuu wa kaya kuamini "Hearsays" nyingi kuliko tafti rasmi za wataalamu. Je haoni kwamba hiyo ni kuwapoteza zaidi wanafamilia wake?

4.Kuna raia wema wengi walikua wameshika kasi kujitolea kusaidia kutoa vitakasa na viziba midomo. Leo kiongozi unatoka na kauli tata zilizojaa tashwishwi ambazo hazina utafti rasmi hapo si ni sawa na kuwavunja moyo wahisani?

Binafsi kwenye hutuba yake sikuona mkakati wowote wa kimantiki.Nilizani kwa ukimya wake angekuja na strategical plan ya kueleweka akiwa kashirikiana na wataalamu wake. Nilichokiona mengi aliyoongea jana kajishauri yeye mwenyewe tu,kwani aligeuka kuwa Daktari.

Halafu vitisho viiingi visivyo na sababu. Kwa ufupi amezidisha taharuki badala ya kupunguza ndio maana nasema ni bora angekaa kimya tu awache akina Bashite waendelee na maigizo yao angalau kuna wakati huwa wanapitia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kupitia Michango ya WADAU natamani na mimi ningekuwepo nasubiri matangazo ya moja kwa moja kutokea TBC.

Jamani
 
Kamgomoli,
Mkuu kimya chote ndiyo umeibuka na andiko hili?...inatia mashaka sana hivi unaelewa kazi ya akili ya Taifa?unafahamu Rais anapewa taarifa sahihi nyingi kuliko wewe?(sikatai kuna wanaopaka mafuta kwa mgongo wa chupa).

Unata kusema maelekezo ya upuliziaji sumu aliyoyatoa na kutaka mchanganyiko wa dawa na pia uhakika kuwa ule unaostahili ni kupingana na wataalamu wa Afya?

Unataka kusema kuwa Rais alipotaka viwanda vya ndani kuzalisha vifaa vya upumuaji " ventilators" na barakoa ni wazo potofu? (unasikitisha sana).

Unataka kusema tuendelee kusubiri misaada hiyo na vifaa hivyo vya Alibaba na mataifa makubwa mpaka lini? Na je vitatutosha?..( Aisee).Tutakuwa na uhakika upi juu ya usalama wa vifaa vya misaada ikiwa wanatunyanyapaa na kutuona Waafrika kama kizazi kilicholaaniwa?

Ila wakati mwingine tuwe unafikiri tunachoandika siyo kukurupuka na pendeleo zetu kupinga kila kitu. Hivi rafiki yangu Rais alipotoa ushauri juu ya Nchi za Afrika kuiomba Benki ya Dunia kusamehe madeni katika kipindi hiki napo nakosea? (unakera sana kama na hili hujaona).
Kwa kifupi umejidhalilisha kwa kuonesha ulivyo.
 
Wizara ya afya imeshafumuliwa tokea Jana ili kulinda taarifa zinazotolewa, kuanzia leo tutegemee kutopata tena report za ugonjwa wa corona maana waziri ummy mwalimu ameshapigwa mkala mzito asitoe taarifa bila kumskirikisha....

Tutegemee maambukizi zaidi Tanzania
 
Acheni ukilaza amesema tujaribu hajasema hiyo nayo ndiyo njia pekee. Zipo njia nyingi za asili.
" labda tuulizane maana ya kujaribu ni nini?)
 
Chige,
Well said.
Magu hana plan yoyote, anawaza kukusanya mapato. Sijui hajui kuwa biashara zinafungwa na nyingi zishafungwa?

Huko IMF na WB amenyimwa pesa.
Wale wamama wamesema kuwa wanapotoa msaada au mkopo sio w kwenda kukabiliana na covid tu.
Lazima muonyeshe jinsi gani jamaa ya chini itapata ahueni ya maisha.
Kwenye mambo ya Uchumi magu ni zero kabisa.
He act arrogant, not like a President but like an enemy.
 
Nchi iko songombingo kweli hii, sasa ile dawa ilokuwa inapulizwa haikufanyiwa utafiti na hawo mnaowapigia kelele siku zote kwamba ni wataalam wa afya?

Ni dhahiri kuna gap kubwa baina ya mkuu na wachini yake, dawa ishapulizwa sana leo ndo inatolewa fatwa, watanzania amkeni corona inaua msisubiri tahadhari za hao wanajiita wataalam kila mtu akae kwake tuangalie upepo
 
Habari wakuu, kinga ni bora kuliko tiba

Ni matuamini yangu sisi Watanzania ni wasikuvu na waelewa wa mambo hasa katika kipindi hiki cha covid19.

Baada ya Rais kutoa tiba ya corona, Watanzania tumeitika na tunaifanya hii kitu ya kujivukisha na mvuke.

Uzi huu tupeane taarifa unajivukisha kutokea wapi, je ni hali gani unaisikia pale unapojivukisha pia ni hatua gani za kufuata pindi unapotaka kujivukisha?

Mimi bado sijajivukisha, natarajia jioni hii nijivukishe

Karibuni wakuu kwa updates za kujivukisha
 
Kuna mtu amejikuta ni rais!
Mpaka leo bado haamini.
 
hapo kuna maelezo ya mtaalamu,na maelezo ya rais kama kiongozi.

unajua maana ya kuongoza mkuu,huu ugonjwa umeeshakosa tiba mpaka sasa ni mwendo wa kubahatisha tu.rais anaposema jaribuni ina maana mbahatishe,ikikubari heri.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona Rostam kapigwa kata funua. Hahahahah hakuna kujipatia umaarufu kuliko mwenye nyumba.

Ajiandae na kesi ya uhujumu uchumi kwa kutaka kuliangamiza taifa.

Sent using iphone pro max
Nafikiri maji yale yana pombe.
 
mlakimtoto, 1.Waziri mkuu,"watu 11 wamepona corona Coroa".
2.Mkuu wa kaya watu zaidi ya 100 wamepona corona.
3.Waziri wa afya dawa ya kufukiza haiui virusi vya Corona" 4.Mkuu wa kaya " Virus vya hupondeka pondeka kwenye centigrade 100,kwanini mnazuia watu wasijifukize?
5.Wataalamu wa afya," Barako za kutengeneza locally si salama na hazina uhakika wa kuzuia corona
6.Mkuu wa kaya," Barakoa zinazotoka nje hazna uhakika wa usalama,huenda zikawa na virusi vya corona".
Akili ya mwewe changanya na yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pensioners wengi ndiyo victims wa huu ugonjwa, nichelee kusema nikiangalia ni kana kuna hidden agenda, wakuu wanataka ku-wipe OFF pensioners, as pension funds zina matundu..

Haiwezekani mkubwa akawa na attitude ya namna hii..katika pandemic!

Everyday is Saturday...................... 😎
ahahaha,dah
 
Back
Top Bottom