Rais Magufuli: Hali kwa sasa ipo vizuri na Corona inapungua. Wanafunzi wa Form VI na Vyuo vyote kufunguliwa 01 Juni 2020

Unampigia simu rais mara 8 kwa siku, Ivi hukupewa job descriptions wakati wa ajira? kama mpango ni huo kuna haja ya uteuzi kweli
 
Sawasawa mkuu, maana nilikuwa nishaanza kwenda katikati ya mji sijavaa barakoa
 
Reactions: BAK
Raisi ninachojivunia kwako ni hiki kuwaambia ukweli watu,na kutufundisha kujitambua dhidi ya mabeberu.Ikumbukwe ya kuwa mabeberu Wana rugha laini na sura za upole ila wanachokuwazia mioyoni mwao usipime.
 
Ina maana tuwavumilie wanaozingua kwakigezo tu umechoka kuteua nakutengua, na wengine wasistaafu kwà kigezo tu kutakuwa na uteuzi!! !?

Mbona una mawazo FINYU Sana!!!

Typed Using KIDOLE
CCM hamtaki tu ku accept; kutakuwa na shida pahala tena ni kubwa!! Sema tu mmeamua kufa kiume
 
Raisi ninachojivunia kwako ni hiki kuwaambia ukweli watu,na kutufundisha kujitambua dhidi ya mabeberu.Ikumbukwe ya kuwa mabeberu Wana rugha laini na sura za upole ila wanachokuwazia mioyoni mwao usipime.
Ila msiombe misaada kwa mabeberu
 
Wapinga maendeleo walikuwepo tangu enzi za Nyerere. Na kuwapuuza tu.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Amejuaje bila kupima na hospitali nyingi kwa sasa zinawarudisha wagojwa nyumbani. Rafiki yangu mmoja yupo nyumbani kwake anaendelea vizuri lakini alikaribia kokosa pumzi, baba yangu mdogo naye anapona hao hawajaenda hospitali wala kupimwa. Hizi mbinu hazitusaidii maana vipimo vingetupa mwelekeo
 
Safi sana karudi nimependa.

Rais yupo kazini 24/7, na hivi sasa yupo kwenye maandalizi ya kuona jinsi ya kurudisha huduma muhimu katika kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Mfano kuona shule zinafunguliwa, Watalii wanavinjari kule Serengeti, Ngorongoro, wengine wanapanda mlima Kilimanjaro au kwenda Zanzibar ku-chill out etc. Tanzania tupo pazuri. Mwezi wa 7 au wa 8 njoo upande Treni ya umeme kwenda Morogoro - mji kasoro bahari.

hapa Kazi tu!

 
Reactions: Sax
Watalii awatawekwa isolation ila ni kupimwa joto tu. Huku tuna ambiwa kuwa incubation ya virusi ni kuanzia siku 2-14. Huyu mtalii tusema amepata maambukizi lakini aonyeshi dalili..

Then baada ya siku 5 au 10 yupo nchini dalili zikajitokeza huku akiwa ameisha interact na watu wengi. Je,si inaweza kua chanzo cha kusambaza maambukizi?

Utalii tusubiri jamani.
 
Reactions: Sax
Dah kumuelewa mkuu mwamba jiwe ni sawa kujaribu kuwaelewa wanawake 😉😉🐾🐾
But napenda msimamo wake,viongozi wa Africa(kanaani) waige mfano huu
🦍🦍🦓🦓
🇹🇿 🤝🤝🤝🇰🇪
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli, ameagiza kuwa mtu yeyote atakayepokea vifaa vya kupambana na Virusi vya Corona, vikishapimwa na Maabara Kuu ya Tanzania na kukutwa vina Virusi hivyo, basi ashitakiwe na apewe kesi ya jinai.

Rais Magufuli ameyabainisha hayo leo Mei 21, 2020, Ikulu ndogo ya Chamwino mkoani Dodoma, mara baada ya kuwaapisha Mabalozi wa nchi mbalimbali , Mkurugenzi wa TAKUKURU na Katibu Tawala Mkoa na kuongeza kuwa vitu vya bure vina gharama.

"Kwa mtu yeyote atakayepewa vifaa vya kuzuia Corona, halafu mkavipima mkakuta vina Corona, huyo mtu apelekwe kwenye kesi ya jinai, Watendaji wajiepushe kupokea pokea, tutatengeneza Barakoa zetu na tutatumia vifaa ambavyo vitakuwa tested na Maabara zetu, Corona inaisha lakini tusije tukapandikiziwa

“Jana nilimuona Mtu mmoja wa NIMR anasema sijui anapokea vifaa gani? Kama ni vifaa vipitie Wizara ya Afya vikaguliwe kwanza, corona ni vita, katika hiyo misaada unaweza kuletewa barakoa zenye corona kwasababu tu wanaona trend yetu nzuri, vya bure vinaponza " amesema Rais Magufuli.

Awali wakati wa hotuba yake, Rais Magufuli amekiri kumpa usumbufu mkubwa sana Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, na kumpongeza kwa namna ambavyo alikuwa mstari wa mbele katika mapambano hayo licha ya kwamba hana taaluma ya Udaktari.
 
Vyuo na shule kuanzia 01-06-2020 wanafunzi wanarudi shule ikiwa wamekaa nyumbani miezi 3.

Ombi langu mulitazame janga hili la corona kuwa limeathiri kila upande kwa wamiliki na wazazi, itakua ni jambo la kheri mkilitazama upya swala la ada.
 
Uelewe! Barakoa hutumika sehemu ambazo hakuna uwezekano wa kukaa mbali mbali kiasi cha angalau mita moja kati ya mtu na mtu kama vile kwenye vyombo vya usafiri wa umma.
Very unscientific, hata kama wakikaa 5 meters apart, kirusi akikaa hewani atadumu kwa muda, ukimaliza mkutano unakutana nae wakati unatawanyika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…