Rais Magufuli, hili la Kangi Lugola hujatenda haki. Sheria ya Uhujumu Uchumi inawahusu wananchi tu?

Rais Magufuli, hili la Kangi Lugola hujatenda haki. Sheria ya Uhujumu Uchumi inawahusu wananchi tu?

Walio pewa kesi za utakatishaji fedha hazifiki hata milioni 100 lakini huyu x waziri kapiga dola bilioni 400 na yupo mtaani
 
Kabendera kadaiwa kutakatisha milioni 173 yuko jela hawa ma matrilioni wanapewa ubalozi.
Koote ulikua unazungu,hiki ndio ulitaka kukileta
Siku hizi hakuna hoja,wewe na Magufuli nani mwenyewe uwezo wa kujua aliefanya makosa ya kimadaraka?
 
Kwa hyo kwenye kampeni Lugola atakuwa wa Demo. Tumeanzisha mahakama ya mafisadi na tumeanza kuwanyosha na hadi mawaziri tunawashtaki mfano waziri wa zamani wa mambo ya ndani Kangi Lugora.
 
Mbwiga usiwe zaidi ya Pimbi.....alliyesafiri kwenda kusaini ni Kamishna mkuu wa Zimamoto.

Mods toa huu uchafu mleta mada amekurupuka hana facts!

Mleta Mada tena? Je umeelewa the essence ya Post nzima ?
 
1T unapigwa mchana kweupe wakati serikali inakopa ili kujenga madarasa ya shule. Kumbe pesa ipo ya kutafuna
 
Mkataba unaostahili kuwapeleka watu uhujumu uchumi ni ule aliosaini Kabudi akishuhudiwa na mzee baba.
Kama tutaundiwa Tume huru ya uchaguzi na Octoba tukampata rais wa chaguo la wengi basi inshallah, panapo majaliwa 2021 hawa wahujumu wa uchumi wetu kupitia Barrick tutakuwa tunaenda kuwasalimia jumamosi Segerea
Una maana kubwa lao hahahaa, mpaka katiba ibadilishwe
 
“Kuwajibika au kujitathmini” ni maneno ya kisiasa yanayotumika vibaya kipropaganda ili kukwepa sheria.

Swala la hawa jamaa ilikuwa ni uvunjaji wa taratibu za kisheria na wanaweza kushitakiwa au kwa matumizi mabaya ya madaraka au kwa kukiuka taratibu!

Tabia hii ya kutoshitaki na kuadhibu watu itatufikisha pabaya. Ndio tofauti yetu moja na mabeberu!! Wanaadhibiana, sisi tunaoneana aibu/haya!!

Impunity - letting crimes go unpunished!!

This is very good comment.

Huyu Lugola amekiuka utaratibu na sheria but still anasema Rais amenipumzisha.

Something is wrong with the whole system.

Lugola hata kuwajibika kwa kuwaomba radhi wa TZ hajafanya hivyo na hata ku admit kwamba amefanya kosa , hajafanya hivyo , alichosema yeye ni kwamba Amepumzishwa.

Kama Adhabu yake ni kumtoa kwenye cheo kisha aendelee na maisha yake; basi tutarajie haya mambo ya ufisadi kutoisha and we will never be the kind of generation we want to be.
IMG_1211.JPG
 
Back
Top Bottom