Rais Magufuli: Lukuvi hawezi kuwa Mgombea urais wa CCM 2025 kwa sababu ana umri mkubwa. Ni fursa ya Vijana

Sisi tunapendekeza Rais awe na umri mkubwa kwa yale ambayo tumeyaona kwa wengine, Rais akiwa na umri mdogo atagoma kutoka madarakani na atatawala maisha yake yote, lakini akiwa mzee hata agome madarakani haitachukua muda atakufa
Atagoma jee wakati katiba inambana

Sent from my SM-J250F using JamiiForums mobile app
 
Hili si jukumu la Rais - Hili ni jukumu la kikatiba. Je katiba yetu unasemaje kuhusu Umri wa Rais wetu?

Hata hivyo hili lilikuwa dogo kwa EL na rafiki yake Mr. 0 baada ya kurudi kundini huku wakiendelea kudhani wanaweza kuukwaa Urais baada ya kuwa uhamishoni kwa muda.
 
Ha ha ha
Naenda badilisha RITA tarehe yangu ya kuzaliwa!
 
Rais ajaye ni mimi. Kwa hiyo mh. Rais amesema hivyo kwa sababu tayari anamjua Rais ajaye ambaye ni mimi
 
Hii inaitwa tentative position. Kabla ya uchaguzi aliwahi kuwatahadharisha wateule wake (PSs, RCs, DCs, etc.) kwamba angewakata endapo wangejaribu kugombea ubunge. At the end of the day, alibadili msimamo na baadhi ya wateule wake wakagombea ubunge!
 
Wewe ni mzushi unataka katiba ieleze kila jambo
 
Kauli hiyo ya JPM inaweza kuwa ni fursa na faida kwa wapinzani kama wataweza kuwatumia wazee na wanaccm ambao wameshapigwa chini mpaka hapo!
Nina amini wapo wanaccm wa umri huo waliokipigania na kukijenga chama ambao hawatakubaliana na utaratibu huo ambao haupo hata kwenye katiba si ya ccm wala ya JMT!
Hawa wanaweza wasikubali nguvu zao kwenda bure, hivyo ni hawa ndio wanaweza kuuza ramani ya vita kwa wapinzani huku wakikipasua chama hicho vipandevipande.
Kubwa zaidi watakuwa na msaada kama watasaidia wapinzani kupenyeza mkono kwa watu wa system na vyombo vya dola!
Hivyo CCM wajuwe wameshawasha moto ambao hawawezi kuuzima!
 
Yeye amesema chama Cha mapinduzi (CCM) yeye Kama mwenyekiti hawawezi kumpitisha aliyempita umri, rejea hata mh. Mstaafu JK alisema hivyo. kwahiyo hapo Katiba haihusiki, usi-genaralize. Bali ni ndani ya chama na utaratibu wao.
Kwani mwenyekiti wa chama huwaapisha mawaziri? Pale aliongea kama Raisi wa Jamhuri ya Tanzania
 
Dongo kwa kina membe
 
Anaongelea CCM wewe katika yako utakutana na NEC na chama chako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…