Nduka Original
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 1,012
- 817
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Na kitendo cha JPM kusema siyo mtazamo huu haijawa sheria. JPM ni mwenyekiti wa Sisiemu, anafahamu mwelekeo, mipango & matarajio ya Sisi-M kwa ajili ya maslahi mapana ya taifa. Ufipa mnaweza kumweka mgombea wenu yeyote hata mwenye miaka 900 ruksa.Kitendo cha Mh Rais kutamka hadharani kuwa mtu yeyote aliyemzidi umri asijidanganye kuomba nafasi hiyo ni kwenda kinyume kabisa na katiba ya Nchi.
Hakuna sehemu katika katiba ya Nchi yetu inayomkataza mtu yeyote kugombea nafasi ya Urais kwa kigezo cha umri mkubwa.
Washauri wa Rais jaribuni kumshauri Bwana Mkubwa kuna kauli akizisema ninaleta mtafaruku mkubwa sana katika jamii.
Jibu makini sana. Kama ulikuwepo we jamaa!Yeye amesema chama Cha mapinduzi (CCM) yeye Kama mwenyekiti hawawezi kumpitisha aliyempita umri, rejea hata mh. Mstaafu JK alisema hivyo. kwahiyo hapo Katiba haihusiki, usi-genaralize. Bali ni ndani ya chama na utaratibu wao.
Umemnukuu kiupotoshi zaidi. Heshimu teknolojiaHii inaitwa tentative position. Kabla ya uchaguzi aliwahi kuwatahadharisha wateule wake (PSs, RCs, DCs, etc.) kwamba angewakata endapo wangejaribu kugombea ubunge. At the end of the day, alibadili msimamo na baadhi ya wateule wake wakagombea ubunge!
Yaa napendekeza tupate raisi wa miaka 80 kuendelea mbele wanakuwaga na hekima sanaSisi tunapendekeza Rais awe na umri mkubwa kwa yale ambayo tumeyaona kwa wengine, Rais akiwa na umri mdogo atagoma kutoka madarakani na atatawala maisha yake yote, lakini akiwa mzee hata agome madarakani haitachukua muda atakufa
Umemnukuu kiupotoshi zaidi. Heshimu teknolojia
Kauli hiyo ya JPM inaweza kuwa ni fursa na faida kwa wapinzani kama wataweza kuwatumia wazee na wanaccm ambao wameshapigwa chini mpaka hapo!
Nina amini wapo wanaccm wa umri huo waliokipigania na kukijenga chama ambao hawatakubaliana na utaratibu huo ambao haupo hata kwenye katiba si ya ccm wala ya JMT!
Hawa wanaweza wasikubali nguvu zao kwenda bure, hivyo ni hawa ndio wanaweza kuuza ramani ya vita kwa wapinzani huku wakikipasua chama hicho vipandevipande.
Kubwa zaidi watakuwa na msaada kama watasaidia wapinzani kupenyeza mkono kwa watu wa system na vyombo vya dola!
Hivyo CCM wajuwe wameshawasha moto ambao hawawezi kuuzima!
Umri mkubwa ila hawakaribii Joe Biden na Donald Trump wana 74yrs na 77yrs na bado wanagombeaMwenyekiti wa CCM Rais Magufuli amesema uchaguzi mkuu wa 2025 utatoa fursa kwa vijana kwa sababu zaidi ya 65% ya wapiga kura ni vijana
Rais Magufuli ametoa mfano wa mh Lukuvi kwamba hawezi kuwa Rais wa JMT 2025 kwa sababu atakuwa na miaka zaidi ya 70.
Maendeleo hayana vyama!
=======
RAIS MAGUFULI: Hakuna mtu alitegemea Mwinyi atakuwa Rais wa Zanzibar lakini pia Mwinyi katika kipindi chake chote hakuutafuta Urais, vitu hivi vinapangwa. Hakuna mtu alijua profesa Ibrahim atakuwa Jaji mkuu wa Tanzania hata mimi sikujua kama nitakuwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Kwa sababu katika miaka yote ishirini nikiwa waziri na nikiwa mbunge sikuwahi kuomba hata ujumbe wa NEC.
Sikuwahi, wajumbe wa NEC walikuwa wakina Lukuvi, tangu aingie mle ni mjumbe wa NEC lakini Urais hakuupata na sina uhakika kama ataupata Urais. Wewe sasa hivi ana miaka sitini na kitu, tukapendekeze kwenye central committee tukachague Rais anaenizidi umri mimi, ndio ukweli.
Maneno mengine yanaumiza lakini nataka niwaeleze muwe mnajitayarisha kisaikolojia kusudi msipoteze hata hela zenu, hata wewe profesa Kabudi huwezi ukawa Rais, najua haya mambo ni magumu lakini huo ndio ukweli.
Mzee Kikwete wakati anaondoka, alisema hataona Rais ambae anamzidi umri wake, sasa muangalie mimi nina umri gani nitakapokuwa namaliza, ujipimie kuanzia kwenye umri pale. Yaani Malecela tumpendekeze awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, haiwezekani! Ameshakuwa mstaafu, tunamheshimu, tunampenda.
Najua mmenyamaza kwa hiyo inawezekana umekaa na jirani yako ambae ndie atakuwa Rais ambae labda ni kijana zaidi kwa sababu 65% ya watanzania ni vijana na hivi ndivyo vilivyomsaidia Mwinyi kushinda kule, wapiga kura ni vijana wether you like or not huo ndio ukweli, sasa huwezi ukawapelekea wapiga kura mtu ambae sio saizi yao.
Maneno yanauma lakini si mmeniomba niseme hapa, mimi nilikuwa nimekaa kimya tu leo nisiseme, nilikuwa nachomekea tu.
Umeeleza vizuri sana. Lakini umesema tena tatizo siyo CCM. CCM ndiyo tatizo kwa sababu ndiyo walitakiwa watengeneze hiyo mifumo na kama ni katiba waongoze kuibadilisha. Mengine umeelezea vizuri tu na hasa tatizo limeonekana kuwa kubwa kwa sababu awamu hii rais anataka kuwa ndiye kila kitu. Kwa kifupi hii mifumo awamu zilizopita japo haikuwa mizuri lakini marais waliokuwepo hawakuwa wanajilimbikizia madaraka mengi kama huyu wa sasa. Mfano mzuri wa kuwa ni mifumo mizuri ni Marekani. Unajua Marekani isingekuwa na mifumo imara Trump angeiharibu sana nchi na hata kwenye madaraka asingetoka.Maneno aliyosema Rais leo kuhusu kazi ya urais na umri inatuonyesha wazi, pale ikulu kwa sasa hatuna watu wanaomsaidia Rais aione vizuri nchi yetu hasa kwa siku zijazo..muhimu si kuongelea mtu wa kujaza nafasi ya urais, nadhani muhim ni kuwa na mifumo na taasisi imara za kumsaidia anayekuwa Rais, na kwa maana hiyo UMRI si muhimu awe kijana awe mzee awe mwanamke au mwanaume kazi nzr itafanyika!! Bahati mbaya sana kwa muda mrefu tumeshindwa kugundua tatizo la nchi yetu liko wapi..wengi tunadhani ni CCM si kweli.
Hata ukisikiliza hotuba ya Rais bungeni inakosa maneno mazuri ya kujenga dira na mwelekeo imara, mfano haisemi kabisa juu ya kulileta taifa pamoja sababu hali baada ya uchaguzi upo mgawanyiko mkubwa..wengine wanakimbia nchi, wengine bado wanalalamikia uchaguzi nk, ulitarajia hotuba ya kujenga udugu na umoja zaidi baada ya uchaguzi..kumbe ni ndoto.
Ushauri:
Kama kutatokea nafasi ya kufanya marekebisho ya katiba, basi tufikirie kuwa na mabadiliko makubwa kwenye taasisi zinazomsaidia Rais, kazi hizi ziwe na kikomo, mtu atumikie hapo si zaidi ya miaka 5 kupisha wengine wenye mawazo mapya kumsaidia Rais..vinginevyo tutaendelea kuwa na hali ya uchakavu wa mawazo, kauli, tabia, mikakati nk hata kama tunapata Rais kijana wa miaka 45..Asanteni.
Usitudangenye ndugu yangu. Mungu ndiye anapanga mpaka viongozi wauaji waingie kwenye madaraka?Cheo na madaraka hupangwa na Mungu mwanadamu hawezi zuia muda wa Mungu ukifika..... Joe Biden amehangaika kusaka Urais tangia mwaka 1988 zaidi ya miaka 32 lakini Mungu akaja kumpa wakati ana miaka 77. Ogopa sana mipango ya Allah, aliwahi kumruzuku mtoto Nabii Ibrahim akiwa mzee aliyekongoroka hata mkewe hakuamini...... Neema ya Mungu haiwezi kupingwa na mwanadamu
Nasema tatizo si CCM sababu wapo watu nyuma yao..Mwl. Baba wa taifa aliwahi kuwaongelea hawa watu, kwamba kila alipotaka kung'atuka wao walikuwa wanamwambia ooh Mwl. watu bado wanakuhitaji na bla bla nyingi, vile Mwl. alikuwa thinker aligundua kuwa kumbe bla bla hizo za kuomba aendelee kubaki kuongoza ni kwa sababu uwepo wake hapo wala si kwa faida ya nchi ni kwa faida ya matumbo yao..hao ndio watanzania wanapaswa kudeal nao.Umeeleza vizuri sana. Lakini umesema tena tatizo siyo CCM. CCM ndiyo tatizo kwa sababu ndiyo walitakiwa watengeneze hiyo mifumo na kama ni katiba waongoze kuibadilisha. Mengine umeelezea vizuri tu na hasa tatizo limeonekana kuwa kubwa kwa sababu awamu hii rais anataka kuwa ndiye kila kitu. Kwa kifupi hii mifumo awamu zilizopita japo haikuwa mizuri lakini marais waliokuwepo hawakuwa wanajilimbikizia madaraka mengi kama huyu wa sasa. Mfano mzuri wa kuwa ni mifumo mizuri ni Marekani. Unajua Marekani isingekuwa na mifumo imara Trump angeiharibu sana nchi na hata kwenye madaraka asingetoka.
Mtu kama Lowassa umemwonea tu. Yule sidhani bado anauwaza urais na angekuwa bado anautamani huu uchaguzi bado angegombea tena kupitia Chadema. Afya yake haimruhusu kwa sasa. Ile 2015 tu ilikuwa shida.Hili si jukumu la Rais - Hili ni jukumu la kikatiba. Je katiba yetu unasemaje kuhusu Umri wa Rais wetu?
Hata hivyo hili lilikuwa dogo kwa EL na rafiki yake Mr. 0 baada ya kurudi kundini huku wakiendelea kudhani wanaweza kuukwaa Urais baada ya kuwa uhamishoni kwa muda.
Hao watu ndiyo CCM yenyewe basi ndugu yangu.Nasema tatizo si CCM sababu wapo watu nyuma yao..Mwl. Baba wa taifa aliwahi kuwaongelea hawa watu, kwamba kila alipotaka kung'atuka wao walikuwa wanamwambia ooh Mwl. watu bado wanakuhitaji na bla bla nyingi, vile Mwl. alikuwa thinker aligundua kuwa kumbe bla bla hizo za kuomba aendelee kubaki kuongoza ni kwa sababu uwepi wake hapo wala si kwa faida ya nchi ni kwa faida ya matumbo yao..hao ndio watanzania wanapaswa kudeal nao.
No..Hao watu ndiyo CCM yenyewe basi ndugu yangu.
Jibu makini au ugoro? Mgombea anapatikana kwa kupigiwa kura na vikao mbali mbali. Hata akiwa mwenyekiti hawezi kutoa uamuzi wa aina huyo.Jibu makini sana. Kama ulikuwepo we jamaa!
Mara hii wameanza kuongelea urais 2025! CCM kweli wameamua kuitafuna nchi milele liwe jua iwe mvua; hii nchi hawaiachii kwa "vikaratasi". Badala ya kuongelea vitu vya muhimu hususan tume huru ya uchaguzi, Katiba Mpya, etc. wanaanza kutajataja nani anafaa na nani hafai mapema hivi? Kwa mtindo huu, tundelee kuzoea "bao la mkono" miaka mingi ijayo!
Really? Influnce ya Mwenyekiti wa Chama (hasa ambaye ndiye President) lazima uiweke kwenye mlinganyo wa tafakari yako.Jibu makini au ugoro? Mgombea anapatikana kwa kupigiwa kura na vikao mbali mbali. Hata akiwa mwenyekiti hawezi kutoa uamuzi wa aina huyo.