Rais Magufuli: Mshahara wangu kwa Mwezi ni Sh. Milioni 9.5. Nitatoa salary slip...

Dumelang

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2011
Posts
3,204
Reaction score
5,710
Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametaja mshahara wake kuwa ni Tsh mil 9.5, huku akiahidi atatoa Salary slip zake punde akitoka mapumzikoni Chato.

Hiyo imetokea wakati wa kipindi cha magazeti leo tarehe 01/04/2016 ambapo watangazaji walisoma habari iliyoandikwa na gazeti la nipashe kuwa Zitto na Lissu waomba ataje Mshahara wake na ukatwe kodi.

Wakiwa katika mjadala huo, walipokea taarifa kuwa Rais kawasikia na katuma taarifa ofisi za Clouds kujuza mshahara wake kuwa ni mil 9.5 na atatoa stakabadhi zake akirudi Dar.

Chanzo: Clouds 360 Asubuhi hii

==========
Kutoka Gazeti la Mwananchi:

 

Aya sawa!!!
Raisi analipwa kidogo kuliko wakurugenzi wa mashirika ya umma sawaa!!
Ila katika kubana matumizi kama vipi adake milioni mbili tu😉😉😉

Happy fools day
 
Hivi zito na lisu huwa swaelewa na wao wanalialia kimoyoyo hakuna posho za kijinga wameanza kujiuzuru,hawa jamaa hawataki kusema ukweli kwa watanzania kuwa jaman maisha yamebadilika siku hiz fedha hakuna wanaanza kumshambulia rais et taja mshahara.kuna baadhi ya wanasiasa nishaachaga kuwasikila kwasababu niwanafiki ni baraa wakibanwa wanaongea vingne kufikisha ujumbe nawaomba watulie sindano ziingie vizuri.
 
...milioni moja inamtosha...
 
Hiyo habari ni ya ukweli haina uhusiano na siku yenu ya wajinga.

Ila milioni 9 ni nyingi sana kwa sababu hanunui chakula ulinzi,maji,umeme,usafiri,matibabu,mavazi yote anapewa bure.

Awe anapata laki 8 tu zinamtosha za kuwatumia ndugu zake chato wakimuomba ela.
 
Baada ya watu kutaka kujua yeye anapokea sh.ngapi awapigia simu clouds tv na kujibu swali hilo kuwa yeye anapokea sh.9.500.000 kwa mwezi na akimaliza likizo atatoa ufafanuzi wote

Source clouds Tv
 
Wamefanya Plagarism pole.mkuu jamaa hawa ni makanjanja sana
 
Jamani hiyo habari ni ya kweli sio sikukuu ya wajinga iliyopo kwenye TV acheki sasa hivi clouds tv
 
Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli amesema mshahara wake ambao yeye ameukuta na ambao analipwa ni Milioni 9 na laki 5.

Rais Dkt.Magufuli amelazimika kuyasema hayo wakati wa uchambuzi wa magazeti katika kipindi cha Clouds360.

Akizungumza na mtangazaji wa kipindi hicho Hudson Kamoga ameahidi akirudi kutoka likizo yupo tayari kuonyesha nyaraka za malipo ya mshahara wake.

Baada ya kusema mshahara wa juu uwe angalau Milioni 15 kumbe yeye hata Milioni 10 hajafikisha
 
Leo wakati nasikiliza Kunani Tanzania Magazetini Clouds TV kipindi, Gazeti la Nipashe nileandika taarifa kuhusu Zitto na Tundu Lissu kumtaka Raisi Magufuli kutaja mshahara wake ili wajue kiasi cha kodi anacholipa!
Haikuchukua muda, taarifa ya Breaking News ikasomwa na Mtangazaji Baby kuwa, Mh. Rais kapiga simu na kuwatajia kiwango cha mshahara wake na kuwa atakapotoka rikizo fupi aliyonayo atawaletea risiti ya mshahara wake! Mh. Rais ametaja kuwa Mshahara wake ni Milioni tisa na Laki tano (Tsh. 9,500,000/-)

Chanzo: Clouds TV, Kunani magazetini!
 
huu uzamwamwa unasemaje mambo ya kitaifa kwenye private media nyeti kama hayo ila kumbukeni leo 1/4
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…