Rais Magufuli: Mshahara wangu kwa Mwezi ni Sh. Milioni 9.5. Nitatoa salary slip...

Inawezekana ikawa mshahara pekee ni hiyo 9milion bila marupurupu, na ndio maana baadhi ya watu wanasema angetaja pamoja na marupurupu mengine anapata jumla ya Tsh ngapi? Nadhani akieleza hilo anaweza akawa na mshahara zaidi ya hiyo tajwa
 
Sasa wewe unayejua mshahara wake si useme analipwa shilingi ngapi na wengine tujue siyo kupinga halafu hata wewe hujui analipwaje
 
We umeshazowea kudanganya na magazeti ya kubenea ndio maana huamini, ok sio mbaya we endelelea na kuzungusha mikono
 
Magufuli akiongea na Clouds alitaja mshahara wake na kuahidi atakaporudi likizo ataweka wazi salary slip yake kwani anapenda uwazi.

Japokuwa alisharudi likizo lakini salary slip imebaki story ama ahadi hewa au ni stunts. Lakini pengine bado inaprintiwa maana salary slip ya rais yaweza kuwa nzito sana ikachukua miezi kuprintiwa.

Naombeni msaada nataka kujua rais anakwepeshewa kodi kiasi
 
SALARY SLIP HAITOKI NG'OOOOOOOO!
 
binadamu hata apate raha kwa miaka 80,akipata shida siku 1tu anasau raha zoote alizopata wakati ule, vilevile alipa shida kwa miaka hata 80 atasau akiwa raha kwa siku moja tu, ILA KWA MWANADAMU NI LAHISI ZAIDI KUKUMBUKA SHIDA KULIKO RAHA.
na ndiomaana tunaona viongozi waliowengi wanapoomba uongozi wanaahidi mambo mengi lakini wanapoupata muda mchache tu wanasahau.
 
Labda Ilikuwa siku ya wajinga..teh teh
 
Ukisema kuna watu wanachukiiaaaaa!! Nchi masikini jamani!
 
Itakuwa watu wa utawala wamesahau tu maana maoni au kauli ya Raisi ni amri
 
Ziko wapi zile salary slip za Mkuu walizopewa clouds 360 kutuonyesha mkuu anakula Mill 9 kwa mwezi?
 
hakuna anayeruhusiwa kupata zaidi ya milioni 32 katika mashirika ya umma,guess m.32 ni mshahara wa nani! chezea uimla wewe
 
Dah Mie wanipe milion moja tu zinanitosha asee duh kuna watu wanakula bata sana dunia hii yaani unalipwa milion 9? ?? Eeeeh Mungu nijaalie mja wako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…