Rais Magufuli nisikilize kwa makini, Sitaki upoteze muda bure

Ulianza kutafakari ukiwa mtoto, kama sikosei 16 yrs ukiwa Sekondari!!

Ndo maana unaandika mada ndeefu kama unafundisha watoto wenzako. Hayo mambo waachie wachumi wabobezi. Unatupotezea muda aisee
 
Ulianza kutafakari ukiwa mtoto, kama sikosei 16 yrs ukiwa Sekondari!!

Ndo maana unaandika mada ndeefu kama unafundisha watoto wenzako. Hayo mambo waachie wachumi wabobezi. Unatupotezea muda aisee

Mtu mbobevu hawezi shindwa kusoma makala fupi kama hii isiyo na maneno hata elfu kumi.

Watoto ningeweza waandikia aya mbili tuu zingewatosha
 

Sipo hapa kukufundisha, niliowaandikia wanajua nini nimelenga na wanaelewa naongelea nini.

Huko juu nimeshaeleza kuwa China ilishavamia nchi kama Vietnam, Burma, Mongolia, Taiwan n.k. Unajua maana ya kuvamia na kutawala?
Hiyo Russia pengine huijui ndio hiyo iliyokuwa inaitwa USSR, pengine hujui kilichoifanya iingie katika vita ya kwanza na ya pili ya Dunia, unafikiri vita hivyo sababu kuu ilikuwa ni nini kama sio maslahi ya kiuchumi katika kutawala makoloni mengine?

Najua hujui kuwa kabla ya vita ya pili ya dunia, Taifa la japan ndilo lilikuwa linaongoza kwa masuala ya uvuvi, lakini baada ya vita ya pili kuisha najua hujui kilichopelekea taifa hilo kushuka katika nafasi hiyo, na nafasi hiyo kushikiliwa na hiyo nchi ya Norway, hata hivyo sina uhakika kama unajua wakazi wa Norway na Denmark asili yao ni jamii zipi.

Kuhusu hiyo Miradi inayoendelea ndani ya nchi labda wewe ndio huijui, au pengine unahadithiwa tuu na kuiona kwenye luninga, mimi mpaka kuishuhudia nimeishuhudia. Kuanzia huo mradi wa umeme katika bonde la Rufiji, vituo vyote vipya vya mabasi mikoani, kuanzia Hiko cha mbezi Luis, Igumbilo, Dodoma, kituo cha mabasi cha kibaha, kituo cha mabasi Mpanda, kituo cha mabasi Singida n.k

Mradi wa SGR kILa mtu kaushuhudia hasa wakazi wa Dsm, Pwani na morogoro. Usafiri wa anga, ukarabati wa terminal 3 na ndege mpya tena kupanda nimeshazipanda, sijui unataka nielewe kwa namna gani hiyo miradi.

Miradi inafanya vizuri lakini ushauri wangu naona kwako hauna maana kwa sababu sio mtu husika, wahusika wanajua nazunguzia nini.

Kuhusu Historia naomba uachane napo maana huko utajitia aibu
 
Dogo ameshusha nondo za maana Sana big up
 
Mkuu nchi haiongozwi kwa historia unazozitaja hapa sio kila kitu ni cha kuiga hamasisha watu kujitambua na kufanya kazi sio swala la kuwa tegemezi na fikra za kitumwa. Unaweza kuwa na ushauri mzuri lakini uwasilishaji ukawa unatia mashaka. Sitakujibu tena sababu umeshasema wewe ni mtu wa fasihi.
 
Mhe. Rais, naomba nifupishe habari hii, huu ni wakati wa kutumikisha watu wa mataifa mengine, kwani kwa kufanya hivyo ndio uhakika wa kuiendeleza nchi upo kwa kiasi kikubwa.
Kijana wa miaka 26!

Kuna mambo mengi uliyoandika yanafikirisha, hata kama ni nadharia kuliko uhalisi wenyewe. Kwa mfano, ni huo hapo juu nilioku'quote'. Hujaeleza hayo mataifa mengine utawatumikisha vipi: utakwenda kuwafanya wawe makoloni kama wao walivyofanya mataifa mengine kuwa makoloni?
Kama kwa mfano huo ulioutoa una maana ya "ushirikiano na mataifa mengine", basi sema hivyo waziwazi, lakini sio "kuyatumikisha" inavyoeleweka hapa.

Pengine ungesoma historia ya China, ingekufungua mawazo kidogo na kujua kwamba wao walijifungia kwa muda mrefu sana, walipojifungua taifa lao likawa lipo tayari kupaa juu kama roketi kimaendeleo. Walipokuwa wamejifungia ("hawatumikishi wengine") walikuwa wakiweka miundo imara)

Nikiri, sikusoma bandiko lako refu lote, huenda kuna mambo kadhaa uliyoandika yanayoeleza undani wa nadharia hii uliyoweka hapa.

Inawezekana sana kukawa na tofauti kati ya uliyoandika na baadhi ya yale ninayoyadhania mimi kama chachu ya kuleta maendeleo ya nchi haraka.

Kwa ufupi niaminiyo mimi:
1. Maendeleo ya nchi ni 'process' ambayo haitokeii "ghafla bin vuuu". Ni mwendelezo na kuongezea kwa yale yaliyokwishafikiwa. Kwa mfano. Mtu hawezi sasa hivi akasema hatujapiga hatua katika kuendeleza elimu yetu ukilinganisha na wakati Mwalimu Nyerere anatwaa nchi toka kwa wakoloni. Ndiyo, elimu yetu imekuwa ni ya kusuasua katika sehemu mbalimbali, lakini mtu hawezi kusema kwamba hatujaendelea. Kinachotakiwa hapa sasa hivi katika eneo hili ni kuifanya iwe bora zaidi na kuwaandaa wasomi wetu katika nyanja mbalimbali kuwa na uwezo wa kuligeuza kwa kasi zaidi kimaendeleo taifa letu. Maana yangu ni kwamba, hatuwezi kuwa na kasi (speed) au (rate) ile ile tuliyokuwa nayo miaka ya sitini au sabini. "Rate" yetu sasa inatakiwa kuwa ya juu zaidi katika kuleta maendeleo.

Na ili nieleweke vizuri juu ya jambo hili; jaribu kufikiria baadhi ya nchi ambazo siku nyingi sana zimekuwepo huru kabisa na hata kihistoria zinafahamika kuwa ni mataifa kamili: Turkey (uturuki), kwa mfano, ni muda huu wa karibuni ndio wameanza kuonekana kupiga hatua za kuwa nchi iliyoendelea, baada ya miongo na miongo mingi ya taifa hilo kuwepo kimuundo kama taifa. Na Misri je? Unaijua nchi inayoitwa Haiti? Inawezekana kabisa kwa hali waliyonayo sasa taifa hilo, ikawachukua miaka mingi sana kubadili hali zao kimaisha.
Unaweza ukasema Tanzania haiwezi kamwe kuwa kama Haiti?

2. Maendeleo yanaletwa na wananchi wenyewe, sio viongozi. Viongozi ni kusaidia kuweka mipango mizuri na kusimamia utekelezaji wake tu wa maendeleo wanayoyaleta wananchi wenyewe. Kwa hiyo, Rais Magufuli hawezi kamwe kuiletea Tanzania maendeleo, hata kama angeanzisha makambi ya kuwatumikisha wananci wake.

3. Nci zetu hizi kamwe hazitakiwi kwenda kuvumbua "tairi" upya. Tairi tayari lipo linalofanya kazi vizuri. Lengo letu sasa ni kujua jinsi ya kuyatumia haya "matairi" ya kuleta maendeleo vizuri. Na hili ndilo jukumu kubwa ambalo wasomi wetu wangelikazia ili kuwafikishia wananchi nyenzo hizi za kuharakisha maendeleo yao.
Wakulima wetu wapate ushauri wa kila aina ili wazalishe mazao kwa wingi na kuhakikisha mavuno yao hayaharibiwi kabla ya kufikishwa sokoni.
Tunanunua kila aina ya dawa toka nje, miaka zaidi ya 60 baada ya kupata uhuru wetu. Tunasomesha kila mwaka wataalam wetu katika nyanja hii ya kutengeneza madawa, lakini kama taifa hawa watu hatuwapi nyenzo za kuwawezesha kufanya kazi yao ya kutengeneza madawa aina mbali mbali, badala yake hawa watu tuliowasomesha kwa gharama kubwa wanaishia kwenda kuwa "wauza duka"! Huu ni utuzizi mbaya wa raslimali zetu. Na huu ni mfano mmoja tu katika mingi! Wengi wa hawa watu sasa mawazo yao ni kuingia kwenye siasa, kama akina Magufuli, badala ya kuvumbua na kutengeneza mafuta yanayozuia kutu yatokanayo na zao letu la korosho! Sasa, si angalao Magufuli mwenyewe angewekea mkazo baada ya kuingia kwenye siasa, ili watu (wasomi) wa aina yake wapewe fursa zaidi kuitumia elimu yao katika maeneo mbalimbali ili taifa lifaidike na utaalam wao? Badala yake, tunaona maprofesa ndio wanaojazwa kwenye vyeo vya kuteuliwa, badala ya kufanya kazi muhimu la kuligeuza taifa hili katika nyanja walizosomea!

Kama taifa, kwa nini viongozi wetu hawa wasingekazia tuandae mfumo mzima wa kuwa na "Chemical industry" yetu wenyewe - mali ghafi ya kutosha ipo ya kufanya hivyo Nchi kama Israel, Taiwan na nyinginezo wameweza, kwa nini sisi tusiweze..., ni umaskini wetu tu wa kifikra ndio unaotukwamisha.
Hatuwezi kama taifa kukubali kutojiandaa kwa mabadiliko haya makubwa yanayoletwa na ''technology" sehemu mbalimbali duniani. Ni wajibu wa viongozi wetu kuweka mipango sahihi na kuhakikisha kwamba hatupitwi na fursa kama hii itakayowezesha watu wetu kuwa wavumbuzi (innovators).
Kwa hiyo unaposikia nchi zinatofautiana, tofauti hizi zinatokana na maono ya viongozi wa nchi hizo.

Ngoja nikuache utafune haya kwanza. Lakini la muhimu, pengine kuliko mengine yote--- sahau kabisa swala la Magufuli kukuletea maendeleo au kuiletea maendeleo Tanzania. Hili ni jukumu la waTanzania wenyewe.
 
kama kweli una miaka 26 na umeweza kuandika hivi hongera sana maana yake utakaopo kuja fika 40 yrs utakuwa ni mwandishi mzuri sana [serekali isaidie sana wakulima ili tupate chakula kingi tuilishe afrika]
Eeenh, wewe huoni hata kaweka 'contact information' yake hapo? Huyu akishateuliwa sehemu fulani sahau kabisa ndoto alizoweka JF. Akina Kala Maganda na Popole hujawahi kuwasikia?
 
Dogo umeongoea vizuri sanaa...too bad rais wetu hana confidence ya kutosha!!! Kwenye outside world
 
LOoooo! Ni wewe uliyeandika haya?

Basi tena!
 
Kwahiyo unataka Mh sana Jiwe akavamie Congo na kupora dhahabu yao sio ?
Uvamizi siyo lazima ubebe rungu. Chatu anamvamia mbwa kwa kutoa harufu ya kuvutia, halafu mbwa anaenda mwenyewe huku akifurahia, na kisha anamezwa.

Uvamizi wa kutumia nguvu ulikwishaisha, unafanywa na wasio na akili. Watu werevu hufanya uvamizi wa akili ambao wale wanaosubiria uvamizi wa nguvu, hawana uwezo wa kutambua kuwa wamevamiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aliyekuambia hayo uliyosema siyaoni ni nani? Naomba ukisoma makala za kikubwa utulize akili yako, kama umezoea makala zenye ufupisho ninngekusihi ufuatilie hizo hizo. Hizi ndefu waachie wakubwa wako
Unavuruga mada yako mwenyewe! Pole sana!
 
Si kweli china imeendelea kwa kutumikisha wananchi wake mpaka leo hii. Hata wewe unaweza kuendelea ukijitumikisha wewe mwenyewe kufanya kazi yako ya kujiajiri kisha kuwauzia watu wenye uhutaji na bidhaa zako. Ulikuwa hujuwi hili?
Unabisha kitu ambacho kipo wazi kabisa ,wachina wanafanya kaz sana tena kwa juhud lkn kaz izo pia mojawapo kutumia nchi nyngne ,mfano apa africa wachina wapo karbu kila sehem na wapo karbu kila sekta
 
Mbona unarudia rudia maneno yale yale? We kweli bado mtoto
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…