Rais Magufuli: Nitaheshimu ukomo wa miaka 10 ya Urais kulingana na Katiba ya Tanzania

 
Hakuna Mtanzania asiyejua uwajibikaji, uzalendo, uaminifu, ujasiri, uchapakazi na weledi wa Rais Magufuli ambaye si tu amekuwa kivutio ndani ya Tanzania, bali amekuwa ni kipenzi cha wengi hata nje ya mipaka ya nchi yetu.

Kutokana na uwezo ambao ameshauonyesha tangu alipoingia madarakani, hasa katika kupigania raslimali za nchi hii, kupambana na rushwa, ukusanyaji wa mapato ya Serikali, udhibiti wa matumizi ya Serikali, uwajibikaji wa wafanyakazi wa sekta za umma, uboreshaji wa miundo mbinu na ukuaji wa uchumi; ningependekeza muda wa Rais kukaa madarakani uongezwe kutoka miaka 5 muhula wa kwanza hadi kufikia “miaka 7” kwa muhula mmoja hivyo akikaa kwa vipindi vyote 2 awe amehudumu kwa “miaka 14” badala ya miaka 10 ya sasa.

Nasema hivi kwasababu muda wa miaka 10 hautoshi kwa Rais kutimiza yote aliyokusudia na isitoshe tumempata Rais mchapakazi(jembe hasa) ambaye ni “hazina” muhimu kwa taifa hili hivyo ni lazima tumuongezee muda zaidi ili taifa “linufaike” kwa uwepo wake madarakani kwa kipindi kirefu zaidi.

Nawaomba Wabunge wote wa CCM waungane pamoja na kuipeleka hoja hii Bungeni mapema sana mwakani kabla ya vikao vya bajeti kuanza ili mchakato wa kuibadilisha KATIBA kwenye kipengele cha muda wa Urais kifanyiwe marekebisho kabla ya uchaguzi mkuu wa 2020 ili uchaguzi huo ufanyike mwaka 2022. Hata kama itahitajika kura ya maoni kutoka kwa wananchi, Watanzania asilimia 75 tutaunga mkono hoja hii. Tena isitoshe Wabunge wa CCM ndio wengi(na wanazidi kuongezeka), lazima hoja hii itapita bila kupingwa. Kuna Mbunge aliwahi kuileta hoja hii Bungeni lakini sijui iliishia wapi. Tafadhalini sana, hakikisheni hoja hii inarudishwa tena Bungeni ili ifanyiwe maamuzi sahihi.

Kwa kufanya hivi sisi Watanzania hatutakuwa wa kwanza wala wa mwisho sababu kuna nchi ambazo ni majirani zetu wamekwisha badilisha muda wa kuhudumu Rais na zingine pia zitafuata hapo baadae. Kwa kifupi Rais akikaa madarakani kwa kipindi cha miaka 7 kuna faida nyingi sana kuliko muda wa miaka 5 ambao ni mfupi sana. Kwa upande wa Wabunge natumaini mnaelewa zaidi nini “faida” ya kukaa Bungeni kwa miaka 7 kuliko miaka 5 ya sasa hivi.

Najua humu ndani ya JF kuna Wabunge wengi sana wa CCM hivyo ningewashauri haraka sana andaeni hoja binafsi ya kuongezwa muda wa Rais ili muiwasilishe kwenye kikao cha kwanza kabisa cha Bunge cha mwaka 2018. Tena msiwe na hofu sababu Watanzania wengi tunamkubali sana Rais Magufuli. Nafahamu kuwa wapo wachache watakaopiga kelele; hao tumeshawazoea na kelele zao, hoja hii ikipita watakuwa wapole tu sababu siku zote demokrasia inaheshimu maamuzi ya walio wengi. Isitoshe upinzani wenyewe umeshaanza kupukutika, mpaka ifike mwaka 2020 watakuwa wamesambaratika kabisa. Kwasasa hivi sisi wana-CCM ndiyo tupo wengi hivyo tuna haki na wajibu wa kuamua mustakabali wa Taifa letu, na uamuzi huu siyo mbaya ni uamuzi wenye faida kubwa kwa Taifa na kwa Watanzania wote kwa ujumla.

Nawasilisha hoja.
 
Bila Shaka wew utakua ngamia au Mr mitako.Ubinafs tu umewajaa hakuna hoja hapa ni ushuzi tu kwakua mnanufaika na umafia wake.
 
Tutajie mafanikio yke toka aingie madarakan,,,,
 
Akili zako ziko kwenye kishundu kama za nkamia, mzoga takataka wewe
 

Mwendawazimu ni hatari kwa maendeleo ya Taifa.

Tuna ndoto ya Nchi ya Viwanda, lakini hadi sasa kiwanda kidogo ni vyerehani 4.

Halafu anatokea mpuuzi analeta mawazo mgado kama haya! Serious?
 
Hivi mtu akikutukana, atakuwa anakuonea? Acha akili za kibinafsi na kibaguzi. Usijione wewe nduo unaakili kuliko watanzania mil 50. Kila mmoja ni raia wa Tanzania na wote wana haki sawa ya kugombea na kutawala.
 
Kwani chato mashamb yamejaa kuwa akitoka madarakani kazi zitakuwa zimeisha
 
Mchukue ukampe uongozi wa familia yako...akutawale wewe na mkeo na watoto wako....hata milele.haitatuhusu....waafrika ni wapumbavu sana na tunatumia mizuka na hisia kuliko akili....Kwa nin hamjifunzi tu kwa baadhi ya nchi watu wanavoheshima katiba zilizopo.....
Kwa hiyo akija raisi mwingine akavurunda kwa mtazamo wako tutabadirisha katiba akae miaka miwili sio?
Halafu utakuta wewe ni mtu mzima kabisaaa....
 
Mr mitako acha ubinafsi,jehanam inakusubir kwa umafia mnaoufanya.Ht 14sio mingi mtataman kuongeza.Mtu aliyezoea kula nyama za watu haachi!!!
 
Kama ni mzalendo aheshimu Katiba iliyomweka madarakani na aliyoapa kuilinda na kuitetea!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…