Rais Magufuli: Sitasomesha Wanafunzi waliopata ujauzito, siwezi kusomesha Wazazi

Rais Magufuli: Sitasomesha Wanafunzi waliopata ujauzito, siwezi kusomesha Wazazi

Rais Magufuli huo NI UJINGA, kwa kiingereza, IGNORANCE. hata hao unaowahutubia wanashindwa kupiga makofi. Elimu ni HAKI YA MTU. Vile vile Rais siyo wa kuamua na kuelekeza mambo kama hayo. kuna vyombo vinavyohusika katika maamuzi, baada ya michakato. hatukumchagua Rais kutuamulia kila kitu. Rais hana mamlaka ya kuamua nani asome na nani asisome. Mengine inabidi tu tumwambie Rais ukweli wake, kwa sababu yeye ni Msema Kweli na ni mpenzi wa Mungu
Elimu isiyo na masharti ni ujinga.Ni lazima kama mtu anataka kupata elimu vigezo na masharti vizingatiwe.Kama mwanafunzi anataka kuendelea na masomo yake ni lazima asipate mimba.Imefika sasa wakati ambapo wazazi ni lazima wa instil good manners kwa watoto wao.Visababu vya kijinga eti wapo wanaobakwa,mazingira ni hatarishi etc. ni unacceptable.Wangapi wanabakwa bwanaa? Mazingira ya zamani yalikuwa magumu zaidi kuliko ya sasa, lakini wanafunzi waliopata mimba hawakuruhusiwa kuendelea na masomo,iweje leo.Watoto walitembea km. 30 kwenda shule na kurudi miaka hiyo na wengi hawakupata mimba why today.Sababu ni bad manners.Jamani sio siri, vitoto vya siku hizi vina very bad manners.
 
Wewe sio mzazi. Kama una watoto labda sio wa kike. Kama unao basi sio baba muwajibikaji. Tunaotatizwa na kauli hizo ni sisi wazazi sio hao watia mimba. Wao watatia mimba na watakimbia. Kazi itabaki sisi wazazi tunaotegemea shule hizi za kata!

Mmmhhhhhh.

Elimu , bila vigezo ni sawa na elimu ya enzi za Ujima na zama za mawe.
 
Dah, inasikitisha sana kuwaona watu kama nyie mnashangalia suala la mtoto wa kike kunyimwa haki yake ya msingi "Elimu". Kuna msemo usemao "mtoto akiunyea mkono haukati", sasa kwanini mtoto wa kike akibeba mimba anyimwe haki yake. Mm nina mdogo wangu alibeba mimba akiwa shule ila alifanikiwa kuendelea na masomo yake na baada ya kujifungua alilea mtoto miezi mitatu akarudi shule kama kawaida. Mimba sio ulemavu na kupata mtoto sio mwisho wa maisha.


Alipokuwa anapanua , hakujua kuwa wapanuaji watataka zaidi na kisha atapata ujauzito!?

Acha nao, waisome namba ndiyo akili zitawarudi na wakome kabisa.
 
One In a million huyo ukweli usemwe tu Nchi itoe Tangazo kuwa atakaepata mimba arudi shule wanafunzi watasoma kweli? ukijua saikolojia ya watu walio katika mobb maamuzi kama hayo ya kuwaruhusu ni sawa kumfunga mfugo katika shamba la mazao!! Naomba nikuulize ile ishu ya mbeya day iliishaje baada ya wale wanafunzi kutetewa sana na ukweli ulipojulikana ni hatua zipi zilichukuliwa??

Tanzania lazima ibaki katika misingi yake kulinda maadili yanayoporomoka kila siku leo mnapiga kelele kwa huyu inaonekana mmesahau kauli ya "viherehere vyao" ya mtangulizi wake yote ni katika kusaidia kizazi cha watanzania na si kuendekeza mambo yasiyo na maadili kama hayo.

Kesi za kubakwa naamini zinaripotiwa katika maeneo husika na mwanafunzi kama huyo sidhani kama kuna kosa la kuendelea na shule kama kweli atathibitika alibakwa. Lakini si kuruhusu watu wa do na wapate mimba then warudi shule Hilo HAPANA.

Kulinda maadili yapi? Unajua unajifanya utasema Tanzania tuliwahi kua na kitu cha kujidai huko nyuma, hakuna hata kimoja, huko nyuma wazee walikua wanabaka tu wanawake bila consequences, hata leo hii vijijini ni hivyohivyo, angalau tena imepungua miaka ya hivi karibuni.

Tunang'ang'ania misingi ipi wakati hatuna lolote tumefata tunachojua miaka mingi toka tupate uhuru na bado nchi masikini ya kutupa. Watu eliku hawana, viongozi hata kusoma wengine hawajui. Hivi we unavyoona unaona tuna cha kujidai kweli? Toka nje uone.

Hizo nchi mnazosema watu wanatembea uchi nimeishi miaka zaidi ya 8 sasa, wadada kutembea na vikaptula vidogo sana vinabana hamna anayewasumbua, hamna ubakaji uliokithiri ka bongo, na watoto wana heshima, uvaaji wanaona kitu cha kawaida tu sio kukaa wanakodoa mimacho ka wabongo. Ila juzijuzi tu huko wametaka kumvua dada wa watu nguo mbele ya watu kisa kavaa miniskirt, kuna joto avae vipi sasa?

Yaani watanzania mmekaa kwenye bubble ya ujinga mko comfortable mnahisi the whole fckn world revolves around you, hamna cha kujidai Tanzania HATA KIMOJA, ni muda tubadilike tuige sasa mazuri wanayofanya wengine.

We unadhani kila aliyepata mimba alipenda? Dont be stupid, angekua mtoto wako ungejua uchungu wake ulivyo, sometimes shit happens, mlee mtoto vizuri na mpe elimu ajue jinsi ya kujikinga sio mnakaa kutoa adhabu za kipumbavu, sasa mdada aache shule, mkaka jela 30years, huyo mtoto anayeletwa duniani hivi ataishia wapi kama sio kuzoa takataka? Mama kazi hawezi pata, baba jela. Umeongeza watu watatu kwenye umasikini bila sababu ya msingi.

Akili ndogo. Mnaboa aisee
 
Kwahili namuunga mkono, lazima tuwe na nidhamu kwenye elimu
 
Haya wanafunzi kazi kwenu masomo au yale mautamu!na hakikisheni hambakwi mana itakula kwenu
 
Elimu ni kumuwezesha haina uhusiano wowote na kuwa mzazi au la.

Kachanganya mbivu na mbichi
 
Kama kweli kasema hivyo basi kapotoka sana na sikubaliani naye kabisa.

Mwanafunzi wa kike kupata ujauzito siyo kosa kubwa hivyo hadi anyimwe fursa ya kujiendeleza kielimu.

Hapo adhabu haiendani kabisa na kosa!
Wewe si ni mpiga debe wake mkuu sasa imekuwaje?
 
Mwanao akipata mimba , akishajifungua mpeleke private asome basi
 
Sema miaka 30 pia ifutwe, hiyo miaka aachwe amtafutie Kijacho na mamaake maisha...
 
Duh! Mkuu katema cheche za maana. Kwa namna yoyote ile kama kuna mtoto alishaanza kufurahi kudonolewa amenywea. Safi!
Mkuu watoto wa shule kupata mimba kuna sababu nyingi sana na nyingi ziko nje ya uwezo wao. Elimu ndogo ya afya ya uzazi, umaskini, mazingira yasiyo rafiki ya kusomea, ufataki wa bahadhi ya wanajamii, utandawazi na nyinginezo. So huwezi toa hukumu ya jumla na kumsifu mkulu kwa kauli yake iliyojaa ukakasi kiasi hicho. Ni suala linalohitaji mjadala mpana ili hawa watoto wapate fursa nyingine ya kuendelea na masomo. Nimekuwa mwl tangu 1997 na nimeona mabinti waliopata bahati ya kurudi shule baada ya ujauzito sasa wako mbali sana kimaisha na wanamchango muhimu kwa jamii. Wale walioikosa hiyo fursa wengi wao wameishia pabaya kwa kweli,wakiuza mboga mboga, kutembeza karanga na ili hali walikuwa na uwezo mzuri tu darasani.
 
Huwezi kusomesha wajawazito,, dunia nzima hakuna, hata ULAYA hawafanyi hivyo, Ukizaa unasoma kama mtu mzima, ukichanganywa na watoto wataiga mwenzao,,kale kamchezo lazma kawekewe sheria
Mi naomba nikuulize,
Kabla ya hii kauli ya mheshimiwa kwani utaratibu ulikuaje?
Nakumbuka Mwanafunzi akipata mimba shuleni anafukuzwa.
Sasa mbona hyo mbinu haijazaaa matunda hadi leo!!???
 
Alipokuwa anapanua , hakujua kuwa wapanuaji watataka zaidi na kisha atapata ujauzito!?

Acha nao, waisome namba ndiyo akili zitawarudi na wakome kabisa.
Ni vigumu sana kujua upendo na uchungu wa mzazi kwa watoto kama wewe mwenyewe si mzazi.
 
Ni hoja dhaifu sana ambazo zina nia ya kuzidi kuingiza jamii yetu kwenye dimbwi la immorality.Hii haikubaliki na hatutakubali.Ni wazi kwa mtu yeyote anayelitakia taifa letu mema kwamba maamuzi ya kuwaruhusu wanafunzi waliopata mimba na kujifungua warudi shuleni yanahamasisha umalaya.You do not need a PhD to know this.Hili hatuko tayari kulivumilia.
Hahahahahah
Critical thinking is better than argumentation!!
No body is fighting with anybody ideologically.. What you have to do is to THINK be for you argue!!!

Tafsiri ya kisheria ni kwamba mwanafunzi akipata mimba amebakwa!!!
Na adhabu yake Ni kifungo kisichopungua miaka 30 jela.

Kama Ni hivyo unawezaje kumwita mtu aliebakwa immoral!!?

Nakama hoja Ni maadili Na yakwamba waschana woote wanaopata mimba Ni umalaya hivyo kurudi shule Ni kuendekeza utovu wa nidhamu Na uvunjifu wa maadili mema..

Kwanini tusianze Na kufuta Sheria ya SOSPA!!!
Na wafungwa woote waachiliwe huru mana hawakubaka isipokuwa walijipatia uroda kwa Malaya!!
 
Back
Top Bottom