Rais Magufuli: Sitegemei kutangaza hata siku moja kwamba tunajifungia ndani (Covid19), tutaendelea kuchukua tahadhari zingine za kiafya. Akemea Chanjo

Hovyo hovyo ya jiwe ni hatari.
 
Ndiyo baba kaza buti twenda tunakunywa mtori na nyama tutazikuta chini 🤣 🤣 🤣🤣
 
Magu ni denialist, kama hataki chanjo sisi tunaitaka. Sisi wengine hatutaki kufa..
Kwa ufupi ktk kipindi kigumu wananchi wanatarajia kumsikia kiongozi wao anaongea maneno ya matumaini lakini leo tumesikia pumba zaidi zikizungumzwa! Ndugu zangu baada ya hotuba hiyo ya hovyo nawaomba mchukue hatua za kujilinda wenyewe. Hakuna msaada toka ktk kodi zetu.
 
Hakuna mtu anayetaka lockdown lakini serikali isimamie mapambano haya kwa mfano,Kukiri kuwa ugonjwa upo,kurudisha tahadhari kama za kuvaa barakoa na kunawa na maji tiririka na sabuni, kupunguza misongamano isyo ya lazima. Wengi tumelegeza mapmbano haya.
 
Sasa wizara ya afya ikifuata kanuni na taratibu zake maana yake chanjo haiepukiki-nashangaa Rais anasema wizara ya afya iwe macho kwani hii idara siku hizi inafanyia kazi matamko au taaluma?
 
Hatukuwahi kukaza kwenye mapambano ya corona,hata sasa mtu atakubali kabisa corona ipo ila hawezi kuwa serious kwenye kuchukua tahadhari. Tizama hiyo picha mwaka jana wakati serikali imekataza kusimamisha abiria kwenye na hicho ndio walikuwa wakikifanya Wabongo.

 
Sasa wizara ya afya ikifuata kanuni na taratibu zake maana yake chanjo haiepukiki-nashangaa Rais anasema wizara ya afya iwe macho kwani hii idara siku hizi inafanyia kazi matamko au taaluma?
Nmesikitika sana ,nmesikitika sana nikiwa kama Mtaalam wa Afya

Kauli hii ya Kubeza Chanjo

Maana yake anawaaambia wamama sasa wajawazito na watoto, waanze kuzikimbia Chanjo.


Ivi nin hii???
 
Maneno ya matumaini ulitaka awaambieje? Kwamba mnaletewa chanjo?
 
Sasa wizara ya afya ikifuata kanuni na taratibu zake maana yake chanjo haiepukiki-nashangaa Rais anasema wizara ya afya iwe macho kwani hii idara siku hizi inafanyia kazi matamko au taaluma?
Waanze na zile za wapeazo watoto wadogo clinic
 
Mungu yupi huyo anayependa Tanzania tu akiacha nchi nyingine zote za dunia zikiteseka na hili gonjwa ikiwa ni pamoja na Italia kwa Baba Mtakatifu wa Rais wetu mpendwa? Huyo ni mungu wa Chato!
Ulishawahi kujiuliza pia inapotokea ajali, Gari laweza kupinduka likauwa karibu Abilia wote, lakini akasalimika mtu mmoja Tu!! Je hapo Napo itakuwa Mungu aliwachukia zaidi hao waliokufa na kumpendelea aliyesalimika!?

Dunia na watu wote ni shamba la Mungu, na anapoamua kuvuna shamba lake, ni yeye Huamua aanzie wapi na amalizie wapi, avune wapi na aache wapi!!

Mtegemee Mungu wewe!
 
Mimi ni CCM damu damu lakini lazima niseme ukweli kuwa huyu jamaa ni kichaa. Haiwezekani rais wa nchi anaongea mambo ya kipuuzi na mna hii tena ni Dr. ambaye nchi imetumia hela kumsomesha.
Huyu hajasoma hata Shule ya Msingi Chato maana toka aingie madarakani hajajitokeza hata schoolmate mmoja wala mwanafunzi aliyemfundisha akiwa mwalimu. Nyerere alipoingia tu madarakani hata Mprof waliofundisha Chuo Kikuu Ulaya walijitokeza kumsifu kuwa alikuwa mwanafunzi mahili!
 
Si ndio nyie mnaowaita watu wanatafuta uteuzi pindi wanapoamua kumsifia Rais??

Pumbavu.. na hata hao unasema wakijitokeza kumsifia ualimu wake, utaponda tu! Unalamaana basi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…