Uchaguzi 2020 Rais Magufuli, Una hofu na matusi gani wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu!?

Uchaguzi 2020 Rais Magufuli, Una hofu na matusi gani wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu!?

RockCarnegie

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2019
Posts
963
Reaction score
1,927


Habari wana JF

Leo wakati Rais Magufuli akivunja bunge, katika hali inayoonyesha hofu ya kutojiamini kuelekea Kampeni za Uchaguzi Mkuu ujao, ametadharisha kuwa watakokuwa wanatoa matusi watashughulikiwa!

'Matusi' ni neno la jumla sana, na sidhani kuna watu waliomuelewa ni matusi gani ambayo hayataki kuyasikia Rais wetu mtukufu!

Ninavyofahamu vyombo vya ulinzi na usalama husimamia sheria, je haya matusi yanayomkwaza Rais yapo kwenye sheria ipi na ni yapi ili tuwe makini tusije tukaingia kwenye matatizo wakati tukishusha nondo majukwaani wakati wa kampeni!?

MATAGA tusaidieni kujua kipi hampendi kusikia, maana nyundo mbili tu za ununuzi wa midege na ujenzi wa uwanja wa Chato za John Pambalu zlitosha kusitishwa kwa kipindi cha Ajenda 2020 cha Star TV!

Nionavyo ni kuwa rais na CCM wana hofu kubwa hawana uhakika kama wataungwa mkono na wananchi wakati wa kampeni na hatimaye uchaguzi.

Nawasihi watakaokuwa majukwaani kunadi hoja na sera kutoka upinzani wajiamini na washushe nyundo za ukweli bila hofu, kwani wananchi wameshachoka kusikiliza mapambio ya kusifu na kuabudu!
 
Anataka watu wasiongelee makosa yake. Wasimseme kabisa! Time will tell, save this thread!

Kweli kabisa, matusi anayoyazungumza yeye ni ukweli unaosemwa dhidi yake. Hata hii kuzuia mikutano ya kisiasa, na kauli zinazorudiwa mara kwa mara kuwa kuna vyama vinatukana kwenye siasa, ni katazo lake binafsi la kuusikia ukweli mchungu. Hiyo ni kwasababu hawezi siasa za ushindani, bali anaamini kwenye siasa za kusujudiwa.
 
Kweli kabisa, matusi anayoyazungumza yeye ni ukweli unaosemwa dhidi yake. Hata hii kuzuia mikutano ya kisiasa, na kauli zinazorudiwa mara kwa mara kuwa kuna vyama vinatukana kwenye siasa, ni katazo lake binafsi la kuusikia ukweli mchungu. Hiyo ni kwasababu hawezi siasa za ushindani, bali anaamini kwenye siasa za kusujudiwa.
Exactly, kusikia kuwa amenunua ndege bila ridhaa ya bunge hayo ndiyo anaona ni matusi!
 
Amefanya vizuri kuonya. Nadhani tutaendesha campeni za kistaarabu
 
Huyu jamaa ana ngozi laini sana ile peacemaker ya kwenye moyo wake inamfanya hasiwezi kabisa kusikiliza habari zidi yake, Jiwe haziwezi challenge kabisa yeye anataka asifiwe tu.

Hutu akimaliza muda wake atakufa mapema sana maana atatukanwa na CCM na Wapinzani.
Hakika. Siasa ni ngumu sana kama hukujiandaa kuwa mwanasiasa
 
Back
Top Bottom