Rais Magufuli: Wasiotutakia mema wanatumia Asasi za Kiraia na NGO kutuhujumu ili kufifisha jitihada zetu kujikomboa kiuchumi kwa maslahi yao binafsi

zebedayo musibha,
Ni kweli mku kwani wao wakitupa sapoti alafu ulaji wao uzibwe si watabaki wananing'inia? Mbinu chafu zipo tu ni kutafuta njia ya kuzikwepa.
 
Anatafuta "The Scapegoat" baada ya kuonekana uchumi unaenda kombo na fedha za kutekelezea hiyo miradi inaonekana haipo.

Inaonekana Tanzania inapoteza Special Drawing Rights Status kufuatia rekodi yake mbovu ya haki za binadamu.

Wakati mtu unakiuka haki za binadamu na ni wazi hauna plan B una A tu ambayo ni kutegemea wahisani/mabeberu ni wazi utakwama tu na hicho ndicho kilichoiponza Zimbabwe, Venezuela, Iran, North Korea nk na sisi sio exceptional, tukicheza tutaungana na hao jamaa very soon.

Tanzania haina uwezo wa ku-finance bajeti yake hata kwa nusu hali inayoiacha at the mercy of the donor countries ambao sharti lao kuu la kukusaidia ni kuwa na viwango vya juu vya rekodi ya haki za binadamu.

Kwani mkiheshimu demokrasia na haki za binadamu hamuwezi kuleta maendeleo..??? Nauliza tu make inaonekana wengine wanaamini hivyo sawa na wale wanaoamini kuwa huwezi kuwa tajiri hadi ufanyiwe uchawi. Very hopeless.
 
Madikteta wote duniani ndo huwa hivyo wakiona kuna dalili za kushindwa kitu huko mbeleni. Hapo anatafutwa mbuzi wa kafara. Mtu huwi mzalendo hadi umsifie jiwe?? Wasaafu wasiongee la sivyo wanawashwa washwa isipokuwa wanaomsifia tu
 
ugonjwa si wakupuuza, chamsingi ni wakisema ipo tuna chukua hatua za tahadhari mapema kuhakikisha haipo kweli,
Hivi mtu anayekupenda akikwambia Oya, Funga zipu ya suluali, Je huyo hakupendi? Unataka utembee barabarani uchi wa mnyama? ''The word to the wise man suffices"
 
Wakati huo huo, hawa anaoona wanamuhujumu, ndio hao hao wanaompa pesa ikiwemo mikopo ili atekeleza miradi anayoitumia kujitukuza!!
 
Kauli yangu huwa ni moja tu.

We are fighting for a better tomorrow.

Acha vyuma vikaze tu, maana tukisema tutafute kiongozi mzuri zaidi ya huyu napo kuna kujikuta tunaangukia pua tu, maana hupinzani hakuna.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mabeberu yakiambiwaga ukweli yanafura sana, demokrasia ni kichaka cha kujificha cha mabeberu kufanya unyonyaji na maslahi mengine kadha wa kadha kwa nchi zinazoendelea
 
Kulalamika hakutamsaidia yeye kaamua kupambana nao sasa asonge mbele atakaeshindwa anyooshe mkono japo mshindi anajulikana!!! Twende nao hivo hivo washashika kila nyanja hapa duniani
 
Tuandamane au tufanyeje!! Mabeberu yanawajambisha Wachina,warusi, waajemi,wahindi sembuse sisi afrika akili ndogo ,,mkuu unajidanganya mchana kweupe tukubali hii dunia ni yao hivyo tushirikiane nao
 
Tuandamane au tufanyeje!! Mabeberu yanawajambisha Wachina,warusi, waajemi,wahindi sembuse sisi afrika akili ndogo ,,mkuu unajidanganya mchana kweupe tukubali hii dunia ni yao hivyo tushirikiane nao
 
We mwimba kwaya ebu tupe mfano hali ilikuwaje kabla ya mabeberu kuleta chanjo,,Idadi ya wagonjwa wa polio ikoje ukilinganisha na awali!!!? Tumia akili yako kutoa maoni sio unaanza eti kama mwenyekiti alivyosema hapo mbele
 
Na bahati mbaya mxungu hatishwi
 

Kimoja hapa si cha kweli hakuna uhusiano mbaya wa demokrasia na maendeleo. Nchi nyingi zina demokrasia na maendeleo. Kama kuna mbinu za kuaminisha Watanzania eti tusiwe na demokrasia kwa kisingizio cha maendeleo Watanzania si wajinga hivyo na haitafanikiwa. Tujue kama Nyerere alishidwa na kuamua yaishe na kungatuka sio hivyo tu na kuwa mpiganaji wa kwanza wa nyama vingi nchini! Huwezi kuja sasa kwa sababu zako ukadanganya Watanzania. Wanaweza kulazimisha na kupora lakini mioyo ya Watanzania wengi wanapenda demokrasia na ni utamaduni wao sio China au Rwanda hii.
 
Mamlaka ishasema haupo wewe ni nani ulazimishe upo?
sasa kama wataalamu wamethibitisha haupo wewe unashadadia nini? jambo likizungumzwa linachunguzwa linapatiwa majibu then topic closed, kinachokufanya uzidi kuchokonoa ni nini, au nawewe una nia ovu?
 
Watawala Wa kiafrika wakifikia ukomo Wa kushindwa kuwaletea maendeleo watu wao usingizia mabeberu,hivi mtu aliyekuacha nyuma miaka 300 akuonee wivu iweje,SGR wanazo toka miaka ya 50 na washatoka huko wako kwenye technology ya hyperlooper transportation ndio watuonee wivu tusiokuwa na uwezo Wa kujenga hata vyoo vya shule.Wenzetu wamewatumia mabeberu wako mbali,hakuna taifa lililowahi shirikiana na mabeberu likawa fukara.Watawala Wa kiafrica wanawananga mabeberu sababu ni kikwazo kwao kung'ang'ania madaraka hivo utumia mnango huo ili kupata sapoti toka kwa wajinga.Nyerere aliwananga na kuwaponda sana mabeberu lkn akipewa misaada akatai,alipotakiwa kupinduliwa aliomba msaada kwa mabeberu alipopigwa njaa akaomba msaada kwa mabeberu wakampa maindi ya njano na maziwa.Watawala Wa kiafrica kuwaamini yatakiwa uwe umelewa.Watawala wa kiafrica ndio chanzo cha ufukara wa waafrica,jiulize mbona wakoloni waliwezawaletea maendeleo Waafrika wao wameshindwa nini kwa mazingira hayohayo maana mkoloni alirudi kwao na begi na akili yake tu kila kitu aliacha Africa.Kwann nchi zisizo za kiafrica tulizokuwa nazo sawa kimaendeleo Leo ziko dunia ya pili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…