Rais Magufuli: Watanzania endeleeni kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Korona. Sijazuia matumizi ya Barakoa!

Rais Magufuli: Watanzania endeleeni kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Korona. Sijazuia matumizi ya Barakoa!

Ewe Mh. Rais waambie watu wako pia wasivae mitumba kwa kuwa nayo inatoka nje, mabeberu wasije pandikiza virusi humo wananchi wako wakaangamia.
 
Kwahiyo mmeridhika, hadi muambiwe mvae barakoa ndio mfurahi. Vaeni sasa baba yenu kasema
Yeye ndo aliongoza kuzodoa watu wanaovaa Barakoa kila mkutano aliohudhuria. Mfariji mkuu anapokuwa mzodoaji mkuu unategemea faraja hapo? Wewe ifike jioni kuna baridi mtoto wako mmoja avae sweta watatu waendelee kucheza kifua wazi , unapotokea unamzodoa aliyevaa sweta na kuwasifu wanaotamba kifua wazi. Kesho wakiugua Pneumonia umlaumu aliyevaa Sweta au watoto waliocheza vifua wazi?
 
Hii paragraph imehitimisha nia ya serekali katika kupambana na janga la corona ni ipi.

Imagine social distancing pamoja na kuvaa barakoa vimepondwa na kuonekana kuwa havina maana na maombi yamewekewa msisitizo!View attachment 1708025
Wewe uelewa wako ni mdogo. Hoja hapo ni ufanisi wa lockdown na social distancing
 
Yeye ndo aliongoza kuzodoa watu wanaovaa Barakoa kila mkutano aliohudhuria. Mfariji mkuu anapokuwa mzodoaji mkuu unategemea faraja hapo? Wewe ifike jioni kuna baridi mtoto wako mmoja avae sweta watatu waendelee kucheza kifua wazi , unapotokea unamzodoa aliyevaa sweta na kuwasifu wanaotamba kifua wazi. Kesho wakiugua Pneumonia umlaumu aliyevaa Sweta au watoto waliocheza vifua wazi?
Unavaaa barakoa hata ukiwa peke yako? Kwa nini usizodolewe?
 
Viongozi wa nchi hii, hasa Rais mwenyewe, wanaongoza kutuchanganya wananchi sana. Hatujui wanalipeleka wapi taifa. Hawa watu sijui vipi.

● Mwezi mzima wanaropoka "NCHI HII HAINA CORONA", na wana aminisha raia kwa kutokuvaa barakoa wala kuzingatia mita moja ya kujiepusha katika mikusanyiko yao, wengine walifikia hatua ya kuvua wenzao barakoa kwa nguvu kisa mamlaka.

● Viongozi wengine walienda mbele zaidi na kusema ni "SHULE YA ISM MOSHI KUTANGAZA INA WANAFUNZI WAWILI WAMEKUTWA NA CORONA NI YA UONGO, HIO NI VITA YA KIUCHUMI".

● Wengine kama Makamu Mkuu Wa Chuo Cha Open University baada ya kutoa wito kwa wanafunzi kujihadhari na kuchukua hatua stahiki kujilinda na Corona, aliamrishwa na Wizara Ya Elimu "AOMBE RADHI KWA KUTOA WITO ULE", zaidi ya yote Mkuu wa chuo nae akamruka hatua 100 na kusema sio wito wa chuo, ni wito wake yeye binafsi.

● Leo Wizara ya Afya inaomba wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya Corona, kwa kunawa na maji tiririka na kuvaa barakoa. Wakati wao ndio walikua vinara kupinga kuwepo kwa Corona nchini, licha ya wananchi kupiga kelele kwa kupoteza wapendwa wao.

● Sasa tunasikia mkuu wa nchi akitoa wito wa "MAOMBI SIKU TATU YA KUMWOMBA MUNGU KWAAJILI YA KULIOMBEA TAIFA".

"MUNGU GANI ATAKAESIKIA MAOMBI YA TAIFA LENYE VIONGOZI WASIO WAKWELI NA WANAFIKI???? SI VIONGOZI WA DINI WALA WA NCHI" Kuomba huko ni sawa na maombi yaliofanywa na watu wa Sodoma Na Gomora baada ya ahadi ya adhabu ya mungu kuwafika, saa ilipofika ilifika, milango ya maombi na dua ilifungwa, na adhabu haikuchagua watoto wala wazee.
 
Tunataka kauli kama hizi, ikibidi ziboreshwe zaidi kwani walipa kodi wako ndio wanaoangamia, naamini sasa tunaanza kwenda kwenye njia moja.
 
Ofcourse Serikali ni vigumu kuzuia mtu (Ingawa kule Moshi kuna mtu ambaye yupo Serikalini aliwaambia watu wazivue)..., pili dhihaka na yeye kusifu watu ambao hawajavaa ni msimamo tosha wakufanya watu wanaovaa waonekane ni wa ajabu.

Pia tujihadhari na Barakoa tu zinazotoka nje ?... Je vipi mitumba, Misaada, Magari, TV, Electronics, Simu, Madawa, Mafuta, Sukari, n.k. Hivyo ni Salama (au ndio kuzua taharuki ?)

Hivi TBS na Taasisi zote zinafanya nini ? Kwanini zisizuie vitu ambavyo sio salama au kuvipiga marufuku ?, Mimi mteja mtaani ninayenunua nina vipimo au ninajuaje kwamba hiki sio salama ?, Au ndio mwanzo wa Trade Wars na kusema kila kinachotoka nje ni sumu ? (Kama ndivyo hio ingefanikiwa tu iwapo tungekuwa tunajitosheleza kwa quality na quantity) unless otherwise ni kuzidisha taharuki na sintofahamu kwa wananchi.. (watu wataogopa kutumia oil wakidhani in Corona)
 
Tulipigwa
Hili ni janga, Marekani walipoona maisha yao yanachezewa na mtu mmoja wakapiga chini. Wapambe wakajitokeza kulazimisha, wenye busara wakasema uhai wetu ni MUHIMU kuliko mtu mmoja. Bila kumtupa YONA Baharini tutakwisha.
 
Back
Top Bottom