Rais Mwinyi wa Zanzibar naye atakuwa anamuachia Mama awe anaenda Safari zake kama Mama afanyavyo Kwake?

EeenHeee, mada hizi!

Wengine tuna'admire' guts alizo nazo mama.

Naona mwana mama ni kama alikuwa amejiandaa kwenye nafasi hii.

Atawachokonoa wenye roho hadi zitapasuka, na hakuna mtakachoweza kufanya!

Mkiropoka, VUNJA!! Hapo mama na kundi lake watakuwa wametimiza lengo.

Sasa 'mta DO?
 
Uwe na adabu mkuu....

Hamkumpangia majukumu VP kipindi cha hayati JPM.....basi mnampangia Rais leo hata wa kumtuma kumuwakilisha ?!!! Khaaaa

Pathetic
Hapana.

Kama ni "Pathetic", wewe inakuhusu sana, kwa sababu umefumba akili , macho na kila kitu, usiweze kuelewa chochote!

Sema, kama ameamua kuvunja utaratibu wa mpangilio wa uongozi chini ya Jamhuri ya Muungano..., basi afanye hivyo kwa kujua anavunja utaratibu huo kwa maksudi.

Hilo haliwafanyi wanaohoji kuwa "Pathetic."
 
Huu ni mfano dhahiri kuwa nchi bado inaongozwa bila kufuata kanuni tulizojiwekea na ni msisitizo kuwa bila katiba mpya tunaweza kurudi tulikotoka.
 
Paul Makonda alikuwa anatumwa na Hayati Rais Dkt. Magufuli ' Kumuwakilisha ' katika Safari zake za Kimataifa ili Kuiwakilisha nchi pia? Kuna Watu huwa mnanilazimisha niwe nawadharau kwa Upumbavu wenu wa Kurithishwa.
Huyu nae hana anachokijua!! Mpuze tu!
 
Mwingine yupo SADC mwingine yupo ana cheza na panya SUA, Kazi iendelee il karma hatari inaweza kukutafuna hata kaburini, Mwendezake alimpuuza leo ndio Namba moja
 
Yeye Mama aliwaambia Urais hautaki 2025? Hivi kwa Afrika hii uijuayo Wewe kuna Mtu ' akiuonja ' tu ' Urais ' atatamani Kuondoka mapema Madarakani na Kumkabidhi Mtu mwingine ' Kiurahisi ' tu kama msemavyo?
Yule mama alikataa kugombea Zanzibar mwaka 2020 akisema hiyo itakuwa ni demotion kwake!
 
Kuna Siri gani kati ya Samia na Hussein?
 
Kwahiyo 'Mama' anakosea au anapatia?
 
Nashukuru kwa wengi kuona Tatizo hili.
 
Huyu mother Theresa aambiwe ukweli aache ujanja wake wa kuipa fursa zenji, kwenye mambo ya msingi ya JMT.
Binti tulia hebu.

Haya mambo usiyaangalie tu juu na wala usiwe kichwa mchunga. Karibu kiembe samaki kwa Butros upate urojo uliokwenda shule.
 
Una uhakika Kichwani Kwako zimetimia?
 
Kwa maana hiyo rais kavunja katiba ?
 
Tunachokisema ni Mama aachwe afanye kazi na neema zitapatikana kwa kila mmoja wetu
 
Ninakubaliana nawe ' Mama ' anakosea.
 

Huu ni mfano dhahiri kuwa nchi bado inaongozwa bila kufuata kanuni tulizojiwekea na ni msisitizo kuwa bila katiba mpya tunaweza kurudi tulikotoka.
Tafadhalini 'Mama' aambiwe anaharibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…