Makonde plateu
JF-Expert Member
- Nov 19, 2022
- 1,443
- 3,480
RAIS Samia Suluhu Hassan amesema ni lazima vijana wabadilishwe mitizamo yao juu ya fursa mbalimbali zinazopatikana Afrika na kuondoa ile mitizamo ya kwenda nje ya bara hilo kutafuta maisha.
Rais Samia ameyasema hayo leo Julai 26, 2023 katika mkutano wa Wakuu wa nchi za Afrika kuhusu rasilimali watu unaoendelea katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julias Nyerere Dar es Salaam.
Idadi kubwa ya vijana tulio nao Afrikia ni fursa ya pekee kwa mageuzi ya uchumi wetu, kuliko kuwaacha wavuke bahari wapigwe njiani wazamishwe, kwa ajili ya kusema kwamba wanakwenda Ulaya kutafuta maisha bora, maisha bora watayapata Afrika tukiwaendeleza,"amesema Samia
Aidha Rais Samia amesema ni lazima elimu ya uzazi itolewe kwa vijana ili kuendana na hali ya idadi ya watu ilivyo kwa sasa katika bara la Afrika.
Ni lazima tuwafundishe watoto wetu kuhusu uzazi wa mpangilio, Afrika tuna idadi kubwa sana ya watu na hii inaweza kutuletea tija au kutuletea mambo yasiyofaa kama hatutoitumia vizuri" amesema Samia.
Rais Samia ameyasema hayo leo Julai 26, 2023 katika mkutano wa Wakuu wa nchi za Afrika kuhusu rasilimali watu unaoendelea katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julias Nyerere Dar es Salaam.
Idadi kubwa ya vijana tulio nao Afrikia ni fursa ya pekee kwa mageuzi ya uchumi wetu, kuliko kuwaacha wavuke bahari wapigwe njiani wazamishwe, kwa ajili ya kusema kwamba wanakwenda Ulaya kutafuta maisha bora, maisha bora watayapata Afrika tukiwaendeleza,"amesema Samia
Aidha Rais Samia amesema ni lazima elimu ya uzazi itolewe kwa vijana ili kuendana na hali ya idadi ya watu ilivyo kwa sasa katika bara la Afrika.
Ni lazima tuwafundishe watoto wetu kuhusu uzazi wa mpangilio, Afrika tuna idadi kubwa sana ya watu na hii inaweza kutuletea tija au kutuletea mambo yasiyofaa kama hatutoitumia vizuri" amesema Samia.