Rais Samia akataa mwananchi kueleza shida kwenye mkutano, amtaka amfikishie kupitia mbunge

Rais Samia akataa mwananchi kueleza shida kwenye mkutano, amtaka amfikishie kupitia mbunge

Rais Samia leo September akiwa Nangurukuru mkoani Mtwara alisimamisha msafara wake kuongea na wananchi wa eneo hilo. Moja wananchi hao aliomba kuongea jambo ambapo Rais alimwambia mambo ni mengi na Tanzania ni kubwa.

Rais Samia alimtaka mwananchi huyo ampatie jambo lake mbunge kisha amfikishie Rais au wasaidizi wake.

Mwaka 2017 Rais Magufuli akiwa anaelekea Mtwara alisimamishwa Somanga na mwananchi aliyeelezea changamoto ya zahanati katika eneo hilo kutokamilika kwa miaka mingi. Rais Magufuli alichangia na kuamrisha ikamilike.

Alipopita tena barabara hiyo miaka 3 baadae mwananchi huyo alimzawadia jogoo kama shukrani ya kutimiza ahadi ya kufanyia kazi dukuduku lake na Magufuli alimsubiri mpaka alipomkamatia na kumpa. Alipofariki, mwananchi huyo alifunga safari kumzika Rais Magufuli mwaka 2021.

Hakuna kipindi nchi yetu ilipata Rais wa ajabu kama kipindi cha jiwe
 
Mabango yenyewe yanaandikwa na UVCCM ya kumsifia Mwananchi akiandika bango lake huru ananyang'anywa na anaitwa CHADEMA habari zote tunazo.
 
Hao wanga tuu Magufuli walimzunguka wakiuliza shida zao na matatizo lakini ukatoka moshi wa ajabu. Safi sana rais Samia usiwasikilize kabisa
 
Huwezi kuongoza nchi kubwa kama Tanzania kwa mfumo wa Rais kusikiliza matatizo binafsi ya watu nchi ikasonga mbele.

Wenzetu wanaojua maana ya Rais, waziri mbunge inapofanyika town Hall meeting watu wanauliza, wanatoa malalamiko yao mapendekezo kwa masuala ya mtaa, mji, jimbo au taifa. Sio malalimiko ya umenyang'anywa kiwanja na tajiri au umefukuzwa kazini ambayo ni masuala ya polisi na mahakama.
Wewe kunguni umeona wapi kila mtu anataka kumpelekea matatizo yake raisi
Simple logic tu washampelekea mtu wa chini kama ni mbuge hakuna ufumbuzi
Zumbukuku wewe
 
Kama Kwa matope haya unayoyaonyesha umeyajaza kichwan ,nawee ndo Mfanya Vetting, kumbe ndio maana NCHI inajiendea endea, imagine Mfanya Vetting ndio mwenye matope ya namna hii .


Mjinga Mmoja wee.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Dokta sawa nitukane tu....

Tengeneza marafiki na si maadui....

Kuna scholarship ya Yale University inakufaa....japo kiburi kimekujaa kijana mwenzangu
 
Watanzania tupo million 61 na laki 7.Hivyo mh Rais hawezi kumsikiliza kila mtu,lakini kupitia wawakilishi wa wananchi na wasaidizi wa Mh Rais kila mwananchi anaweza kufikiwa na mkono wa Mh Rais na akatatuliwa shida yake.

Kila mtanzania anasikilizwa na mh Rais kupitia wasaidizi wake.Ndio maana ya uwepo wa mbunge ambaye umesikia alivyoekezea changamoto za wapiga kura wake ikiwepo changamoto ya barabara kipande fulani,pembejeo hasa madawa ya korosho,maji, n.k. wewe unafikiri akisimama njia nzima na kila mtu akasema kero yake unafikiri itachukua muda gani kumaliza kuwasikiliza maelfu ya wananchi wa Eneo moja tu?

Lengo la mh Rais kusimama eneo fulani ,kwanza ni kuwasalimu wananchi wake ,lakini pia kusikiliza kero zao za eneo husika kupitia mbunge wao wa jimbo husika. Na kutolea majibu ya papo kwa papo kupitia watu kama mawaziri kama ambavyo umeona akiwapa nafasi akina juma Aweso na wengineo. Lakini pia kuna wakuu wa mikoa,ma DC ,ma DED, mameneja wa maji na umeme mikoa n.k.
Hahahaha
Nakuona mshauri mkuu wa mavazi ya malkia ukielezea ubora wa vazi la malkia ambalo wasio na hekima hawatoweza kuliona......🤣🤣

The fall is real
 
Kazi ya Rais sio kutatua matatizo binafsi ya raia. Kazi ya Rais ni kushughulika na kuzungumzia mambo ya kitaifa na kimataifa sehemu yoyote anayoona inafaa kufanya hivyo.
Wewe kichwa maji kwa hiyo mwananchi akisema kuna shida ya maji au soko ni shida binafsi? Kwani alitaka kumuomba hela ya mboga ? Na umejuaje ni shida binafsi ikiwa hajasikilizwa? Na kiherehere cha kusimama njiani kilitokea wapi? Nani alimtuma au kumsimamisha? Na hapa alikuwa anaongea na Mbunge?
 

Attachments

  • IMG_0974.jpeg
    IMG_0974.jpeg
    54.6 KB · Views: 2
Wewe ni mjinga, unaona Sawa mwananchi kutosikilizwa na Rais ? Au hujui ujinga unaofanywa ngazi za mkoa na wilaya ?
Nitajie Rais Mkapa aliwahi kumsikiliza nani kwenye ziara zake , pole mjinga ni mimi ila wewe ni boya
 
Samia ni Rais wa mabango yaliyowekwa barabarani na kutuletea majambazi ya DP World na Ngorongoro.
 
Hapana, Rais anatakiwa ashughulike na mambo ya kitaifa. Huyo raia unaweza kukuta analalamikia kesi ya mirathi ya familia yao au kucheleweshwa mshahara kazini kwake.
Acha kumpigia mwananchi ramli ,je kama KERO yake ni ukosefu wa mafuta???.Kama mwananchi ametega sikio kukusikiliza basi na yy analakwake msikilize
 
Ndio ila kama raisi anatakiwa kuwapa nafasi ya kuwasikiliza. Wakati mwingine ni lazima uoneshe unajali. Hiyo ni elitism ndo anayotuonesha. Sio kila mbunge ana access na raisi wa nchi.
Mbona juzi kawaita wazee wa Mtwara kuwasikiliza?

Huyu Rais wa bahati mbaya sana
 
Rais Samia leo September akiwa Nangurukuru mkoani Mtwara alisimamisha msafara wake kuongea na wananchi wa eneo hilo. Moja wananchi hao aliomba kuongea jambo ambapo Rais alimwambia mambo ni mengi na Tanzania ni kubwa.

Rais Samia alimtaka mwananchi huyo ampatie jambo lake mbunge kisha amfikishie Rais au wasaidizi wake.

Mwaka 2017 Rais Magufuli akiwa anaelekea Mtwara alisimamishwa Somanga na mwananchi aliyeelezea changamoto ya zahanati katika eneo hilo kutokamilika kwa miaka mingi. Rais Magufuli alichangia na kuamrisha ikamilike.

Alipopita tena barabara hiyo miaka 3 baadae mwananchi huyo alimzawadia jogoo kama shukrani ya kutimiza ahadi ya kufanyia kazi dukuduku lake na Magufuli alimsubiri mpaka alipomkamatia na kumpa. Alipofariki, mwananchi huyo alifunga safari kumzika Rais Magufuli mwaka 2021.

MPAKA AMEAMUA KUMWAMBIA YEYE RAIS NI WAZI MBUNGE HAKUMSAIDIA
 
Ni kweli Rais hawezi kusikiliza kero za mwananchi mmoja mmoja, itakuwa jau sana .... mwingine kapigwa na mumewe anataka kesi apeleke kwa Rais, tutamaliza saa ngapi?
Mnatetea kila kitu cha Rais hata kama haiko sawa
 
Back
Top Bottom