Rais Samia, akili za kuambiwa changanya na za kwako

Rais Samia, akili za kuambiwa changanya na za kwako

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kumbuka madaraka uliyo nayo sasa kwa mujibu wa katiba kuna watu hawakupendezwa uwe nayo.

Kama ujuavyo, watu hao wala si wa upinzani bali wa kijani wenzako.

Walisema waswahili kikulacho ki nguoni mwako.

Au unadhani walishakuridhia sasa na kila kitu wewe na wao ni shwari?

Hadi sasa kuna mengi umefanya. Hata hivyo tambua wanaokupongeza na kukukosoa kwa dhati ni watu kutokea upinzani peke yao. Kuwa macho na wanao kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa.

"Akili za kuambiwa Changanya na za kwako." -- JK.

Tulipo sasa tunaelekea kwenye kimbembe cha katiba mpya. Wapinzani wanakwambia ukweli kuhusu hili. Heri kwako ungewasikiliza.

Kujaribu kuzuia au kuuchelewesha ujio wa katiba mpya kutakugharimu wewe binafsi kisiasa, kinyume na wanavyo kushauri. Bado kuizuia haitakuwa rahisi.

Mivutano na ujanja ujanja vya nini? Kama watu wanataka katiba mpya si uwasikilize?

Utawalazimisha kinyume na matakwa yao kwa gharama ipi?
 
Naomba niambie tatizo la katiba iliyopo?

Yameongelewa sana hayo. Ila kwa faida yako na wengine wenye siku chache hapa duniani, ninakuletea hapa baadhi.

Bila shaka hujui kuwa:

IMG_20220324_225211_042.jpg
 
Yameongelewa sana hayo. Ila kwa faida yako na wengine wenye siku chache hapa duniani, ninakuletea hapa baadhi.

Bila shaka hujui kuwa:

View attachment 2163399
Mambo haya 8 ndio yanahitaji katiba mpya? Maana hapa ndio wametaja(huko ulipoitoa hiyo screenshot) mambo Muhimu kuliko mambo yote..

Kingine uache Copy and Paste, badala yake toa mawazo yako kulingana na uelewa wako..
 
Kumbuka madaraka uliyo nayo sasa kwa mujibu wa katiba kuna watu hawakupendezwa uwe nayo.

Kama ujuavyo, watu hao wala si wa upinzani bali wa kijani wenzako.

Walisema waswahili kikulacho ki ngumu mwako.

Au unadhani walishakuridhia sasa na kila kitu wewe na wao ni shwari?

Hadi sasa kuna mengi umefanya. Hata hivyo tambua wanaokupongeza na kukukosoa kwa dhati ni watu kutokea upinzani peke yao. Kuwa macho na wanao kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa.

"Akili za kuambiwa Changanya na za kwako." -- JK.

Tulipo sasa tunaelekea kwenye kimbembe cha katiba mpya. Wapinzani wanakwambia ukweli kuhusu hili. Heri kwako ungewasikiliza.

Kujaribu kuzuia au kuuchelewesha ujio wa katiba mpya kutakugharimu wewe binafsi kisiasa, kinyume na wanavyo kushauri. Bado kuizuia haitakuwa rahisi.

Mivutano na ujanja vya nini? Kama watu wanataka katiba mpya si uwasikilize?

Utawalazimisha kinyume na matakwa yao kwa gharama ipi?
Hapo ataenda Msoga kuomba ushauri.
 
Back
Top Bottom