Rais Samia akizindua mradi wa maji Kigamboni na kugawa mitambo ya Kuchimbia visima, Leo Novemba 11, 2022

Rais Samia akizindua mradi wa maji Kigamboni na kugawa mitambo ya Kuchimbia visima, Leo Novemba 11, 2022

TOKA MAKTABA :

Ujenzi wa Bwawa la Maji Kidunda kata ya Serembala, Morogoro Kusini

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:-
Ujenzi wa Bwawa la Maji Kidunda lililopo katika kata ya Serembala, Morogoro Kusini umesababisha matatizo makubwa kwa wananchi wa kata ya Serembala, Magogoni na vijiji jirani kutokana na fidia kidogo kwa kupisha ujenzi wa mradi huo ikilinganishwa na mali walizoziachia yaani mashamba, nyumba zao na mali nyingine zilizo kwenye maeneo makubwa ya ardhi iliyochukuliwa kwa ajili ya mradi huo.

(a) Je, Serikali iko tayari kurudia zoezi la tathmini ya mali za wanavijiji wote walioathirika kwa kutoa nyumba na mashamba yao ili kupisha mradi wa bwawa la Kidunda na kuwalipa fidia wanayostahili?

(b) Je, Serikali iko tayari kwenye bajeti hii kumalizia malipo ya takribani shilingi bilioni 3.7 kuwafidia wananchi hao kulingana na tathmini iliyofanyika?

(c) Je, Serikali itakuwa tayari kuwawekea miundombinu ya uanzishwaji wa mashamba ya umwagiliaji na viwanda vidogo vidogo kwenye kata ya Serembala kwa ajili ya kutoa ajira kwa wananchi Serembala Magogoni, Mvuna na Kkata za jirani?

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Prosper Joseph Mbena, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-


Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaandaa malipo ya fidia kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi ya mwaka 1999 ambayo inaelekeza pia kuwa endapo malipo ya fidia yatachelewa kulipwa kwa zaidi ya miezi sita tangu kupitishwa, mlipaji anapaswa kufanya mapitio na kulipa nyongeza kutokana na muda uliozidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshalipa jumla ya shilingi bilioni 7.4 kwa familia 2,603 kama fidia ya kupisha ujenzi wa Bwawa la Kidunda.

Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kwa mwaka wa fedha 2016/2017 na imetenga kiasi cha shilingi bilioni mbili kwa mwaka wa fedha 2017/2018, kwa ajili ya fidia kulingana na tathmini iliyofanyika. Malipo yamekuwa yanafanyika kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, Bwawa la Kidunda linajengwa mahsusi kwa ajili ya kuhifadhi maji ya matumizi ya majumbani kwa wakazi wa Kibaha, Bagamoyo na Dar es Salaam. Bwawa hilo halitahusu kilimo kikubwa cha umwagiliaji. Serikali itaangalia uwezekano mwingine wa kuweka miundombinu wezeshi ya kilimo cha umwagiliaji kulingana na maeneo husika.(Makofi)
Source : Bunge Polis
 
Kwa bajeti ipi? Hiyo mitambo imeagizwa kutokana na fedha za uviko. Hakuna bilioni 700 alizotenga jiwe kwa kazi hiyo acheni kumpa sifa asizostahili.
Tunaofuatilia "hansard", tunajua hili lilizungumzwa bungeni. Ndio twauliza vi wapi hivyo vifaa vilivyopangiwa bajeti na kupitishwa bungeni 2020 - 2021!!???
 
Tunaofuatilia "hansard", tunajua hili lilizungumzwa bungeni. Ndio twauliza vi wapi hivyo vifaa vilivyopangiwa bajeti na kupitishwa bungeni 2020 - 202
Nafikiri viongozi na wataalamu wa wizara husika wangejikita kwenye kutatua chanagamoto na pia kuwa pro active
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akizindua mradi wa maji Kigamboni na kugawa mitambo ya Kuchimbia visima, Leo Novemba 11, 2022



=====

Mradi wa maji wa Kigamboni umezinduliwa rasmi na Rais Samia, Rais amejafungua maji na yanatoka kwa wingi.

Rais amekata utepe na kukabidhi magari ya kuchimbia visima na mabwawa na kukabidhi funguo. Magari hayo yatatumika kuchimbia visima vijijini na mijini, pia ameagiza magari hayo yakatunzwe.

Hotuba ya Rais Samia Suluhu

Awali ya yote nijielekeze Kumshukuru Mungu kwa kutukunanisha hapa leo, kama mnavyoelewa wiki iliyopita ajali ya ndege ilitokea hivyo naomba tusimame kwa dk moja tuwaombee ndugu zetu.

Nitumie nafasi hii kutoa shukrani zangu kwa Waziri wa maji kwa kunialika kwenye shughuli hii, ya kukabidhi magari kuchimbia visima vya maji, kukabidhi ardhi kwa mkandarasi wa ujenzi wa bwawa la Kidunda na Kufungua mradi wa Maji Kigamboni.

Nawaachia kazi DAWASA kuhakikisha Kigamboni inapata maji kwa asilimia 100 kwani imekuwa ikitoa maji Dar ila yenyewe haipati maji, Dar ilitikiswa na ukosefu wa maji kutokana na mabadiliko ya tania ya nchi, na hii ni kutokana na watu kuchepusha maji, kupeleka mifugo na shughuli nyingine za kiuchumi.

Waziri wa mifugo naomba mkae muangalie njia ya kufanya mifugo isizagae ovyo, na hii ni nchi nzima, Picha niyooneshwa hapa ni ng'ombe karibu 5000 na ng'ombe 1 anakunyw alita karibu 45 kwa siku kwa ng'ombe 5000 ni lita ngapi watakunywa na waachie maji ya kuchujwa kuleta kwa wananchi, lakini endeleeni kutoa elimu na hic=zo picha pelekeni TBC zionekane kwa jamii ili waone uharibifu unaofanywa.

Katika miaka miwili hii wanangu wa idara ya maji umeifanya kazi nzuri sana, niwaombe ongezeni juhudi kwani kumpatia mwanandamu maji ni sadaka, ongezeni juhudi na wanasema mcheza kwao hutunzwa hivyo huko mbele tutakuja kuwatupia jicho la rehema, na serikali itaendelea kutoa fedha.

Kila mmoja ahakikishe kulinda miundombinu na vifaa vyite vilivyotolewa kwani vinanunuliwa kwa gharam kubwa, na visipotunzwa vitaharibika haraka. Tambue mitambo hii imegharibu bilioni 35 fedha ambazo zingeweza kufanya mambo mengine hivyo mtunze.

Mitambo hii ikatumike kama ilivyokusudiwa kwani inauwezo wa kutambua eneo lenye maji na si kuchimba kisima halafu maji hakuna, mkimbicha kisima maji hakuna sitawavumilia waliohusika nataka wawajibishane wao kwa wao kabla ya kufika kwangu.

Pamoja na kugawa mitambo lakini leo tumezindua mradi wamaji ni matumaini yangu shida ya maji itakwenda kupungua Dar, tunatambua mradi huu ni wa kupunguza makali tu lakini suluhisho la kudumu ni ujenzi wa bwawa la Kidunda na mkataba umesainiwa na linakwenda kuanza kujengwa. Likimaliza kujengwa na kujaa tuna uhakika hakutakuwa na shida ya Maji Dar, nitoe rai kwa makandarasi kukamilisha kazi hii kwa viwango vilivyokusudiwa na kwa wakati.

Pamoja na juhudi za serikali kuhahakisha wanapata huduma ya kuvuka Kigamboni kama tulivyoanza kuwashirikisha sekata binafsi tutaendelea kuwashirikisha sekta binafsi, pamoja na kuagiza kivuko kipya kijengwe kikijengwa tutawakabidhi sekta binafsi wakiendeshe halafu tunaelewana huko kwenye mikataba.

Jambo lingine ni daraja la Kigamboni, kuna tozo na watu wanaomba ziondoke, haziwezo kuondoka kwa kuwa ni mkopo na watu inabidi wazoee kuna miradi migni ya aina hii itakuja ili tuendele. Watu wanatolea mfano daraja la Tanzanite, lile ni fedha ya serikali kwa asilimia 100 ila hii ya kulipia ni uzoefu wa mwanzo ile bure inabidi iondoke tuwe na miradi mikubwa madaraja makubwa ila yakiwa ya mikopo wa kulipa mikopo hiyo ni sisi waanchi na inabidi tuzoee kulipa. Hatutaweza kuondoa tozo labda tuone namna ya kuipunguza.

Mradi ulioshindikana toka enzi za Nyerere umewezekana chini ya SSH..

Bado mna maswali? Kwa wanawake.huyu ndio Rais atakayewapunguzia madhila ila wanaume zaidi ya kujitapa Hakuna kitu.
 
Hivi hivi vitu huwa haviwezi kufanya kazi hadi vizinduliwe na kiongozi kama Rais, Makamu wake au Waziri Mkuu?
Watajuaje kwamba walivyovila vimeshabalikiwa?

Walamba asali wajanja sana.
 
Wamesema pesa alizokopa Mh Samia kutoka IMF.
Hakuna kitu kinachonikera kama kumfanya hayati JPM kuwa ni mtakatifu halafu Samia ni shetani, naiona kama ni tabia ya kinafiki na ya watu waliozibiwa mianya yao ya kula kwani Samia kaingia na watu anaowapenda yeye.
 
Tangu lini ngombe wanasababisha ukame kwa kunywa maji??
 
Mradi unazinduliwa Kigamboni wakati wa kigamboni hawajawahi kutumia maji ya NUA, sijui DAWASCO sijui Duwasa, DAWASA--- tangu karne za Kitwana Kondo hadi muda huu navyoandika - aliyeliona bomba la maji kwenye nyumba ya mkazi wa kigamboni na aseme sasa... 98% wakazi wa huko wanajigemea kwa maji ya binafsi.

Siasa bana !!
 
Mradi unazinduliwa Kigamboni wakati wa kigamboni hawajawahi kutumia maji ya NUA, sijui DAWASCO sijui Duwasa, DAWASA--- tangu karne za Kitwana Kondo hadi muda huu navyoandika - aliyeliona bomba la maji kwenye nyumba ya mkazi wa kigamboni na aseme sasa... 98% wakazi wa huko wanajigemea kwa maji ya binafsi.

Siasa bana !!
cc: Mzee Sabodo
 

11 November 2022​

RAIS SAMIA AKIZINDUA MRADI WA MAJI KIGAMBONI NA KUGAWA MITAMBO YA KUCHIMBA VISAMA


Source : majiDigital Tanzania
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akizindua mradi wa maji Kigamboni na kugawa mitambo ya Kuchimbia visima, Leo Novemba 11, 2022



=====

Mradi wa maji wa Kigamboni umezinduliwa rasmi na Rais Samia, Rais amejafungua maji na yanatoka kwa wingi.

Rais amekata utepe na kukabidhi magari ya kuchimbia visima na mabwawa na kukabidhi funguo. Magari hayo yatatumika kuchimbia visima vijijini na mijini, pia ameagiza magari hayo yakatunzwe.

Hotuba ya Rais Samia Suluhu

Awali ya yote nijielekeze Kumshukuru Mungu kwa kutukunanisha hapa leo, kama mnavyoelewa wiki iliyopita ajali ya ndege ilitokea hivyo naomba tusimame kwa dk moja tuwaombee ndugu zetu.

Nitumie nafasi hii kutoa shukrani zangu kwa Waziri wa maji kwa kunialika kwenye shughuli hii, ya kukabidhi magari kuchimbia visima vya maji, kukabidhi ardhi kwa mkandarasi wa ujenzi wa bwawa la Kidunda na Kufungua mradi wa Maji Kigamboni.

Nawaachia kazi DAWASA kuhakikisha Kigamboni inapata maji kwa asilimia 100 kwani imekuwa ikitoa maji Dar ila yenyewe haipati maji, Dar ilitikiswa na ukosefu wa maji kutokana na mabadiliko ya tania ya nchi, na hii ni kutokana na watu kuchepusha maji, kupeleka mifugo na shughuli nyingine za kiuchumi.

Waziri wa mifugo naomba mkae muangalie njia ya kufanya mifugo isizagae ovyo, na hii ni nchi nzima, Picha niyooneshwa hapa ni ng'ombe karibu 5000 na ng'ombe 1 anakunyw alita karibu 45 kwa siku kwa ng'ombe 5000 ni lita ngapi watakunywa na waachie maji ya kuchujwa kuleta kwa wananchi, lakini endeleeni kutoa elimu na hic=zo picha pelekeni TBC zionekane kwa jamii ili waone uharibifu unaofanywa.

Katika miaka miwili hii wanangu wa idara ya maji umeifanya kazi nzuri sana, niwaombe ongezeni juhudi kwani kumpatia mwanandamu maji ni sadaka, ongezeni juhudi na wanasema mcheza kwao hutunzwa hivyo huko mbele tutakuja kuwatupia jicho la rehema, na serikali itaendelea kutoa fedha.

Kila mmoja ahakikishe kulinda miundombinu na vifaa vyite vilivyotolewa kwani vinanunuliwa kwa gharam kubwa, na visipotunzwa vitaharibika haraka. Tambue mitambo hii imegharibu bilioni 35 fedha ambazo zingeweza kufanya mambo mengine hivyo mtunze.

Mitambo hii ikatumike kama ilivyokusudiwa kwani inauwezo wa kutambua eneo lenye maji na si kuchimba kisima halafu maji hakuna, mkimbicha kisima maji hakuna sitawavumilia waliohusika nataka wawajibishane wao kwa wao kabla ya kufika kwangu.

Pamoja na kugawa mitambo lakini leo tumezindua mradi wamaji ni matumaini yangu shida ya maji itakwenda kupungua Dar, tunatambua mradi huu ni wa kupunguza makali tu lakini suluhisho la kudumu ni ujenzi wa bwawa la Kidunda na mkataba umesainiwa na linakwenda kuanza kujengwa. Likimaliza kujengwa na kujaa tuna uhakika hakutakuwa na shida ya Maji Dar, nitoe rai kwa makandarasi kukamilisha kazi hii kwa viwango vilivyokusudiwa na kwa wakati.

Pamoja na juhudi za serikali kuhahakisha wanapata huduma ya kuvuka Kigamboni kama tulivyoanza kuwashirikisha sekata binafsi tutaendelea kuwashirikisha sekta binafsi, pamoja na kuagiza kivuko kipya kijengwe kikijengwa tutawakabidhi sekta binafsi wakiendeshe halafu tunaelewana huko kwenye mikataba.

Jambo lingine ni daraja la Kigamboni, kuna tozo na watu wanaomba ziondoke, haziwezo kuondoka kwa kuwa ni mkopo na watu inabidi wazoee kuna miradi migni ya aina hii itakuja ili tuendele. Watu wanatolea mfano daraja la Tanzanite, lile ni fedha ya serikali kwa asilimia 100 ila hii ya kulipia ni uzoefu wa mwanzo ile bure inabidi iondoke tuwe na miradi mikubwa madaraja makubwa ila yakiwa ya mikopo wa kulipa mikopo hiyo ni sisi waanchi na inabidi tuzoee kulipa. Hatutaweza kuondoa tozo labda tuone namna ya kuipunguza.

Hii iingie kwenye rekodi haijawahi fanywa na Rais yeyote hapo kabla..

Hizi Ni Pesa za uviko 19,tunasubiria ambulances na magari ya kusambaza chanjo..
 
Back
Top Bottom