Rais Samia akubali ongezeko la asilimia 23.3 kwa kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa umma

Rais Samia akubali ongezeko la asilimia 23.3 kwa kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa umma

Set up ya mshahara inaanzia chin kwa maana hiyo mshahara huu utaongezeka kati ya 60000_ 80000 kwa watumishi
Kwanini barua isijifafanue yenyewe ?
Hadi tukutegemee wewe uweke mambo sawa [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Njaa mbaya sana
 
Kwa Mujibu wa Sheria za Tanzania , nyongeza ya mshahara wa wafanyakazi kila mwaka ni takwa la kisheria , limo ndani ya Katiba ya Nchi ambayo kila kiongozi mwenye akili timamu anapaswa kuifuata , hii ni kwa sababu aliapa kuilinda na kuitii .

Kwa Hiyo kwa Mama kuongeza mshahara kwa hizo 23.3 % si ajabu na wala si jambo la kushangaza , Kwa vile amefuata matakwa ya Katiba ya nchi kama inavyomuelekeza , nyongeza ya mshahara si mapendo ya Rais , amelazimishwa ndani ya Katiba , hakuna haja ya kumsifia as if Mshahara huo ameongeza kutoka nyumbani kwake , sana sana apongezwe kwa kuanza kuijua vizuri Katiba ya nchi .

Ikumbukwe kwamba sipingi nyongeza ya mshahara kwa Wafanyakazi wa Tanzania makapuku , waliosomeshwa namba kwa miaka 7 , isipokuwa nanyoosha tu maelezo kwamba KUPANDA KWA MSHAHARA SI HISANI YA RAIS , BALI NI MATAKWA YA KATIBA YA NCHI .

Naomba kuwasilisha .


Kwa maelezo haya tunakubaliana kuwa katiba iliyopo ni nzuri ila tu usimamiaji ndio mbaya,au vipi mkuu?
 
Tatizo kuna watu humu hata maana ya asilimia 23% hamjui ni vichwa panzi mnashangilia tu kama mazuzu! Serikali imepandisha kwa wale wanaopata kima cha chini kwa asilimia 23% Ila kwa wengine haijaweka wazi! Hesabu ni mhimu sana maishani!
Rudi shule

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Hapo kuna sentensi mbili zinazo jitegemea.

1. Raisi amekubali nyongeza ya mishahara.

2. Raisi amekubali nyongeza ya mishahara ya kima cha chini kwa asilimia 23.3.

Sasa hapo hao ambao sio wa kima cha chini wataongezwa kwa kiasi gani ?

Lakini msijali nchi ina fulsa nyingi za kujiongezea kipato.
..siyo "kwa kima cha chini", ni "ikiwemo kima cha chini" ...someni vzur, msipotoshe ...
 
Rais wa TUCTA ulimsikia jana TBC1?
Hakuna flat rate 23.3% wengine watapata 5% hadi 1%
Ongezeko ni kwa Flat rate, huo upungufu unaousema ni adjustments za kodi kutokana na ongezeko la mshahara huo.
Ila nyongeza hucheza kwa pamoja kote.
 
Ulitaka isiwepo hata hiyo 23.3%?
ulitaka wasishangilie?


Wanashangilia naona hawana miradi ya ujenzi,hiyo asilimia iliyoongezwa ebu waende wakaulize bei ya nondo rola Moja waone,bati,sementi na vifaa vingine vya ujezi,hiyo asilimia itawasaidia kuilipia chumba Cha kupanga Kwa mwezi elfu 50 tu,sijajua watu wanashangilia Nini wakati vitu vimepanda bei sana,hiyo 23.3% kama huna shuguli zingine utabaki ukipiga marchtime hapohapo bila kusogea popote
 
80%?? jaribu halafu utaona inflation yake hutaamini utasema maisha yalikuwa rahisi zamani kuliko sasa. Ukiongeza pesa nyingi kwenye mzunguko usio uwiana na uzalishaji basi inflation kubwa itatokea.
Kupanda Kwa bei ya bidhaa sio inflation?
 
Roho ya korosho!
Ninacho kuambia hakuna kitu huyu mpuuzi anaweza kufanya kisiwe na madhara makubwa zaidi hapa tz ,bado watz hawataki kukubali ukweli kuwa rais tuliye naye ni zuzu wa mazuzu ila ukweli mtaujua. Ninachokuambia ni mchakato qa kuchapa pesa ili kuongeza mishahara na kukopa
 
Umesahu kusema wengine itaongezeka kwa asilimia 0000.1 si hakuna formula?
Unabishana na Rais wa TUCTA aliyeshiriki kwenye vikao na mjadala wa kuongeza mshahara. Amesema kadri mshahara unavyoongezeka na asilimia inapungua. Akatoa mfano mtu mwenye mshahara wa milioni 3 hawezi kupata 23.3%.
 
Lakini Kuna issue moja: Hadi Sasa kima Cha chini kilikuwa hakitozwi Kodi, je baada ya ongezeko hili kitaendelea kutozwa Kodi? Kama kikitozwa Kodi bado take home itasinyaa!
Kuna salary ambazo zikifall chini ya tax band flani hazitozwi kodi, increment ikifanyika tu zikavuka hiyo band zinalimwa kodi na hasa hilo ndio lengo kubwa la govt.

Tukumbuke tu kiasi taslimu kichoongezeka ni Tril 1.5 tu ktk bajet ya mwaka huu na ndicho kitaenda kubeffect hayo maongezeko yooooote mwaka mzima.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Unabishana na Rais wa TUCTA aliyeshiriki kwenye vikao na mjadala wa kuongeza mshahara. Amesema kadri mshahara unavyoongezeka na asilimia inapungua. Akatoa mfano mtu mwenye mshahara wa milioni 3 hawezi kupata 23.3%.
Mi nilitaka tu nijue ndugu yangu mwenye mshahara wa Tsh 500,000/= atapata nyongeza ya kiasi gani.

Halafu mambo ya nyongeza zao zinapaswa zijulikane kikanuni na sio kuishia kama ulivyosema.

Mtu anataka ajue nyongeza yake itakuwa kiasi gani. Kama ilivyo fafanuliwa Kenya na Zanzibar.

Mambo ya itaongezeka kadri kadri ni ujanja ujanja tu.
 
Mnaumia sana Sukuma gang.
Bahati nzuri niliajiriwa 2015 July kwahiyo hunielezi chochote kipya kilicholeta unafuu wa mtumishi kutoka kwa Ibilisi wenu marehemu.
Mama kuingia tu miezi 3 madaraja hayo tukavuta pesa benki.
Na sasa tunasubiri kidogo tu tuvute tena pesa.
Asiye na nyumba atajenga, asiye na gari atanunua sasa.
Na ambao tumeshaoata hivyo vyote tutafungua business Kariakoo
Sukuma gang ana miaka 20 kazini Ila wewe mwenye miaka mitano huelezwi chochote,wacha nicheke kwanza,
 
Sioni sababu ya kitaalamu ya kuonheza mishahara kwa wafanyakazi wa umma.

Serikali unatakiwa kujikita kupandisha thamani ya shilingi ya Tanzania ili pesa inayo patikana kwa wananchi kwa ujumla wao iweze kukidhi mahitaji yao ya kila siku.

Kuoambana na mufumko wa bei ya bidhaa na huduma mbalimbali.

Upo ushahidi kila mshahara unapo panda bidhaa hupanda bei .

Hivyo inawaumiza wale wasio na mshahara wa mwezi Bali ni wahangaikaji wa vibarua visivyo rasimi.
Acha ufala na utaalamu wako
 
Back
Top Bottom