Rais Samia akutana na Mwalimu Wake aliyemfundisha Chuo kikuu cha Mzumbe Mwaka 1983-1986

Rais Samia akutana na Mwalimu Wake aliyemfundisha Chuo kikuu cha Mzumbe Mwaka 1983-1986

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Snapinsta.app_453907779_18246812248258462_8982240898289947426_n_1080.jpg

Ndugu zangu Watanzania,

Katika muendelezo wa ziara yake Mkoani Morogoro ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo,uzinduzi na uwekaji wa mawe ya msingi kwa ujenzi wa miradi mbalimbali,utatuzi wa kero mbalimbali za wananchi.

Mheshimiwa Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan,katika hali ya kuteka hisia za watu ameweza kuonana ana kwa ana Na Mwalimu wake Mama Sabina Gellejah ,aliyemfundisha alipokuwa mwanafunzi katika chuo hicho Mwaka 1983-1986 ambacho kwa sasa kinafahamika kama Mzumbe.

Kwa hakika Mungu ni Mwema sana .ukiangalia katika picha hii namna mama huyu alivyokuwa anaonesha uso wake uliojaa furaha na tabasamu mpaka unaona anatamani kutoa machozi ya furaha inagusa sana kiukweli.

Maana bila shaka Mama huyu haamini kama Ameweza kukutana uso kwa uso na Rais na Mkuu wa Nchi aliyepita mikononi mwake kama mwalimu wake. Haamini kama leo anaweza kupata nafasi ya kusalimiana na Mkuu wa nchi na Amiri Jeshi Mkuu.Haamini kama ni yeye aliyeingia katika kitabu cha historia cha kufundisha Mwanafunzi ambaye amekuja kuwa Mkuu wa Nchi na Amiri Jeshi Mkuu.

Bila shaka moyo wake umebubujikwa na machozi ya furaha sana kuona amepata bahati ambayo wengi hawapati katika Maisha yao yote mpaka wanakufa ,kuweza kupewa heshima ya hadhi ya juu kabisa kusimama na Rais Na kushikwa mkono kusalimiwa na kutambulishwa.

Leo Tanzania nzima imetambua na kumfahamu miongoni mwa watu waliompika na kumuivisha Mama yetu. Kwa hakika Mungu amjalie Maisha Marefu sana Mama na Mwalimu huyu aliyetupikia na kumfundisha Rais wetu Mh Dkt Mama Samia ,ambaye leo kama Taifa Tunajivunia uwepo wake madarakani.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Komredi Mwashambwa mbona huyo msaidizi wa rais mwenye nguo za kijeshi anatabasamu? Imekaaje hii kwa mujibu wa kazi yake?
Katika uongozi wa Rais Samia hakuna ambaye hatabasamu. Rais Samia amekuwa akiteka hisia za watu wengi sana mpaka inakuwa ni vigumu sana kwa mtu mwenye moyo wa nyama kubakia amenuna tu kama kiapo au maadili ya kazi yanavyomtaka. Kumbuka hata yeye ni Mwanadamu anayeguswa. Hata ungekuwa ni wewe kwa tukio hilo la kugusa hisia za watu ni lazima ungetabasamu tu.

Rais Samia kwa namna anavyopendwa na kugusa hisia za watu,ndio maana unaona hata akienda hospitalini unoana wagonjwa wakitabasamu na kuona wamepona kabisa.
Screenshot_20240802-154542_1.jpg
 
Waalimu wangu wa chuo sitaki hata kuwaona wajinga wale.

Walikua wanagawa maksi kwa machawa wao na wanafunzi wa kike waliokuwa wanatembea nao.
Sema wewe hukuwa na akili na hivyo kuwaonea wivu waliokuwa wanafaulu na kupata makisi za juu. hata hapa kila mmoja anafahamu kuwa wewe huwa hupo vizuri kichwani.
 

Ndugu zangu Watanzania,

Katika muendelezo wa ziara yake Mkoani Morogoro ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo,uzinduzi na uweiongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
  • Kuhusu Kupa Heshima kwa Mwalimu:
    • Mtume Muhammad (S.A.W) alisema: "Yeyote anayeongozwa na kuwaongoza wengine kwa mema, anapata thawabu, na anayejifunza kutoka kwake anapata faida." (Hadithi hii inaonyesha kuwa mwalimu anayefundisha mema na kufundisha wengine anastahili kuthaminiwa.)
  • Kuhusu Heshima na Utambuzi:
    • Mtume Muhammad (S.A.W) alisema: "Mtu ambaye haishughuliki na elimu anapaswa kuwa na heshima kwa wale wanaoifanya kazi ya kutoa elimu." (Hadithi hii inaonyesha umuhimu wa kumheshimu mwalimu kwa kazi yake ya kutoa elimu.)
 
Back
Top Bottom