Rais Samia amesema anarejesha mahusiano na nchi za Ulaya. Je, kukopa ndio njia bora ya kufanya hivyo?

Laana ambayo na yeye ameshiriki kuitenda.
 
Tangu Nyerere mpaka Samia hakuna rais ambaye hajapokea misaada wala hajachukua mikopo, huo ndio ukweli wenyewe.

JPM alitaka tujitegemee lakini gharama ya miradi aliyoianzisha isingeweza kumalizwa kwa kutegemea makusanyo ya kodi, ambayo na yenyewe zipo habari kuwa namba zake zilikuwa zinapikwa na kina Kidatta.

Tuache hizi mbwembwe za kusema kuomba ni laana wakati hatuna rais hata mmoja ambaye hajawahi kupokea pesa iliyo matunda ya ukusanyaji wa kodi wa nchi za Ulaya.
 
Inahitaji kujitoa ufahamu kutetea mikopo.

Ukizingatia kwamba punde tu umetoka kutetea kutokukopa.
 
Ndio nakwambia kwamba hii ni hali ambayo tangu uhuru tunayo. Labda tumeshindwa kama taifa kujitegemea.
Haimaanishi tunachokifanya sasa ni sawa.

Na wala sio kosa kuachana na utamaduni huo mbaya.

Na hatupaswi kutetea makosa haya ya ukopaji tena pale wenye mamlaka wanapoonesha wazi wazi kwamba kukopa ni jambo zuri tu kama unavyotaka wewe tuamini hivyo kwamba it is just ok kukopa.

Mkuu unakosea sana na nakuhurumia sana.

Kwanini tu usiwe mkweli na kuachana na unafiki maana husaidii Taifa lako ukifanya hivyo.

Acha unafiki mkuu. Jifunze kusema ukweli kwa faida ya nchi yako.
 
Walikuwa wanashangilia magu kutokopa bado wapo chamani wanapiga shangilio
Ndipo hapo nimemuuliza shemeji yangu mmoja ambaye ni mwenyekiti wa CCM mkoa fulani,kwamba mbona alishangilia JPM kutokopa na sasa anashangilia SSH kukopa, kakosa jibu.
 
Kujitgemea ni kitu kingine na kushindana kiuchumi ni kitu kingine.
Kujitegemea tunaweza ila kushindana kiuchumi bado sana.
Kwa nini tusisaidiwe kwa kupewa scholarships kwa ajili ya kupata wataalamu wa kuchimbwa mabwawa ya kuhifadhi maji,wataalamu wa umwagiliaji, wataalamu wa zana rahisi za kilimo,wataalamu wa afya,wataalamu wa taaluma zote muhimu ili kesho tuweze kujitegemea!!!
Kwa nini tunapewa samaki badala ya kufundishwa kuvua na tupewe ndoano/nyavu ili tuvue wenyewe!!!
 
Wewe ulikuwa miongoni mwa waliomsupport Magufuli na falsafa zake hivyo huna moral authority kumkosoa sasa.
Wewe pia ni mmojawapo wa supporters mzuri wa CCM, chama kisicho na sera, mipango kwa ajili ya Tanzania ya miaka 100 ijayo zaidi ya kuwaza uchaguzi ujao tu.
 
Kukopa ni aibu yetu sote kama watanzania. Na hatujapata suluhisho la kudumu.

Kumshambulia SSH kwa kukopa ni kutomtendea haki tukizingatia ukweli kuwa sio wa kwanza kukopa. Na anakopa kufanya kazi zinazoonekana.

Kusema kukopa ni laana wakati huna wazo mbadala litakaloingiza pesa hazina ya nchi , ni kujidanganya. Ni fikra zile zile za JPM za sisi ni matajiri wakati huo utajiri bado upo ardhini na anamtegemea Dotto James aongee na wazungu ili tupate mikopo.

Hakuna dhambi yoyote ya kuchukua mikopo, ikiwa JPM mwenyewe alikuwa akijisifu kuwa mabosi wa benki ya dunia walikubali kutupa mkopo wa kujenga flyover ya Ubungo na akisema hivyo pembeni yake akiwa amekaa bosi wa benki ya dunia!.

SSH akikopa ni nongwa ya kuanzishia uzi kabisa lakini JPM akifanya hivyo ni suala zuri tu, unafiki ni wa kwako wewe.
 
W
Wewe uliona wapi Magufuri akienda ulaya kubembeleza mikopo?wazungu ndio walimfuata Magu kumbembeleza wamkopeshe, huyu Mama yenu ni empty kichwani, mikopo yote na msaada anavimalizia kwenye nauli, sijui mwezi kesho anaelekea nchi ipi kuomba.
 
Unajipendeza.
 
Wewe ulikuwa miongoni mwa waliomsupport Magufuli na falsafa zake hivyo huna moral authority kumkosoa sasa.
Kumuunga mkono JPM sio sawa na mimi kuwa mkristo mkatoliki kwamba siwezi kubadilisha dini yangu. Kukosolewa au kuungwa mkono huenda kukibadilika kutokana na maarifa anayoyapata mtu, kutokana na kuelewa mambo ambayo wakati huo sikuwa ninayajua.

Ukosoaji sio sawa na dini useme kwamba mtu hawezi kubadilika. Humu ndani tunaongelea hoja halisi hatuongelei watu, hayo ni masuala ya instagram na facebook ambapo kuna team Diamond na team Ali Kiba.
 
Watu kama hao wanaitwa Malaya wa kisiasa na wasaka tonge.
 
Reactions: nao
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…