mr gentleman
JF-Expert Member
- Aug 1, 2012
- 3,222
- 4,689
Sabaya ni hazina ya nchi hii. ni kijana mzalendo anaepigania maslahi ya taifa.Huyu jamaa kiufupi na bila kuficha ni moja kati ya mashetani wakubwa kuwahi kutokea nchi hii
Katesa watu sana, kaandaa magenge yake ya uporaji na unyanganyi na kufanya ubabe usio na maana Arusha na Moshi.
Walinzi wa mbowe walibambikiwa kesi za ugaidi na uhujumu uchumi, hadi leo wanaozea gerezani, kwa kifupi huyu mtu alitakiwa apelekwe mahakamani na ahukumiwe haraka sana
Habari ya kujificha kwenye uzalendo wa kutetea chama huku ukiumiza watu wasiokua na hatia nayo ni ushamba wa huyu dogo,
Kazi yako ni kutetea majambazi kama Sabaya na JPM?Huyu Madam SSH anafanya kazi au anafanya maamuzi kwa kusikiliza kelele na porojo za mitandaoni.
Ni hatari sana kuwa na Rais anayesikiliza umbea, udaku na mihemuko ya mitandaoni kisha anachukua maamuzi ili kuwaridhisha followers wake.
Kaaazi kweli kweli!!!
Sabaya ni hazina ya nchi hii. ni kijana mzalendo anaepigania maslahi ya taifa.
Chuki yake imetengenezwa na wafanya magendo wakichaga.
Unajipendekeza kwa Mbowe akupe ajira?Kama ameshamtoa dikteta Mbowe haina shida.
Watu wa Hai hawatarudi tena kanani
Mkuu Sabaya ni kijana Mdogo mbona. Kama ana mika mingi kwa sasa ni 34Sabaya Kuna Maisha fulani hivi ya kijana akiwa na miaka 20-30 inaonekana Kama hakupitia hivi au alipitia lakini hakufaidi. Siku moja hivi mwaka juzi , aligombea dem Pin Point Arusha mshamba sana huyu
Pole mtegemezi! Huwezi kuishi bila kuajiriwa. Ndio maana mnaloga ili mng'ang'anie na kufia kwenye ofisi za umma huku mkiwaambia watoto wa wenzenu wakajiajiri huku ilihali ninyi huko ccm mkishindwa kujiajiri!Yaani wewe mtoto ungekuwa karibu na mimi ningekuwa nishakuchapa viboko.inaonekana huna adabu kwa wakubwa zako.unajibu jibu tu.
Embu kalale huko.kesho ukatume maombi serikali yenye matunda ya jpm imetoa kazi.
Jpm alishasema kuhusu hizi ajira.kwahiyo sio jambo geni msije anza kunikera hapa. Tutakerana ooh!!
Kwendraaaaa tangu lini mimi nikawa mtumishi wa serikali?Pole mtegemezi! Huwezi kuishi bila kuajiriwa. Ndio maana mnaloga ili mng'ang'anie na kufia kwenye ofisi za umma huku mkiwaambia watoto wa wenzenu wakajiajiri huku ilihali ninyi huko ccm mkishindwa kujiajiri!
Sijapenda hii tabia yako ya kumsifia mtu aliyeharibu mifumo yote ya ajira nchi hii kwa tabia yake ya kuajiri kwa upendeleo Tena watu wa kabila lake tu!
Hivi mnapata wapi ujasiri wa kumtisha mwenyekiti wenu wa chama na mliye mchagua kwa 100% ya kura zote? Hili tangazo tangu jana mnalisambaza pasipo na hofu yoyote ile!Nipo kwenye magroup mengi ya WhatsApp na Facebook nimeona wanaccm wengi sana zaidi ya asilimia 80% walivyochukizwa na kitendo cha Ole Sabaya kusimamishwa na kukiita usalaliti kwa chama, Chadema siwezi kuwalaumu kwa furaha walionayo sasa maana Sabaya aliwaweza sana.
Kiukweli Sabaya licha ya U-DC alikuwa Hai kwa kazi maalumu ya kichama kuvunja ngome ya CHADEMA na hilo alilitimiza kwa kiasi kikubwa.
Wanaccm wamekuwa wachungu najua hapa JamiiForums kuna watu wako huko kwenye makundi wameona hali halisi na kule muhambwe kelele zimeanza kutolewa kuhusu mwenendo wako wa kuwaengua Pro John Pombe Magufuli na kuanza kusuka muungano na upinzani huku WanaCCM waliotembea kifua mbele wakianza kuwa ndio wapinzani
WanaCCM wanahoja za wewe kusema utaanza kuteua kutoka kokote sio mbaya maana hata John Pombe Magufuli aliteuwa lakini sio sera ya chama hapo unaonesha ubaguzi wa kuwataka WanaCCM waanze kujificha na kujiona sio priority tena.
Kijana Sabaya, Arusha alimbana sana Lema akafanikiwa akaenda Hai, Mbowe akaondolewa kuwaona viongozi wa BAVICHA na BAWACHA wakikesha wanakunywa kwa shangwe jua kuna sehemu umekosea na unazidi kukosea kila siku.
Kinachoitwa usaliti wa chama kwa kiongozi mkubwa kama wewe ni ishara mbaya sana.
Jitafakari
Umenena vema!Haina haja ya kumtete Sabaya kwa Rais kwa sasa
Mengi yameongelewa, mengi yameonekana sasa Wacha uchunguzi ukamilike apewe kilicho haki yake