Rais Samia amteua Zuhura Yunus kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu kupangiwa kazi nyingine

Rais Samia amteua Zuhura Yunus kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu kupangiwa kazi nyingine

Mama aJitahidi kubalance Dini, hii sio sawa manake JPM alilaumiwa kwa ukanda ila Dini it’s more sensitive matter! Huwezi ikawa kila teuzi anawaza dini na sio qualification na expertise kwenye eneo husika
 
Mama aJitahidi kubalance Dini, hii sio sawa manake JPM alilaumiwa kwa ukanda ila Dini it’s more sensitive matter! Huwezi ikawa kila teuzi anawaza dini na sio qualification na expertise kwenye eneo husika

Serikali haina dini
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu amemteua aliyekuwa mtangazaji wa BBC, Zuhura Yunus kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu akimrithi Jaffar Haniu. Mwezi uliopita Zuhura aliaga BBC na hakusema anapoelekea.

Haniu aliyerithi kijiti kutoka kwa Gerson Msigwa Juni mwaka jana atapangiwa kazi nyingine akihudumu kwenye ofisi hiyo kwa miezi saba.

Wanawake oyeee, mpaka maji yaitwe mma.. Tunasubiri matokeo kutoka Dodoma japo tunayajua


======

Zuhura Yunus ni mwanamke wa kwanza kutangaza kipindi cha Kiswahili cha televisheni BBC, Dira ya Dunia akihudumu kwenye shirika hilo kwa miaka 14. Zuhura alijiunga na BBC Swahili mwaka 2008 akiwa mtangazaji na mtayarishaji wa matangazo. Alijulikana kwa wasikilizaji wa BBC Swahili kuwa mtangazaji kinara wa matangazao ya redio, Dira ya Dunia, Zuhura ameripoti na kutangaza uchaguzi wa Tanzania mwaka 2010.

Kabla ya kujiunga na BBC, Zuhura alifanya kazi ya utangazaji katika vipindi mbalimbali vya redio ya Times FM na Uhuru FM nchini Tanzania. Mwaka 2002 Zuhura alishinda tuzo ya Habari ya Ishi nchini Tanzania kutokana na ripoti ya HIV/Aids. Pia amefanya kazi ya uandishi wa habari katika gazeti la The Citizen newspaper.

Mwaka jana Zuhura aliandika kitabu chake cha wasifu wa Biubwa Amour Zahor, mwanaharakati mwanamke wa kisiasa wakati wa mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964.

Zuhura katika utumishi wake amewahoji viongozi wa Afrika kama vile Rais wa zamani wa Tanzania, Jakaya Kikwete kama sehemu ya taarifa kuhusu biashara haramu ya wanyama pori pamoja na Rais wa Uganda Yoweri Museveni. Mahojiano aliyoyafanya na mgombea urais wa upinzani, Edward Lowassa mwaka 2015 yalizua gumzo katika vyombo vya habari nchini.

Zuhura ni muhitimu wa shahada ya kwanza katika Chuo Kikuu cha Mbale IUIU, Uganda na ana shahada ya Uzamili ya Mawasiliano ya Vyombo vya Habari kutoka Chuo Kikuu cha Leicester, Uingereza.

Safi sana mama,ni wakati wa kuweka professionals kwenye nafasi kama hizi,sio "sycophants,and ass kissers"kama akina Msigwa.
Huyu mama ilibidi apewe ukurugenzi wa TBC,Yule Profesa aliyejaza nadharia kichwani pale TBC,hajuhi kitu,hajawahi hata kutangaza achilia mbali kufsnya uandishi wa habari zaidi ya kufundisha tu,
Hongera Mhe Raisi,tuwekeze na IGP mwanamke,mwenye weredi.
 
Mwaka wa Waislamu huu, Ndugu yangu Jaffar Haniu kakosea wapi? Sitaki kuamini kakubali kirahisi hivyo kuacha yale mapochopocho mix kuku sambusa wa ikulu.

Mwezake Msigwa tangu afutwe kazi ikulu siku hizi kapauka kweli, Ikulu ikulu tu.

Mbona mauwaji yaliokithiri sasa ni majina yenu tu na sisi tumekaa kimya?
Mnakosea wapi?

Huwa hatuna unafiki anzisha uzi wa kujadili ukristo uone wangapi waislam wataponda au kuchangia
Ila sasa uzi uwe wetu utakuta viherehere kibao [emoji23][emoji23]
 
Kumbe wengi mnakiri kuwa uwiano wa kidini katika nafasi za kazi serikalini ni muhimu uzingatiwe, sasa kwanini huwa mnapopoa mawe mzee wangu Muhamed Said akija natakwimu zake za uwiano wa 80:20?


Kama mnaona kuna tatizo ipendekezwe basi 50/50 kabisa na iwe kwenye katiba tuone nani atakayelalamika na hapo ndiyo tutakapomjua mchawi ni nani kwenye hili.
 
Duh! Usipime!

Kazi imepata mtu stahiki.

Hongera Zuhura Yunus!

P
Nilijua kuwa wewe sio mzalendo wa kweli. Walichosema wengine humu JF kuwa wewe ni bendera inayo fuata upepo sasa nakubali.

Unajua maana ya mtu kuwa mtangazaji kwenye Institutions kama BBC? BBC ni shirika la Habari la uingereza na ambalo linaendeshwa kwa fedha za walipa kodi wa uingereza. Kwa hali hiyo hili shirika haliwezi toa habari mbaya kuhusu Uingereza. Mda wote litatoa habari kwa maslahi ya waingereza na yeyote atakaye fanya kazi kwenye shirika hili itambulike kuwa atakuwa amepikwa vizuri sana.

Ningewashauri kwanza mjiulize kabla ya kumpigia shangwe. What is BBC (British Broadcasting Corporation)?

Watanzania amkeni. Huyo mwanamke ni spy wa New Scotland Yards. Nasikitika kuona nchi inauzwa mchana kweupe na watanzania wanashangilia.

Mtu ambaye mambo yake mengi hayajulikani na zaidi ya hayo ni raia wa uingereza mnakubali kweli leo akae Ikulu watanzani?

Zuhura Yunus ni mwingereza na ana uraia wa uingereza. Ushahidi huu hapa chini.



Mama Samia na Rais Kikwete lao ni moja. Ni ma-puppet wa wazungu. Wana nia moja tu ya kuiangusha Tanzania.

Subirini mda sio mrefu mtasikia mengi kuhusu nchi yetu.

Mungu Ibariki Tanzania na watu wake!!!
 
Saa 100 amtengue mwislamu halafu aweke mkristo thubutuu

Yeye akitengeu mwislamu anarudishia mwislamu

Ila akitengua mkristo (wakristo) anajazia waislamu
Dikteta yeye alikuwa anafanyaje teuzi zake???!
 
Mwaka wa Waislamu huu, Ndugu yangu Jaffar Haniu kakosea wapi? Sitaki kuamini kakubali kirahisi hivyo kuacha yale mapochopocho mix kuku sambusa wa ikulu.

Mwezake Msigwa tangu afutwe kazi ikulu siku hizi kapauka kweli, Ikulu ikulu tu.
Jafar ni wakwetu Ila havai blazia huu ni mwendo wa blazia
 
mkuu wangu kabisa kutoka viunga vya Oysterbay opposite na St. Peters hebu tupe 'ubuyu' nini kimemsibu Bw. Haniu? Naskia kuna inshu kubwa pale jumba jeupe
Kwaiyo kwa akili yenu fupi mnahisi kafukuzwa au??! Anapelekwa kwenye nafasi nyingine kubwa kuliko hiyo
 
Safi sana mama,ni wakati wa kuweka professionals kwenye nafasi kama hizi,sio "sycophants,and ass kissers"kama akina Msigwa.
Huyu mama ilibidi apewe ukurugenzi wa TBC, Yule Profesa aliyejaza nadharia kichwani pale TBC, hajui kitu,hajawahi hata kutangaza achilia mbali kufsnya uandishi wa habari zaidi ya kufundisha tu,
Hongera Mhe Raisi,tuwekeze na IGP mwanamke,mwenye weredi.
Dah mkuu umesahu kuwa miaka ya nyuma alikuwa mtangazaji wa ITV ye na marehemu Misanya Bingi, kina Charles Hillary nk.
 
Back
Top Bottom