Sina CV ya Jaffar Haniu lakini kwa sisi wafuatiliaji wa kazi zake tuliona makosa makubwa kama matatu.Niwekee CV ya Jaffar hapa boss
Hebu acha kutukana watu usiowajua wewe kijana . Unaweza kuta unabishana na RSO humu, shauri zakoHalafu kuna jamaa anaitwa nyboma huyu jamaa ni zuzu sana....
Alikung'ata sikio, au unahisi tu akipewa huo uteuzi ataukataa? Kama Charles Hilary na uzee wake, amekubali! Pascal Mayalla ni nani mpaka akatae uteuzi kutoka kwa Rais wa nchi?Pascal Mayalla alishakataa hizo kazi
Pascal ni very senior kwa Msigwa na Jafari lakini alishajiondoa kwenye system anafanya yake
Mama D wewe ni mimi kabisa, sijawahi ona shida watu wa dini au kabila kujazwa kwenye teuzi .Labda kwa kuwa Mimi ni muislamu ninayeamini njia za kuishi vizuri ni nyingi mno duniani na teuzi hazikamilishi furaha ya mwanadamu.
Maelezo yote haya ya nini??!
Chawa wa Saa 100 wanajaribu kuficha upendeleo wake kwa wazanzibariUko sahihi ndiyo maana hata ADC wake ni wa kike!πMsemaj ni mtu wa karib sana wa rais...sasa jinsia mbili tofaut inakua ngum...
Kwahiyo Zuhura hana qualification and expertise?Mama aJitahidi kubalance Dini, hii sio sawa manake JPM alilaumiwa kwa ukanda ila Dini itβs more sensitive matter! Huwezi ikawa kila teuzi anawaza dini na sio qualification na expertise kwenye eneo husika
Umejua je kama pale wengi ni waislamu.Hujaelewa nilichomaanisha kwenye hiyo post hapo juu mkuu, kama Jaffar kafutwa kazi kwanini nafasi hiyo isijazwe na mkiristo.
Maana 95% ya watendaji pale ikulu wote ni waislamu kwanini isiwe 50% kwa 50%
whatever! that does not invalidate the Samia intention.....Pale mlangoni ikulu Kuna Aya ya quran..tangu nyerere
Ndo hapo nashangaa. Wafanyakazi wengi wa serikali 80% ni wakristu.Muwe na uvumilivu japo kidogo ndugu zetu,kwanini mnawafanya waislamu ni kama raia daraja la pili na hivyo hawastahili kupata nafasi yoyote ya juu katika utumishi wa umma au hata wa kisiasa katika nchi hii?
Hadi hivi sasa ni waislamu wachache sana ambao ni viongozi kwenye taasisi za umma na hata kwenye uongozi wa kisiasa lakini bado mkisikia jina mnalohisi ni la kiislamu likitajwa kwenye uteuzi mioyo yenu inawauma sana.
Jamani Pascal.Na hii umeikosa Bwana Pascal
Wonders shall never end
Siamini Kinachotokea hapa uwanjani, Pascal Mayalla anawekwa benchi tena
Sio Mzanzibar....ni M-bara wa Kaskazini
Mwaka gani huo? Zuhuru alifanya kazi Redio Uhuru miaka zaidi ya 12 iliyopita baadae akaenda The Citizen linalomilikiwa na Mwananchi ndipo baadae akaenda BBC.πππRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu amemteua aliyekuwa mtangazaji wa BBC, Zuhura Yunus kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu akimrithi Jaffar Haniu. Mwezi uliopita Zuhura aliaga BBC na hakusema anapoelekea. Kumbukumbu zinaonyesha Zuhuru atakuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhfa huu wa kuisemea taasisi kubwa zaidi nchini kimamlaka.
Haniu aliyerithi kijiti kutoka kwa Gerson Msigwa Juni mwaka jana atapangiwa kazi nyingine akihudumu kwenye ofisi hiyo kwa miezi saba pekee na pengine ndio anaweza kuwa mtu aliyehudumu muda mfupi zaidi katika nafasi hiyo.
Wanawake oyeee, mpaka maji yaitwe mma.. Tunasubiri matokeo kutoka Dodoma japo tunayajua
===
Zuhura Yunus ni mwanamke wa kwanza kutangaza kipindi cha Kiswahili cha televisheni BBC, Dira ya Dunia akihudumu kwenye shirika hilo kwa miaka 14. Zuhura alijiunga na BBC Swahili mwaka 2008 akiwa mtangazaji na mtayarishaji wa matangazo. Alijulikana kwa wasikilizaji wa BBC Swahili kuwa mtangazaji kinara wa matangazao ya redio, Dira ya Dunia, Zuhura ameripoti na kutangaza uchaguzi wa Tanzania mwaka 2010.
Kabla ya kujiunga na BBC, Zuhura alifanya kazi ya utangazaji katika vipindi mbalimbali vya redio ya Times FM na Uhuru FM nchini Tanzania. Mwaka 2002 Zuhura alishinda tuzo ya Habari ya Ishi nchini Tanzania kutokana na ripoti ya HIV/Aids. Pia amefanya kazi ya uandishi wa habari katika gazeti la The Citizen newspaper.
Mwaka jana Zuhura aliandika kitabu chake cha wasifu wa Biubwa Amour Zahor, mwanaharakati mwanamke wa kisiasa wakati wa mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964.
Zuhura katika utumishi wake amewahoji viongozi wa Afrika kama vile Rais wa zamani wa Tanzania, Jakaya Kikwete kama sehemu ya taarifa kuhusu biashara haramu ya wanyama pori pamoja na Rais wa Uganda Yoweri Museveni. Mahojiano aliyoyafanya na mgombea urais wa upinzani, Edward Lowassa mwaka 2015 yalizua gumzo katika vyombo vya habari nchini.
Zuhura ni muhitimu wa shahada ya kwanza katika Chuo Kikuu cha Mbale IUIU, Uganda na ana shahada ya Uzamili ya Mawasiliano ya Vyombo vya Habari kutoka Chuo Kikuu cha Leicester, Uingereza.