Rais Samia amteua Zuhura Yunus kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu kupangiwa kazi nyingine

Rais Samia amteua Zuhura Yunus kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu kupangiwa kazi nyingine

Wangempeleka TBC angedakwa na Azam chap chap!
Hongera Zuhura Yunus!
 
Mwaka wa Waislamu huu, Ndugu yangu Jaffar Haniu kakosea wapi? Sitaki kuamini kakubali kirahisi hivyo kuacha yale mapochopocho mix kuku sambusa wa ikulu.

Mwezake Msigwa tangu afutwe kazi ikulu siku hizi kapauka kweli, Ikulu ikulu tu.
mkuu wangu kabisa kutoka viunga vya Oysterbay opposite na St. Peters hebu tupe 'ubuyu' nini kimemsibu Bw. Haniu? Naskia kuna inshu kubwa pale jumba jeupe
 
Mwaka wa Waislamu huu, Ndugu yangu Jaffar Haniu kakosea wapi? Sitaki kuamini kakubali kirahisi hivyo kuacha yale mapochopocho mix kuku sambusa wa ikulu.

Mwezake Msigwa tangu afutwe kazi ikulu siku hizi kapauka kweli, Ikulu ikulu tu.
Ubaya wa mapochopocho ndio chanzo wa magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza ! Heart disease, diabetes and the likes !! Hatari mzee !! Siku hizi tunakula dona, mchicha, maharagwe, matunda and the likes !! Dunia inaenda mbio sana !!!
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu amemteua aliyekuwa mtangazaji wa BBC, Zuhura Yunus kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu akimrithi Jaffar Haniu. Mwezi uliopita Zuhura aliaga BBC na hakusema anapoelekea.

Haniu aliyerithi kijiti kutoka kwa Gerson Msigwa Juni mwaka jana atapangiwa kazi nyingine akihudumu kwenye ofisi hiyo kwa miezi saba.

Wanawake oyeee, mpaka maji yaitwe mma.. Tunasubiri matokeo kutoka Dodoma japo tunayajua


======

Zuhura Yunus ni mwanamke wa kwanza kutangaza kipindi cha Kiswahili cha televisheni BBC, Dira ya Dunia akihudumu kwenye shirika hilo kwa miaka 14. Zuhura alijiunga na BBC Swahili mwaka 2008 akiwa mtangazaji na mtayarishaji wa matangazo. Alijulikana kwa wasikilizaji wa BBC Swahili kuwa mtangazaji kinara wa matangazao ya redio, Dira ya Dunia, Zuhura ameripoti na kutangaza uchaguzi wa Tanzania mwaka 2010.

Kabla ya kujiunga na BBC, Zuhura alifanya kazi ya utangazaji katika vipindi mbalimbali vya redio ya Times FM na Uhuru FM nchini Tanzania. Mwaka 2002 Zuhura alishinda tuzo ya Habari ya Ishi nchini Tanzania kutokana na ripoti ya HIV/Aids. Pia amefanya kazi ya uandishi wa habari katika gazeti la The Citizen newspaper.

Mwaka jana Zuhura aliandika kitabu chake cha wasifu wa Biubwa Amour Zahor, mwanaharakati mwanamke wa kisiasa wakati wa mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964.

Zuhura katika utumishi wake amewahoji viongozi wa Afrika kama vile Rais wa zamani wa Tanzania, Jakaya Kikwete kama sehemu ya taarifa kuhusu biashara haramu ya wanyama pori pamoja na Rais wa Uganda Yoweri Museveni. Mahojiano aliyoyafanya na mgombea urais wa upinzani, Edward Lowassa mwaka 2015 yalizua gumzo katika vyombo vya habari nchini.

Zuhura ni muhitimu wa shahada ya kwanza katika Chuo Kikuu cha Mbale IUIU, Uganda na ana shahada ya Uzamili ya Mawasiliano ya Vyombo vya Habari kutoka Chuo Kikuu cha Leicester, Uingereza.

Tuache mambo ya Jinsia, U-dini na U-Zanzibar au U-Bara. Wote ni Watanzania. Tuunge mkono Rais anapojenga timu yenye uwezo na weledi wa kumsaidia ili aweze kutimiza wajibu wake. Zuhura Yunus ni msomi mzuri na amethibitisha kuwa ana uwezo wa utendaji katika ngazi ya kimataifa kuliko wengi wetu. Tatizo langu tu ni kama utamaduni wa kuleta masuala ambayo hayahusiani na utendaji unaonesha kama ndiyo kipimo chetu cha ustaarabu, hususan, maadili? Je,utameuhusu Zuhura afanye kazi hiyo katika kiwango kile kile cha kimataifa au itakuwa kama Messi acheze mpira na timu daraja la pili hapa Bongo!? Kuwatoa hofu mashabiki mimi ni Mkristo wa Bara! Vinginevyo Hongera na Kila la Kheri Zuhura Yunus!
 
Huyu binti kupewa u- DPC ikulu ni kati ya matusi makubwa sana anayoendelea kutukanwa Hayati Magufuli, huyu na Kikeke ndio walikuwa wakiisema na kuichafua sana awamu ya Magufuli
Umegeuza msimamo. Kwanza ulianza udini ukaona hai hold water umekuja na ramli chonganishi.
 
Tutafakari kidogo, chemsha bongo.
Hivi Haniu Jaffer kafanya kosa gani/kaboronga wapi?
 
Tuache mambo ya Jinsia, U-dini na U-Zanzibar au U-Bara. Wote ni Watanzania. Tuunge mkono Rais anapojenga timu yenye uwezo na weledi wa kumsaidia ili aweze kutimiza wajibu wake. Zuhura Yunus ni msomi mzuri na amethibitisha kuwa ana uwezo wa utendaji katika ngazi ya kimataifa kuliko wengi wetu. Tatizo langu tu ni kama utamaduni wa kuleta masuala ambayo hayahusiani na utendaji unaonesha kama ndiyo kipimo chetu cha ustaarab, hususan, maadili? Je,utameuhusu Zuhura afanye kazi hiyo katika kiwango kile kile cha kimataifa au itakuwa kama Messi acheze mpira na timu daraja la pili hapa Bongo!? Kuwatoa hofu mashabiki mimi ni Mkristo wa Bara! Vinginevyo Hongera na Kila la Kheri Zuhura Yunus!
Badala ya kumhukumu kwa weledi wake watu wanahangaika na ujinga..

Mbumbumbu hawataa waishe hapa Africa
 
Mama D wewe ni mimi kabisa, sijawahi ona shida watu wa dini au kabila kujazwa kwenye teuzi .Labda kwa kuwa Mimi ni muislamu ninayeamini njia za kuishi vizuri ni nyingi mno duniani na teuzi hazikamilishi furaha ya mwanadamu.
Mimi ni mkristo ila Bora Waislam wawe wengi Wana utu kuliko wagalatia,roho mbaya sana hawana adabu wala heshima japo ya dini.
 
Hapa ndugu unakosea sana...mbona hao waislam wakati wa Magufuli akifanya teuzi walikuwa hawasemi kuwa mwaka wa wakristo huu! Usitake niamini "the lights are on,but nobody is home!
Hilo zee bwabwa lisamehe bure
 
Sasa bado CDF mwanamke, bado IGP mwanamke na bado JAJI MKUU mwanamke ili itifaki izingatiwe 100%
shida ni kwamba, wakifanya sana hivyo, wanaweza wasije kupata tena uongozi miaka ya mbeleni.ni sawa na sasaivi ati mtu atoke kanda fulani hivi ya wale watu wanaoongea kama wanaporomosha miamba, agombee urais, watu watakuwa wametoneshwa vidonda watakuwa tayari kumpa kura hata nccr mageuzi kuliko yeye hata kama atatoka ccm. trust me.
 
Back
Top Bottom