Rais Samia anakubali kuwa Rais Magufuli aliambukizwa UVIKO-19?

Rais Samia anakubali kuwa Rais Magufuli aliambukizwa UVIKO-19?

Wewe ni mpumbavu unayetaka kila mtu awaze na afikirie kila unachoandika wewe ni sahihi

Umekosa maarifa na ufahamu wa mambo, Unachokifahamu wewe tambua Wengine walianza kukitambua kabla yako na kuweka kwenye maandishi

Rais ni mamlaka, Na kwa Tanzania lazima ufahamu umpende au Usipende Rais ndie Sheria, Kanuni na taratibu

Kwa mfumo wa Tanzania wa sasa hakuna mwenye nguvu ya kumsema na kumkosoa Rais hiyo ndio Tanzania

Sheria ya kumuweka mtu Kizuizini bado Rais anayo na haijafutwa Tanzania, Anaweza kukupeleka jela daima

Sasa wewe unataka wasaidizi wake wamwambie Rais Jamaa hakupata corona wakati Yeye alikuwepo kama Makamu wake wa Rais

Hakuna Rais alipokosea kuwa Jamaa alipata korona

Thibitisha hapa kwa vyeti kuwa hakuwa na korona

Je wewe una akili?
Rais ndiye sheria , kanuni na utaratibu?
 
.....who contracted COVID?.....
.......Ambaye alipata COVID?....

It doesn't mean kwamba alikufa kwa COVID! hata kama aliugua.
JPM alikuwa special kiasi gani asife na Covid? wakati huyu mtu alikuwa na afya ya trip moja ya pili gereji
 
... mdogo mdogo MATAGA & Co; wataelewa tu. Ubishi mwingi akili punje ya haradali. Kauli rasmi kutoka kwa Rais na Amri Jeshi Mkuu vyombo vya ulinzi na usalama ambaye taarifa zote za taifa hili ziko mikononi mwake! Nani anapinga kauli ya Amiri Jeshi Mkuu?
UTAKUWA NBIRIKIMO WA FIKRA,WAKATI ANAHOJIWA,HAKUJIBU KAMA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,ALIJIBU KAMA SAMIA,LKN SIKU ANATANGAZA KIFO CHA MAGUFULI,ALIKUWA KAMA MKUU WA NCHI AKIITANGAZIA DUNIA, SASA NYIE WENYE AKILI MBIRIKIMO NA FIKRA ZENYE MATEGE,MNA AJENDA ZENU BINAFSI,
 
Kulikuwa na ulazima gani starings wa loyal tour kuulizana hayo maswali?
Kuna narrative fulani ambayo ukielewa western mentality iliyojengeka kumhusu Magufuli, na western mentality kuhusu underdog kushinda adversity, ndiyo utaelewa hapo kimefanyika nini.

Yani hapo unaambiwa Tanzania ni nchi nzuri sana, ila, ilikuwa na uongozi mbovu wa rais ambaye hakukubali Covid-19 ipo, hata chanjo. Rais Samia alipojaribu kumtetea Magufuli kwamba jamaa alikuwa mkemia mzuri tu, mzungu akasema that is even worse. Yani Rais aliona anamtetea mwenzake kwamba alikuwa msomi, mzungu akapigilia msumari hapo hapo kwamba kama kasoma halafu anakataa Covid-19/ chanjo, hicho ni kitu kibaya zaidi, kwa maana ya kwamba elimu yake haikumsaidia.

Kwa hivyo, narrative iliyotengenezwa hapo, ni kwamba, Tanzania ni nchi nzuri, ila haikuwa na uongozi mzuri. Sasa kwa bahati uongozi huo mbaya umepita, tumepata uongozi mzuri wa Rais SSH unafungua nchi.

Yani, kuuza nchi wenzetu wanaona ni lazima uweke drama (au useme ukweli kuhusu nchi, watu waijue, depending on your view), uoneshe upekee fulani wa Tanzania. Nchi inayoanza kufunguka kuita watalii. Maana nchi nyingi zinaita watalii.

Mimi tatizo naona Rais Samia na timu yake kama hawajapanga na kukubali hili, wanapelekwapelekwa tu. Hawajakubaliana na hao waliopiga interview kwamba wanataka kusema nini, kukisema vipi, mambo gani yaachwe, mambo yapi ni sawa kusema.

Inaonekana ama walipanga hivi, ama hawakupanga wamekosa creative control.

Kama wamepanga ina confuse sana watu, kama hawajapanga wao wenyewe wako so confused.
 
Mama hakuwa anajua anacho jibu hapo alijibu tuuu..kimsingi hakuelewa[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Atakuwa anaona noma kusema 'sorry' kama hakuelewa swali au kuomba ufafanuzi zaidi wa swali ili asionekane yai linamgonga....
 
UTAKUWA NBIRIKIMO WA FIKRA,WAKATI ANAHOJIWA,HAKUJIBU KAMA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,ALIJIBU KAMA SAMIA,LKN SIKU ANATANGAZA KIFO CHA MAGUFULI,ALIKUWA KAMA MKUU WA NCHI AKIITANGAZIA DUNIA, SASA NYIE WENYE AKILI MBIRIKIMO NA FIKRA ZENYE MATEGE,MNA AJENDA ZENU BINAFSI,
... ni wakati gani unamuunganisha au kumtenganisha Samia na urais wake? Alipokuwa kwenye mahojiano aliyekuwa anahojiwa ni mkuu wa nchi iitwayo Tanzania au mtu binafsi? Kilichokupelekea ufikiri kwamba hakujibu kama Rais bali kama Samia ni nini?

Hebu tupe majibu ya hayo maswali tuone huo upana wa fikra ulio nao na sio "NBIRIKIMO" wa fikra kama mimi.
 
Ila kusema ukweli, pamoja na maoni yote yaliyotolewa, ukweli hicho kipande ambacho chief hangaya anaitikia "Yeah" kimehaririwa (editing) manaake kuna maneno fulani yanasikika kablaa.

Japo ukweli ni kwamba, 'mama'anatakiwa kuwa makini sana anapojibu maswali yanayohusu taifa.
Kwasababu hata alipokuwa makamu, kuna story fulani za maisha yake ambazo alizungumza pengine bila kujua athari zake kwa wadadavuaji wa masuala ya siasa!
 
Hiki hapa ni kipande kifupi cha video kutoka kwenye filamu ya Royal tour ambapo Samia anaulizwa kama Magufuli aliambukizwa Corona na yeye kujibu ndiyo.

Anakiri hilo kwenye sekunde ya 18.

NANUKUU:

Peter: In all honest your predecessor (Magufuli) was not a big friend of Vaccines and of the Science.

Samia: No he's a scientist.

Peter: Even worst!

Samia: He is a chemist… he was a chemist.

Peter: He was a chemist?

Samia: Yes

Peter: Who contracted COVID?

Samia: YEAH!

View attachment 2203911
Nilifungua bandiko kuhusu tuhuma hiyo haionekani. Hii hapa kutoka kwa mchambuzi mmoja

MADAI YA SINEMA YA ROYAL TOUR NI KASHFA KUBWA! TUME HURU ICHUNGUZE UKWELI!

1) Niliposikia kwa mara ya kwanza kwamba hii Sinema ya Royal Tour (ambayo Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ni Main Actor and Tour Guide) ina maneno haya kuhusu Kifo cha Rais John Pombe Magufuli nilistuka na sikuamini!

2) Kwa MAONI yangu hii inam-compromise sana Rais Samia ambaye ndiye aliyetutangazia Kifo cha Rais Magufuli na kutufahamisha kwamba kilichomuua Rais Magufuli ni Ugonjwa wa Moyo! Sasa haya ya COVID-19 yanatoka wapi tena?!

3) Najiuliza!

a) Hivi Rais Samia alikubalije kushiriki Sinema inayopotosha Taarifa ya Serikali kuhusu Jambo zito kama hili?!
b) Kwa nini hakudai hicho kipande kiondolewe?!!

4) Ntashangaa sana akitokea "Mtetea Chochote" akasema nae Rais Samia hakuiona na kujiridhisha na Script (if it is all acceptable) kabla ya Uzinduzi wa Movie huko Marekani! It would constitute a serious blunder. An act of gross incompetence on the part of Presidential Advisers (maana "Rais hakosei").

5) Kwa MAONI yangu, huyu anayeongea kwenye hii script ni "Spin Master", Utetezi wake umekaa kipuuzi na hauna mashiko. Ashakum si matusi.

6) Iwapo anachosema "Spin Master" ndiyo Hoja na Majibu ya Serikali (kwamba kilichosemwa kuhusu sababu ya Kifo cha Magufuli kuwa ni COVID-19 ni kauli ya Wanaharakati (ambao wanatajwa kwa Majina)), mimi BJC naomba kuuliza ifuatavyo:

Mbona sasa hawakusema (kwenye hiyo Sinema ya Royal Tour) kwamba "kuna na Watanzania wengi wengine (na hata Watu wa Nje) ambao wanaamini Rais Magufuli kauawa"?!

7) Ushahidi!

a) Rais Samia aliwahi kuwakemea kwa hasira wanaodai Rais Magufuli kauawa.
b) Rais Samia akasema wenye Ushahidi kwamba Rais Magufuli kauawa wampelekee.

8) Ushauri wa Bure!

a) Baada ya Sinema ya Royal Tour kulikoroga big time, ni wazi kwamba kumbe kweli kuna umuhimu wa kuunda Tume Huru ya Kuchunguza Kifo cha Rais John Pombe Magufuli. Wadanganyika tunataka kujua kwa uhakika: Je, Rais Magufuli alikufa kwa Ugonjwa wa Moyo (ambao haukusababishwa na mkono wa Mtu), alikufa kwa COVID-19 au aliuwawa?! Na alikufa lini exactly?!
b) Naamini Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ataona umuhimu huu. Asipuuze hili, hasa ikizingatiwa kwamba yeye ndiye Main Actor and Main Guide in this movie that has come up with this act of not only gross disrespect for our late President but also explosive provocation directed towards our Nation and all Tanzanians!
c) Namshauri Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan awe mwangalifu sana kutambua kwamba Kifo cha Magufuli kimeligawanya Taifa... na hivyo afanye kazi ya ziada kutuunganisha badala ya kutugawa na kuruhusu Watu (na hasa) Viongozi kutonyesha vidonda kila kukicha!

9) Kauli Tata zimeshamiri Nchini na zinaleta taharuki kila kukicha!

10) Mfano wa Kauli Tata!

a) "...ile ilikuwa Nidhamu ya woga tu!"
b) "Nchi imeharibiwa sana hii!"
c) "Sasa tunairudisha Tanzania Duniani!"
d) N.k.

11) Kwa bahati mbaya sana, kauli zinazotolewa kila kukicha kumkandia na kumharibia jina Rais Magufuli zinachochea wasiwasi wa baadhi ya Watanzania! Kama nilivyosema, zinaleta taharuki. Baadhi ya Wadanganyika tunajiuliza:

a) Kwa nini wenzie waliomo Serikalini ndio wanaongoza Mashambulizi?!
b) Kwa nini Serikali ya Awamu ya 6 inaonekana ku-enjoy kuitupia Madongo Serikali ya Awamu ya 5?! Serikali ya Magufuli! Strangely, by more than 90% Serikali ya Awamu ya 6 ndiyo Serikali ya Awamu ya 5!! Rais wa sasa ndiye alikuwa Makamu wa Rais Magufuli (na Mshauri wake Mkuu), Makamu wa Rais wa sasa ndiye alikuwa Waziri wa Fedha, Waziri Mkuu yuleyule, Mkuu wa Usalama wa Taifa yuleyule, IGP yuleyule, CDF yuleyule, Jaji Mkuu yuleyule, n.k., n.k.
c) Kwa nini baadhi ya Viongozi wa Serikali ya Awamu ya 6 wanatoa matamshi ambayo yanaashiria kwamba kumbe (labda) walikuwa na Chuki kubwa kwa Rais, Mwenyekiti na Amiri Jeshi Mkuu wao, Rais Magufuli?!
d) Inakuwaje wale wote waliotofautiana na Rais Magufuli wamepandishwa vyeo na Kauli zao na Matendo yao yanaonyesha hawajutii walichofanya?! Ni kama vile wanatamba kwa "Ushujaa" wao wa Kupambana na Rais Magufuli?! Wote tunazikumbuka zile audio clips...!!
e) Kwa nini baadhi ya Viongozi wa "Matawi ya Juu" Nchini wako bize kumbomoa Magufuli and his Legacy! Hivi hii well-coordinated attempt at "Character Assassination" ina Lengo gani na Faida gani?! Imesababishwa na nini?!
f) Kwa nini Serikali na Chama hamumtetei Magufuli?! Saa zote ni Kimya au Mashambulizi tu! Why?!
g) Hivi mmesahau kwamba mwenzenu amepumzika na hana tena Uwezo wa Kujitetea?!
h) Hivi mmesahau kwamba Rais Magufuli ameacha Mke na Watoto ambao mnawaumiza sana kwa Mashambulizi yenu na/au Kimya chetu?! Kwa nini msiwaache walau wakauke machozi?!
Hivi mnasahau kwamba wao ni Bin Adam na wanawashangaa sana, to say the least?!

12) Hivi ni sawa kweli kwamba Serikali, Chama Tawala, Wabunge, Mawaziri, Taasisi mbalimbali, Jumuia mbalimbali (mfano: UV-CCM, UWT, Wastaafu, n.k.)... wote mko kimya kabisa kila Hayati Magufuli anavyotukanwa na kudharirishwa?! Eti hata Viongozi wa Dini nao mko kimya! Mbona haiingii akilini?!

Unafiki huu, mmhuuu...! Au labda ni ukondoo tu...?! Au ni Guilty Consciousness...?!

13) Sasa kama Magufuli alikuwa Rais mbaya kiasi hicho (which I don't believe anyway), inawezekanaje nyinyi Washirika wake wote muwe wasafi kiasi hicho cha kuthubutu kumtupia mawe mazito hivyo Mwenzenu?!

a) Collective Responsibility iko wapi?!
b) Hivi nyie wengine mnaponaje?!
c) Hivi mnajua kwamba kwenye Sheria za Kimataifa iliwekwa precedent kwenye Nuremberg Trials (baada ya Vita Kuu ya Dunia)?! Kesi za Washirika wa Hitler...! Kwa kifupi, Mahakama ya Kimataifa iliamua kwamba Rais/Kiongozi Mkuu hawezi kuwa Shetani na Mawaziri/Wasaidizi wake wote wakawa Malaika...!! Never!
d) Mbona mnatufanya Wadanganyika Mafala?!
e) Mbona mnajichanganya hivyo?!

14) Narudia!

a) Wasiwasi na Hasira za Wadanganyika vinasababishwa na mengi.
b) Mungu anayajua Maovu yetu yote (sisi wote) na Hukumu zake!
c) Tusicheze na moto!

15) MUNGU IBARIKI TANZANIA!


BJC. DSM. 26.04.2022. 1924hrs.
 
Ukitazama kile kipande ni ya wazi hakuzamiria kumaanisha kuwa Magufuli alikufa kwa Corona maana jamaa kama alimpandishia maswali wakati yuko kwenye mood ya swali lililopita na yeye akajikuta anasema “yaaah”

Rais hakuelewa anaulizwa nini hakuiwa dhamira yake kukubali kuwa Magufuli alikufa kwa Corona
Lakini ukweli ulio wazi ni kuwa Rais Magufuli alikufa kwa corona. Na kufa kwa ugonjwa wowote ule siyo aibu.
 
Kuna neno limekatwa hapo kuridhisha njaa zako... ...liishia herfu t' tya ndo yeahh!?;! Acha ujinga.
 
He is a Chemistry... oooohh He was a Chemistry
Bongo bado sana rasi Simba anahitaji kuongeza madarasa
Amesema he was a Chemist siyo he was a Chemistry. Chemist ni mkemia na Chemistry ni somo la kemia.
 
Mbona tunalijua hili tangu zamani! Serikali ilikuwa inatumia staili ya mbuni kuficha kichwa wakati mwili upo peupe!
Kwahiyo alipotuambia kuwa amekufa kwa ugonjwa wa.UMEME alitupiga kamba diyo?.
 
JPM alikuwa special kiasi gani asife na Covid? wakati huyu mtu alikuwa na afya ya trip moja ya pili gereji
Nawe una matatizo yako kichwani. Tujaribu kujiongeza badala ya zomea-zomea inayotufanya tutawaliwe kiurahisi kabisa!
Nani kasema hawezi kufa kwa COVID. Tunaongelea tabia ya rais wetu KUROPOKA kwa mambo ambayo hata hajawahi kuwaeleza wa-TZ. ukweli ana tabia ya 'KIHERE-HERE" Kiongozi mzuri husikiliza na kutafakari maana ya swali. Maana ya mazungumzo. Marais wetu wengi wanataka kujionesha kwamba ni miamba kuliko anayewahoji. Mtu hajamaliza swali, anakuja na jawabu au tusi. Angalia mahojiano yote ya akina Mkapa, Kikwete, Magufuli na sasa huyu, ni majibu uchwara tu!

Nyerere alikuwa tofauti kabisa!! Ukitaka raha ya Nyerere tafuta mahojiano yake na Lynda Chalker aliyekuwa ni minister of state overseas...... wa UK alipokuja Dar na kumuuliza Nyerere juu ya mgogoro wa Pemba. Ilikuwa baada ya uchanguzi wa Mkapa uliokuwa na vurugu.
 
... mdogo mdogo MATAGA & Co; wataelewa tu. Ubishi mwingi akili punje ya haradali. Kauli rasmi kutoka kwa Rais na Amri Jeshi Mkuu vyombo vya ulinzi na usalama ambaye taarifa zote za taifa hili ziko mikononi mwake! Nani anapinga kauli ya Amiri Jeshi Mkuu?
Hakuna😂
 
Kwahiyo alipotuambia kuwa amekufa kwa ugonjwa wa.UMEME alitupiga kamba diyo?.

..haikuwa kamba.

..maambukizi ya Covid husababisha maradhi mengine aliyonayo mhusika kuwa hatarishi na mabaya zaidi.

..kwa mfano, ukiambukizwa Covid huku una ugonjwa wa pumu basi hilo tatizo la pumu litakuwa baya zaidi.

..ukiambukizwa Covid ingali una tatizo la kisukari basi sukari hiyo itakusumbua ktk kiwango ambacho hujawahi ku'experience.

..Jpm alikuwa na tatizo la moyo. Sasa kama aliambukizwa Covid upo uwezekano ilifumua tatizo la moyo kwa namna ambayo haikuwahi kumtokea huko nyuma.

..Jambo lingine linaloacha maswali ni kwamba, kama tatizo lilikuwa ni moyo, kwanini hawakumlaza Jakaya Kikwete Cardiac Institute ambako ndiko waliko wabobezi wa magonjwa ya moyo? Kwanini alikuwa akitibiwa Hospitali ya Mzena?

..Kwa maoni yangu Ssh hakukosea kutangaza kuwa Jpm alifariki kutokana na tatizo la mapigo ya moyo.

..Vilevile hii ni mara ya kwanza Ssh kuulizwa kuhusu Jpm kuambukizwa Covid na majibu yake yamekuwa hayo.

..Mtu anayeweza kukanusha statement ya Rais kwa sasa hivi ni Daktari wa Jpm au mwanafamilia aliyekuwa na taarifa za afya na matibabu yake.
 
Back
Top Bottom