Rais Samia anavuna alichopanda, hana budi kuvumilia

Rais Samia anavuna alichopanda, hana budi kuvumilia

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2020
Posts
7,799
Reaction score
14,215
Habari zenu ndugu zangu,

Wakuu wenzangu, wakati Rais Samia anaingia madarakani wengi tulimshauri aache kufanya maamuzi kwa kufuata mashinikizo ya watu ndani ya mitandao ya kijamii. Kama ilivyo kawaida ya ushauri ni mshauriwa kufuata au kuacha kufuata anachoshauriwa.

Raisi akaamua kupuuza ushauri wetu kwa kuanza timua timua ya viongozi wote waliokuwa wanashutumiwa na wapinzani humu mitandaoni bila kujali uchapaji wao wa kazi. Lakini raisi hakuishia hapo katika kutaka kuwafurahisha wapinzani na wanaolalamika mitandaoni, Rais akauonesha umma wa Watanzania na dunia kwa ujumla kwamba kuna watu walikuwa wameonewa na kukamatwa bila makosa yoyote chini ya utawala wa awamu ya tano na hata ya nne pia. Akaamua kutengeneza mazingira ambayo yamewasaidia wengi kutoka ndani ya vifungo vyao walivyokuwa wamefungwa kutokana na kesi mbalimbali.

Kati ya wafungwa hao walioachiwa kutokana na mipango au jitihada za mama ni wale mashehe wa uamsho, na yule muhindi ambao walikamatwa wakati wa utawala wa JK. Pia yupo kijana anaeitwa Mdude ambae alikamatwa wakati wa utawala wa JPM. Wote waliokamatwa wameonesha shukran zao kwa raisi kutokana na jitihada alizofanya mpaka kuachiwa kwao, lakini huyu Mdude yeye ameonekana kutoshukuru kwa lolote, anachofanya yeye ni kutafuta njia ya kumchafua raisi kana kwamba haoni jitihada zake katika kuachiwa kwake.

Je, Mdude hafahamu kwamba bila mama kuweka jitihada zake na huruma wake mpaka leo angekuwa bado ananyea debe kama alivyokuwa ananyea wakati wa utawala uliyopita? Hata hivyo simlaumu Mdude bali hii itumike kama fundisho kwa mama. Asiwe anafanya mambo kwa kufuata mashinikizo ya mitandao, bila shaka Rais Samia ashapata jibu kwamba ni kwanini watu aina ya kina Mdude waliwekwa ndani na hawakuachiwa hivi hivi. Wakati mungine mtu unaweza kuwa sio katili, lakini watu wakakufanya ukawa katili.

Rais Samia sasa inambidi avumilie maana ni kama vile kinyago amekichonga mwenyewe afu leo kinamtafuna pia ajue siku zote shukrani ya punda ni mateke.

Asanteni.
 
Wakati mungine mtu unaweza kuwa sio katili, lakini watu wakakufanya ukawa katili

(Hapa nimekuelewa sana) Na ndio wengi walikua hawamuelewi Magu. Hawa wanaojiita wapinzani wanahitaji style ya magu ili mambo yaende.
 
Mama kama unasoma huku mtandaoni,. Tunakuomba usiwachekee hawo watu wanaojiita wapinzani hawakawii kumwaga damu za watanzania ,. Tunakupenda sana ila hichi kikundi cha chadema wanataka kukudhalilisha mama wakazie
 
Wakati mungine mtu unaweza kuwa sio katili, lakini watu wakakufanya ukawa katili

(Hapa nimekuelewa sana) Na ndio wengi walikua hawamuelewi Magu..hawa wanaojiita wapinzani wanahitaji style ya magu ili mambo yaende.
Kweli mkuu, just imagine mtu kama Mdude badala ya kumshukuru raisi kwa kusimamia haki hadi yeye akatoka eti anaanza kumtengenezea na yeye beef mwisho wa siku mama kama walivyo binadam wengine uzalendo utamshinda na kuanza kutumia madaraka yake kumwadhibu yeye Mdude na wengine wa aina yake.

JK alikuwa mvumilivu na mwenye huruma lkn watu walimlazimisha kutumia madaraka yake matokeo yake watu wakaanza kulalamika sijui kina Mwangosi wameng'olewa kucha, sijui aliuwa watu katika bomu la soweto kule Arusha nk.
 
Maajabu hivi ni mwana CCM gani hakulionja joto la Magu? Nani hakuumia moyo juu ya yaliyokuwa yakifanyika,ni nani kati yenu alipona juu ya udharirishaji uliokuwa ukifanyika juu ya wana wa nchi hii? na vibaraka wapenda vyeo walevi wa madaraka akina sabaya,makonda and so on.

Kwa hali hiyo mnamtaka huyu mama nae aige ujinga huo ili iweje? ni dhihaka,matusi mangapi yametamkwa na wana CCM Katika kipindi hicho bila kukemewa na mtu yeyote! mmesahau hadi mlikuwa mnapendekeza akina nani wana faa kuuwawa,kuna kosa kubwa kama mtu binafsi kupitisha hukumu ya kifo juu ya raia mwenzake.

Enyi CCM Jaza Tumbo kweli mnamshauri huyu mama atende sawasawa na matendo ya mwendazake? Je, watoto wake wanayo mioyo ya kuhimili machungu wanayoyapata sasa watoto wa mwendazake juu ya matendo ya baba yao?

kWA HURUMA KABISA, namshauri mama asije akakubari ushauri wa kipumbavu kama huu kabla hajatekeleza hayo aitizame mioyo ya kizazi chake kama inaweza kuhimili mateso na moto utakao tokana na matendo yake mabaya akiwa jumba jeupe maana hapo yeye ni mpangaji tu,
 
Kwa hiyo tuseme huyu Mama (Samia Suluhu) anafanya yale yale ya Mwendazake John P. Magufuli?

Kwamba, mahakama haikuzingatia sheria katika kutoa hukumu ya Mdude Chadema isipokuwa ilifuata maagizo ya Rais na kwa hiyo alitoka kwa "hisani ya Rais Samia Suluhu?"

Kumbe ndo maana mnamwandama hivi kiasi cha kutaka kumfanya kuwa mtumwa wa "hisani ya Rais Samoa" siyo?

Tukisema kuwa Rais Samia aweza kuwa Magufuli wa kike msishangae na ndiyo maana Mdude Chadema anasema "...wembe uliomnyoa Magufuli ndiyo huohuo utamnyoa na huyu mama!"

Kiukweli, kama mambo ndo yako hivi, basi Mimi naunga mkono hoja, wembe uleule uliomnyoa yule basi umnyoe na huyu.
 
Maajabu hivi ni mwana CCM gani hakulionja joto la Magu? Nani hakuumia moyo juu ya yaliyokuwa yakifanyika,ni nani kati yenu alipona juu ya udharirishaji uliokuwa ukifanyika juu ya wana wa nchi hii? na vibaraka wapenda vyeo walevi wa madaraka akina sabaya,makonda and so on.

Kwa hali hiyo mnamtaka huyu mama nae aige ujinga huo ili iweje? ni dhihaka,matusi mangapi yametamkwa na wana CCM Katika kipindi hicho bila kukemewa na mtu yeyote! mmesahau hadi mlikuwa mnapendekeza akina nani wana faa kuuwawa,kuna kosa kubwa kama mtu binafsi kupitisha hukumu ya kifo juu ya raia mwenzake.

Enyi CCM Jaza Tumbo kweli mnamshauri huyu mama atende sawasawa na matendo ya mwendazake? Je, watoto wake wanayo mioyo ya kuhimili machungu wanayoyapata sasa watoto wa mwendazake juu ya matendo ya baba yao?

kWA HURUMA KABISA, namshauri mama asije akakubari ushauri wa kipumbavu kama huu kabla hajatekeleza hayo aitizame mioyo ya kizazi chake kama inaweza kuhimili mateso na moto utakao tokana na matendo yake mabaya akiwa jumba jeupe maana hapo yeye ni mpangaji tu,
Kwahiyo unaona Mdude ana haki ya kumkosea heshima mama kwa sababu ya makosa yaliofanywa na JPM au Sabaya? Je hauoni kwamba Mdude alistahili kumshukuru mama kwa kufanya juhudi za kusimamiwa sheria mpaka yeye akatoka kitu ambacho kabla ya mama kuingia madarakani kilikuwa hakiwezekani?

Je ni haki mtu kukulaumu ww kwa makosa yaliofanywa na ndugu au rafiki yako? Je Mdude alitaka mama aachane na kesi zao ili aendelee kunyea debe kama alivyokuwa ananyea hapo kabla?
 
Kwa hiyo tuseme huyu Mama (Samia Suluhu) anafanya yale yale ya Mwendazake John P. Magufuli...?

Kwamba, mahakama haikuzingatia sheria katika kutoa hukumu ya Mdude Chadema isipokuwa ilifuata maagizo ya Rais na kwa hiyo alitoka kwa "hisani ya Rais Samia Suluhu..?"

Kumbe ndo maana mnamwandama hivi kiasi cha kutaka kumfanya kuwa mtumwa wa "hisani ya Rais Samoa" siyo?

Tukisema kuwa Rais Samia aweza kuwa Magufuli wa kike msishangae na ndiyo maana Mdude Chadema anasema "...wembe uliomnyoa Magufuli ndiyo huohuo utamnyoa na huyu mama...!"

Kiukweli, kama mambo ndo yako hivi, basi Mimi naunga mkono hoja, wembe uleule uliomnyoa yule basi umnyoe na huyu...
Kabla ya kukimbilia kunilaumu mimi ebu jaribu kuusoma uzi wang vizuri ili ujue ninachomaanisha, kuliko kusoma nusu na kuja na lawama zisizokuwa na msingi.
 
MPAKA Sasa shida iliyopo KAULI YA SSH rais kuonekana kutokua tiyari endeleza Mchakato wa Katiba MPYA, vinginevyo hajatoka nje ya mstari MPAKA Sasa , ila nyie CCM Kindakindaki, maslahi, limbukeni mnaharibia Sana, angalau CCM HURU naona wanaweza msaidia japo ndo hawapendwi NDANI ya Chama chenu maana wanasimamia haki Katika chama na taifa
 
Jamii forums imeingiliwa na watu wa ajabu kweli kweli! Hivi Mdude alitolewa na Mama au alishinda?

Hao Mashekh wa uamsho Kama wlikuwa na kosa, kwanini hawakufunguliwa mashtaka kwa miaka 8?

Mleta mada wewe ni wa hovyo Sana. Samahani lakini.
 
Kwahiyo unaona Mdude ana haki ya kumkosea heshima mama kwa sababu ya makosa yaliofanywa na JPM au Sabaya? Je hauoni kwamba Mdude alistahili kumshukuru mama kwa kufanya juhudi za kusimamiwa sheria mpaka yeye akatoka kitu ambacho kabla ya mama kuingia madarakani kilikuwa hakiwezekani?

Je ni haki mtu kukulaumu ww kwa makosa yaliofanywa na ndugu au rafiki yako? Je Mdude alitaka mama aachane na kesi zao ili aendelee kunyea debe kama alivyokuwa ananyea hapo kabla?
Maumivu ya Mdude ni nani anayajua? Ni nani anajua ameathirika kwa kiwango gani,kiakili, kisaikolojia,kimawazo nani anaweza kututhibitishia kuwa Nyangari ni mzima wa afya ya mwili na akili baada ya mateso aliyopitiani nani kati yatu.
Kabla ya kupata majibu ya mambo hayo hatuna haki ya kumlaumu mdude nyangali.
 
Msimsingizie Mama, Anafanya kazi zake kwa haki na utaalamu, hakurupuki wala hatishiki, Ngoja asimamishe uchumi, mpaka sasa anaonyesha atakuwa ndiye Raisi bora tangu uhuru
 
Wakati mungine mtu unaweza kuwa sio katili, lakini watu wakakufanya ukawa katili

(Hapa nimekuelewa sana) Na ndio wengi walikua hawamuelewi Magu. Hawa wanaojiita wapinzani wanahitaji style ya magu ili mambo yaende.
MFUFUE SASA AJE AWASHIKISHE ADABU
 
Maumivu ya Mdude ni nani anayajua? Ni nani anajua ameathirika kwa kiwango gani,kiakili, kisaikolojia,kimawazo nani anaweza kututhibitishia kuwa Nyangari ni mzima wa afya ya mwili na akili baada ya mateso aliyopitiani nani kati yatu.
Kabla ya kupata majibu ya mambo hayo hatuna haki ya kumlaumu mdude nyangali.
Kama ni tatizo la kisaikolojia au akili kwanini vitisho na kejeli hizi hakumwambia Mbowe, Lisu, Sugu au kiongozi yoyote wa Chadema. Yeye amezielekeza kwa raisi ambae utawala wake umesimamia sheria kikamilifu mpk yeye kutoka jela katika mazingira ambayo hata yeye Mdude hakuyategemea? Raisi huyu huyu anaetolewa maneno ya kashfa na vitisho na Mdude ndio aliembadilisha mwanasheria mkuu wa serikali ambae amefanya mchakato kuhakikisha watu wenye kesi kama za kina Mdude wanaachiwa huru. Leo hii Mdude badala ya kushukuru kwa usimamiaji wa sheria uliochagizwa na mama, eti anakuja na vitisho visivyokuwa na maana. Hivi mtu anawezaje kukulaumu ww kwa kosa lililofanywa na ndugu au rafiki yako?
 
Maajabu hivi ni mwana CCM gani hakulionja joto la Magu? Nani hakuumia moyo juu ya yaliyokuwa yakifanyika,ni nani kati yenu alipona juu ya udharirishaji uliokuwa ukifanyika juu ya wana wa nchi hii? na vibaraka wapenda vyeo walevi wa madaraka akina sabaya,makonda and so on.

Kwa hali hiyo mnamtaka huyu mama nae aige ujinga huo ili iweje? ni dhihaka,matusi mangapi yametamkwa na wana CCM Katika kipindi hicho bila kukemewa na mtu yeyote! mmesahau hadi mlikuwa mnapendekeza akina nani wana faa kuuwawa,kuna kosa kubwa kama mtu binafsi kupitisha hukumu ya kifo juu ya raia mwenzake.

Enyi CCM Jaza Tumbo kweli mnamshauri huyu mama atende sawasawa na matendo ya mwendazake? Je, watoto wake wanayo mioyo ya kuhimili machungu wanayoyapata sasa watoto wa mwendazake juu ya matendo ya baba yao?

kWA HURUMA KABISA, namshauri mama asije akakubari ushauri wa kipumbavu kama huu kabla hajatekeleza hayo aitizame mioyo ya kizazi chake kama inaweza kuhimili mateso na moto utakao tokana na matendo yake mabaya akiwa jumba jeupe maana hapo yeye ni mpangaji tu,
Hayo mwambie huyo Mdudu sijui Mdude wenu alokosa ADABU
 
Msimsingizie Mama, Anafanya kazi zake kwa haki na utaalamu, hakurupuki wala hatishiki, Ngoja asimamishe uchumi, mpaka sasa anaonyesha atakuwa ndiye Raisi bora tangu uhuru
Kama mnaamini hivyo, kulikuwa na maana gani ya Mdude kuongea yale aliyoongea? Je Mdude hajui wala haoni kama mama hakurupuki wala hatishiki kama ulivyoandika hapa? Je kama anajua ni kwanini kajaribu kumtishia kumnyoa kwa wembe alotumia kumnyolea mtangulizi wake? Naomba twende hoja kwa hoja ndugu yang.
 
Back
Top Bottom