Rais Samia aongeza Saa 24 kwenye uokoaji Kariakoo

Rais Samia aongeza Saa 24 kwenye uokoaji Kariakoo

Kunadugu bado wako chini kabisa ila hawaongeibsbb hawana nguvu,,serikali injitahidi kupekua Kila kitu kiwaokoa
 
Kuna kitu sielewi, ina maana ukishapita muda huo ulioagizwa na Rais ni kwamba jengo litaporomoshwa lote kwa kuamini kwamba ambao bado wapo chini ya kifusi watakuwa wamekwisha fariki?
 
Saa 72 ni sawa na siku 3, hizi UN wamesisitiza kuwa ni muhimu sana na zinaweza kuokoa hadi 95% ya watu kwenye majanga. Katika muda huo wa siku tatu, maana yake kila anayekumbwa na majanga kuna vitu vya kuzingatia na UN wameweka baadhi ya vitu hivyo ktk tovuti yao 5 essentials for the first 72 hours of disaster response

Rais Samia amesema ameongeza saa 24 ili zoezi la uokoaji uendelee na watanzania wanapongeza suala hili nadhani hawajaelewa maana ya saa 72. Ndani ya saa 72 uwezekano wa kukuta watu wako hai ni mkubwa, sasa kuongeza saa 24 inathibitisha kwamba tumeshindwa kujipanga dhidi ya majanga hadi kuhitaji muda wa ziada ambao kimsingi haukoi watu bali unaokota maiti tu. Kwa saa 72 ilitakiwa kujua muktadha, kupeleka vifaa stahiki na watu wenye ujuzi ili kuokoa watu.

Na UN wanapoweka saa 72 za uokozi haimaanishi kuwa baada ya saa hizi msiendelee kuokota maiti. Mtaendelea ila kwa kujali mazingira siku tatu zinathibitisha uwezo wetu wa kukabiliana na majanga. Fikiria sasa maiti tayari zimeshaanza kuharibika badala ya kuongeza nguvu ili kuokoa watu na kuopoa maiti ili shughuli nyingine ziendelee tunaongeza muda.

Imekuwa ni aibu ninapoona watu wanasema rais ana huruma kaongeza muda. Utadhani kwamba UN wamewaambia baada ya saa 72 fukieni eneo la tukio. Hivi ni lini tutaiwajibisha serikali ili kuboresha namna ya kudeal na majnaga ili kupounguza idadi ya watu tunaowapoteza kwa uzembe tu.

Mtu yeyote mwenye tusi jipya aliseme hapa ili nitukane maana nimekereka sana kwa hizi akili za machawa
 
Wao wakifa wanataka tuwazungushe Tanzania nzima mwezi mzima, leo wapendwa wetu wanapewa masaa ya kuokolewa?Kweli inawezekana sisi ni zaidi ya maiti, mimi sikujua kama kunasheria ya kigaidi kama hii
Sheria za uchaguzi zinakanyagwa kwa manufaa yao Leo wanajifanya sheria za uokozi ndio wanazifuata kwa makini
 
Tukitegemea serikali kutupa data jua tumeisha.

Kuwe na platform ya kutoa taarifa ya raia ambao hawajaonekana tangu siku ya ajali ya jengo ili tupate estimated data.
 
Kwahiyo kumbe uokoaji una muda maalum kwamba ukipita tunaondoka eneo la tukio kuwe na Watu ama Lah?
Bila shaka wanamaanisha uokoaji wa walio hai.
Baada ya hapo zoezi litabadilika na kuwa na kuopoa miili ya wafu.
Baada ya hapo zoezi litakuwa na kuhamisha vifusi.

Kila hatua hapo kuna taratibu zake! Nawasilisha!
 
Wakuu,

Wajuvi wa masuala haya, kwahivyo, bila kujali hali ilivyo muda wa uokoaji ikitokea janga kama hili huwa ni masaa 72 pekee?

Kwa jinsi ile ajali ilivyotokea watakauwa waokoaji watakuwa wamefika maeneo yote? Naona kama kuna watu wataachwa huko wajifie!

=====

View attachment 3155882View attachment 3155883

View attachment 3155951
Maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuongeza saa 24 za uokoaji katika jengo lililoporomoka eneo la Kariakoo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemuelekeza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kuongeza saa 24 za uokoaji katika jengo lililoporomoka eneo la Kariakoo.

Rais Dkt. Samia ametoa maelekezo hayo wakati akizungumza kwa njia ya simu na Mhe. Majaliwa kuhusiana na zoezi la uokoaji na kusema:

"Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninatambua utaratibu wa uokoaji una muda maalum wa saa 72 mpaka kusitisha zoezi hilo. Binafsi nina matumaini kuwa Mwenyezi Mungu anaweza akatenda miujiza yake na kuweza kuwanusuru ndugu zetu wengine ambao bado wamenasa kwenye jengo hilo. Ninakupa maelekezo ya kutositisha zoezi la uokoaji na kuongeza muda wa saa 24 zaidi ili kuwapambania ndugu zetu ambao tunaamini bado wako hai."

Aidha, Rais Dkt. Samia pia ameongeza kusema kuwa: "Kwa vikosi vyetu vyote na wananchi wote wanaopambana kuokoa maisha ya ndugu zetu katika zoezi hilo ninaomba ufikishe salamu zangu na uwaeleze kuwa natambua na nina wathamini sana. Wameonyesha utu, uzalendo mkubwa na uchapakazi wa hali ya juu sana. Hivyo nawatia moyo na kuwapa nguvu ya kuendelea kuwapambania ndugu zetu kwani ninyi ni mashujaa wa taifa letu"

Rais Dkt. Samia anawaombea kwa Mungu awalinde na kuwapa nguvu muda wote wakiwa wanateleleza jukumu hilo kubwa na la kizalendo.

Kwa upande mwingine, Rais Dkt. Samia amewasihi wananchi, ndugu na jamaa kuendelea kuwa na subira na kama taifa tuendelee kuwaombea ndugu zetu na wapiganaji wetu ili tufanikishe zoezi hili kwa mafanikio makubwa.

Mwenyezi Mungu tunakuomba utufanyie wepesi kwenye zoezi hili. Amin
Sharifa B. Nyanga
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu
Masaa 24 ni madogo kuwaokoa Watu bado wapo Wangeongeza Masaa 72 mengine tena aka siku 3 au mpaka jumapili ingelikuwa ni vizuri sana. Kuliko kuweka masaa 24 ni madogo sana kuwaokoa watu kazi yake sio ndogo jamani kuna watu bado wapo ndani wanasubiri kuokolewa Rais anatoa Masaa 24 kuwaokoa watu? Duhhhhhh Majangaa kweli.


View: https://www.youtube.com/watch?v=t56sMX_8jMk&ab_channel=GlobalTVOnline
 
Mungu nisamehe mie mja wako, lakini akili inaniambia kinamna fulani kuzaliwa tz ni kama kalqana fulani hivi.

Pengine umeniepusha kuzaliwa somalia, ama haiti n.k.. Ila bongo napo sio kipolepole.
 
Bila shaka wanamaanisha uokoaji wa walio hai.
Baada ya hapo zoezi litabadilika na kuwa na kuopoa miili ya wafu.
Baada ya hapo zoezi litakuwa na kuhamisha vifusi.

Kila hatua hapo kuna taratibu zake! Nawasilisha!
Kwanini waongeze saa 24?
Kumbe zoezi linaendelea
 
Back
Top Bottom