Rais Samia atengua Uteuzi wa Wakuu wa Wilaya za Temeke na Kilindi

Rais Samia atengua Uteuzi wa Wakuu wa Wilaya za Temeke na Kilindi

vivo hivyo kwa anaetenguliwa taarifa anapewa hata kabla haijawa public.
Siyo kweli. Acha kuandika stori za vijiweni. Yaani mtu ataarifiwe kuwa atatumbuliwa??

Mkuu wa wilaya ameishitaki serikali baada ya kutumbuliwa. Sasa ameishitaki kwann wakati alosaini kukubali kutbuliwa??

Watanzania ni watuwajinga sana. Hawajisomei. Wanakariri wanachosimuliwa vijiweni . Jinga kabisa.
 
Huu uongo. Kaji alitenguliwa toka mwaka juzi, akarudi kwenye mambo yake ya ukitengo huko idarani. Sasa hivi ndio kateuliwa kuwa DC.

Ukiwa kitengo unapaswa kufanya kazi yoyote utayopangiwa. Nafasi yako idarani ipo palepale
umeelewa nilichoandika
 
1.Mobhare Holmes Matinyi
2. James Wilbert Kaji

Hawa wametokea wapi kwenda kuwa wakuu wa Wilaya???

Wametokea CWT au UVCCM???

Je wana sifa za kuwa wakuu wa wilaya???

Tunahitaji katiba mpya kwa kweli ili wananchi wenyewe wawe na uwezo wa mkumchagua mkuu wawilaya yao,

hii wananchi wa wilaya fulani wanalala na kuamka wanakutana na mkuu wa wilaya mgeni na wa zamani hayupo na hajulikani kaelekea wapi na aliyeletwa hajulikani katokea wapi na ana sifa gani za kupewa ukuu wa wilaya IMEPITWA NA WAKATI kwa karne hii ya 21.

Watanzania tumesoma na kuelimika hila hili hatulielewi hata kidogo.
Hao kila mtu ni mtu na nusu; watu bingwa sana
 
Mpaka sasa ashaumbuka ndomaana hajarudi tena kuandika uharo wake aliobebeshwa na wachumia tumbo.
Kumtukana mwenzako hakukufanyi wewe uonekane bora zaidi. Uliyeumbuka ni wewe maana hamna mkataba kama huo unazungumzia.
Amandla...
 
Kumtukana mwenzako hakukufanyi wewe uonekane bora zaidi. Uliyeumbuka ni wewe maana hamna mkataba kama huo unazungumzia.
Amandla...
Mbona unaonekana kushindwa mapema kijana?
Mkataba nimeanza kuomba mimi hamjaleta. Kwahiyo sijui unajisikiaje nafsini kung'ang'ania kutetea kitu ambacho umeambiwa tu na wajanja fulani ili wakutumie uwapiganie wao na familia zao.

Pili unasema nimemtukana lkn pia hata na hilo dogo tu la kutukana umeshindwa kunionesha tusi lenyewe.

Kwa mawazo haya, acha wanasiasa uchwara waendelea kuvuna waburuzwaji katika ajenda zao.
 
Rais mla rushwa🐒🐒🐒
 
Mbona unaonekana kushindwa mapema kijana?
Mkataba nimeanza kuomba mimi hamjaleta. Kwahiyo sijui unajisikiaje nafsini kung'ang'ania kutetea kitu ambacho umeambiwa tu na wajanja fulani ili wakutumie uwapiganie wao na familia zao.

Pili unasema nimemtukana lkn pia hata na hilo dogo tu la kutukana umeshindwa kunionesha tusi lenyewe.

Kwa mawazo haya, acha wanasiasa uchwara waendelea kuvuna waburuzwaji katika ajenda zao.
Kama umeshindwa kuipata IGA mpaka uletewe basi una matatizo. Humu ndani iko hiyo IGA, yako maoni ya TLS n.k. inaelekea wewe ndie unaetetea kitu ambacho hukijui. Hata Waziri Mbarawa alituambia tukausome maana umejaa mtandaoni. Usipende kutafuniwa kila kitu kijana.

Lakini sikushangai maana hata matusi unayotukana unataka uonyeshwe. Wewe kumwambia mwenzako kuwa anachoandika ni uharo hauoni kama unamtusi?

Amandla...
 
Kama umeshindwa kuipata IGA mpaka uletewe basi una matatizo. Humu ndani iko hiyo IGA, yako maoni ya TLS n.k. inaelekea wewe ndie unaetetea kitu ambacho hukijui. Hata Waziri Mbarawa alituambia tukausome maana umejaa mtandaoni. Usipende kutafuniwa kila kitu kijana.

Lakini sikushangai maana hata matusi unayotukana unataka uonyeshwe. Wewe kumwambia mwenzako kuwa anachoandika ni uharo hauoni kama unamtusi?

Amandla...
Nimeusoma na sijaona kosa. Sasa wewe ulieona kosa ndo utuwekee na kutuambia kosa ni kifungu hiki au mstari huu nk.
Si kila kitu ambacho wewe unakiona kizuri basi na mungine akione hivyo hivyo.
 
Nimeusoma na sijaona kosa. Sasa wewe ulieona kosa ndo utuwekee na kutuambia kosa ni kifungu hiki au mstari huu nk.
Si kila kitu ambacho wewe unakiona kizuri basi na mungine akione hivyo hivyo.
Sasa kama umeusoma kwa nini unang'ang'ania uwekewe? Si upinge tu hoja zinazoletwa kuupinga kwa kukanusha kwa kutumia vifungu? Kwa mfano, watu wanaposema mkataba hauna ukomo, wewe ungesema ukomo uko kwenye kifungu hiki na hiki. Watu wanaposema mkataba hauonyeshi mgao wa faida zitakazopatikan, wewe ungesema, mgawanyiko uko katika kifungu kadha wa kadha. TLS wameonyesha mapungufu yaliyomo katika mkataba huo kwa kupitia kifungu kwa kifungu. Na humu ndani wengi tu wamefanya hivyo lakini mnashindwa kuwajibu. Mkiona hivyo mnakimbilia kwenye matusi.

Kukazania uwekewe mkataba ina maana haujausoma au lugha iliyotumika katika mkataba inakupiga chenja.

Amandla...
 
Sio kweli
Bado ataendelea kupata stahiki zake Kama kawa
 
Nasikia kalamba Tena u DC huko mtwara Leo Sasa sijui mother kasahau au hamna watanzania wengine wa kufanya hiyo kazi?
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 02 Julai, 2023 amefanya mabadiliko madogo ya Wakuu wa Wilaya kama ifuatavyo:

1) Ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Athumani Munkunda na kumteua Mobhare Holmes Matinyi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke.

2) Ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Abel Yeji Busalama. Amemhamisha kituo Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mjini, Hashim Shaib Mgandilwa kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi.

3) Amemteua James Wilbert Kaji kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mjini.

😆😆😆😆😆
 
Back
Top Bottom