Rais Samia athibitisha uhusiano wake na Waziri Mchengerwa

Rais Samia athibitisha uhusiano wake na Waziri Mchengerwa

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1695219406930.png
Kama ulikuwa unasikia tu basi leo Rais Samia Suluhu Hassan amethibitisha uhusiano wake na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Mohamed Mchengerwa.

Mara kadhaa imekuwa ikizungumzwa kuwa wawili hao ni mtu na mkwewe lakini hakuna kati yao aliyewahi kuzungumzia hilo.

Akiwa safarini leo Septemba 20, 2023 kutoka mkoani Lindi Rais Samia amesimama wilayani Rufiji na kuwasalimia wananchi waliokuwa wamejipanga barabarani kusubiri msafara wake.

Baada ya Mchengerwa ambaye ni Mbunge wa Rufiji na mawaziri wengine kupata fursa ya kuwasalimia wananchi ikafika zamu ya Rais Samia na ndipo alipoeleza hilo japo kwa mafumbo.

“Nilikuwa safarini lakini isingewezekana kupita Rufiji bila kusimama, nina Vichengewa viwili nyumbani kwangu sasa siwezi kupita nisisalimie wajukuu, ndiyo maana nikasema nisimame niwasalimie wajukuu,” amesema.

Rais Samia ametumia fursa hiyo kuwasisitiza wakazi wa Rufiji hasa vijana kujikita kwenye kilimo cha mpunga kwa kuwa sasa ni zao la biashara.

“Mpunga imekuwa zao la biashara hivyo niwasihi wakazi wa Rufiji hasa vijana ingieni kwenye kilimo hiki. Mshiriki kwenye mradi wa BBT tulime mpunga kwa wingi ili tuweze kuuza nje,” amesema Rais Samia.
 
Msafara wa Rais Samia ulisimama Rufjji jimboni kwa mh Mchengerwa na Rais akasema asingeweza kupita Rufjji bila kusimama kusalimia Wajukuu zake

Rais amesema ana Vichengerwa Viwili pale nyumbani kwake yaani Wajukuu wake

Source: Gazeti Mwananchi
Ukiuliza pesa iliyomwangwa hapo ndo utashangaa ya Mchengelwa na Mama mkwe wake, leo nataka niwambie kwa mfumo za tawala za kafrika ,Mchengelewa ananguvu sana kuliko waziri yoyote , thats

Unaweza msikiliza matamshi yake huingilia mpaka wizara isiyo mhusu ya mambo ya ndani,

Ila Mungu anasema na narudia kwa kua utawala wa ccm alisha ufutwa ,hata wawepo mchengelwa 100, uchaguzi ukifanyika hatakuja hamini macho yao,ilisha kua asema Bwana
 
Back
Top Bottom