Rais Samia atoa TZS 35BL Ujenzi wa Musoma Airport kumuenzi Baba wa Taifa

Rais Samia atoa TZS 35BL Ujenzi wa Musoma Airport kumuenzi Baba wa Taifa

Ze Bulldozer

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2020
Posts
1,070
Reaction score
568

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ATOA TZS 35BL KUJENGA UWANJA WA "MUSOMA AIRPORT " ILI KUMUENZI HAYATI BABA WA TAIFA KWA VITENDO.​

3-25.jpg
Huu ni muonekano wa baadhi ya vifaa vya ujenzi vya mkandarasi Beijing kutoka nchini China ambavyo vinatarajiwa kutumika katika kazi za maboresho ya uwanja wa ndege wa Musoma karibu na Sehemu alikozaliwa muasisi wa Taifa hili Mwl Julius Kambarage Nyerere,

Serikali sikivu ya Rais Samia Suluhu Hassan imesema inatarajia kutumia kiasi cha TZS 35BL ili kuboresha uwanja wa ndege wa Musoma uliotelekezwa na awamu zote tangu Uhuru,

Maboresho hayo ni pamoja na kuweka lami na kuongeza urefu wa uwanja huo ili kuruhusu ndege kubwa na ndogo kuweza kutua mkoa wa Mara. Uwanja huu pia utahudumia na maeneo ya jirani kama Simiyu na Mwanza,

Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Khalfani Haule, amesema kuwa mradi huo ukikamilika utarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Musoma|Mara na pia kuchochea biashara ya utalii kupitia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo ipo mkoani humo kwani kabla Watalii wengi walishuka uwanja wa KIA,

Ameongeza kuwa Uongozi wa Wilaya tayari umejipanga kwa kuupokea mradi huo na wameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mkandarasi huyo kwa kumpatia eneo la kuchimba mchanga na kokoto za ujenzi.

Naye, Meneja wa Uwanja wa ndege wa Musoma, Mohammed Bakari, amesema kuwa uwanja huo utajengwa na Kampuni ya kikandarasi ya Beijing kutoka China na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.

Amefafanua kuwa Mkandarasi huyo tayari ameshawasilisha vifaa vyake katika eneo la mradi kwa ajili ya kuanza rasmi ujenzi huo, na kusisitiza kuwa ujenzi wa uwanja huo unasimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mkoa wa Mara.Hakika hakuna kama Rais Samia Suluhu Hassan,
 
Cheap!

Kumuenzi Mwalimu Nyerere kiuhalisia ni kumaliza Bwawa la Nyerere hilo lilikuwa ni wazo lake na kuhamia Dodoma, Nyerere alianzisha Mji Mkuu mpya wa Dodoma.

Yote mawili Bwawa la Nyerere na Dodoma Samia anayapiga vita, kama si kwa maneno basi kwa vitendo, angalau kulingana na matendo ya watendaji wake.

Mengine yote usanii tu.
 
Cheap, kumuenzi Mwalimu Nyerere kiuhalisia ni kumaliza Bwawa la Nyerere hilo lilikuwa na wazo lake na kuhamia Dodoma, Nyerere alianzisha Mji Mkuu mpya wa Dodoma.

Yote mawili Bwawa la Nyerere na Dodoma Samia anayapiga vita, kama so kwa maneno basi kwa vitendo.

Mengine yote usanii tu.
JNHPP mama umeona pesa aliyotoa?
 
Tunazidi kufeli kila kukicha yaani Kuna shule hazina madarasa halafu tuna kazi ya kuenziana tu kweli Kama tz tumelogwa mchawi wetu yupo karibu Sana na sisi kuhakikisha hatufurukuti
 
Mm nafikiri ingekuwa vizur Kama angemalizia ile Hospitali yao ya Kanda ya Serengeti
 
Cheap!
Kumuenzi Mwalimu Nyerere kiuhalisia ni kumaliza Bwawa la Nyerere hilo lilikuwa na wazo lake na kuhamia Dodoma, Nyerere alianzisha Mji Mkuu mpya wa Dodoma.

Yote mawili Bwawa la Nyerere na Dodoma Samia anayapiga vita, kama si kwa maneno basi kwa vitendo, angalau kulingana na matendo ya watendaji wake.
Mengine yote usanii tu.
We kweli akili zako ziko ma ta koni,samia anaendelea kutoa fedha kuhenga hilo bwawa la nyerere na ameenda misri kwa nia hiyohiyo leo unasema anaupiga vita?
 
We kweli akili zako ziko ma ta koni,samia anaendelea kutoa fedha kuhenga hilo bwawa la nyerere na ameenda misri kwa nia hiyohiyo leo unasema anaupiga vita?

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app

Kwa mujibu wa watendaji wake Waziri wake muhusika, labda basi nitumie ule msemo wetu ,,anaangushwa na watendandaji wake“ .
 
Back
Top Bottom