Rais Samia atoa TZS 35BL Ujenzi wa Musoma Airport kumuenzi Baba wa Taifa

Rais Samia atoa TZS 35BL Ujenzi wa Musoma Airport kumuenzi Baba wa Taifa

Kwa hiyo kuboresha Uwanja wa Ndege wa Musoma, alikozaliwa Mwalimu sio kumuenzi? Mwendazake alifanya unafiki mkubwa kwa kutoanzisha mradi wowote mpya mkoani Mara, japo alikuwa anajifanya anamuenzi Mwalimu. Mradi pekee aliowazuga watu wa mkoa wa Mara ni kukamilisha (sio kujenga) mawodi mawili matatu ya akinamama wajawazito na watoto kwenye hospitali ya Kwangwa, Musoma zaidi ya hilo hakuna. Hata mradi wa maji wa Bunda aliukuta ukiwa unaendelea tangu enzi za Kikwete. Mama kaamua kutengeneza airport ili kufungua njia nyingine za kiuchumi ikiwemo utalii maana wazungu wakishuka Musoma ni rahisi kwenda Serengeti

Kwa hiyo hoja yako ni nini ? Ni Samia vs Magufuli ? Au Samia + Magufuli ?
 
Tatizo lako ukisikia jina Samia unafananisha na jina la bibi yako kule kijijini!

Jina Samia linawakilisha taasisi ya urais.

Ndio maana Masoud alipoulizwa juu ya kuchora vikatuni vya Samia, alijibu kwamba yeye anachora urais na siyo mtu.

Bavicha mna vichwa vigumu sana.
CCM mpaka mpate akili itachukua muda mrefu sn, hizi ni pesa za umma na siyo mali ya mtu binafsi
 
Hii mradi kanda ya ziwa tu,,mikoa ya mbeya iringa njombe songea ccm wanawaona mapimbi sana
Huu ni muda wa kuifuta ccm mikoa ya nyanda za juu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kanda ya juu kusini, kazi tunayo mbona.
 
Nyerere haenziwi kwa kujenga viwanja vya ndege bali kwa kuheshimu

Wewe tunajua kuwa ndiwe bi kidude mwenyewe unajisifia kwa majina bandia kwenye mitandao
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sasa hizo pesa Mwaka jana za fidia nani alitoa mkuu
Ni serikali na huo mradi ulianza tangu enzi za Kikwete katika mpango wake wa kuboresha viwanja vya ndege vya Songwe, Kigoma, Kagera na Musoma, jiwe akawa anaukwepa kwepa, fidia zililipwa kwa sababu tu ilikuwa kwenye mpango lakini plani ya ujenzi haikuwepo kabisaaaaaaaa
 

BILIONI 35 KUJENGA UWANJA WA NDEGE MUSOMA KUMUENZI BABA WA TAIFA KWA VITENDO,​



3-25.jpg

Huu ni muonekano wa baadhi ya vifaa vya ujenzi vya mkandarasi Beijing kutoka nchini China ambavyo vinatarajiwa kutumika katika kazi za maboresho ya uwanja wa ndege wa Musoma sehemu aliyozaliwa muasisi wa Taifa hili,

Serikali ya Rais Samia Suluhu imesema inatarajia kutumia kiasi cha TZS 35BL ili kuboresha uwanja wa ndege wa Musoma,

Maboresho hayo ni pamoja na kuweka lami na kuongeza urefu wa uwanja huo ili kuruhusu ndege kubwa na ndogo kuweza kutua.

Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Khalfani Haule, amesema kuwa mradi huo ukikamilika utarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Musoma na pia kuchochea biashara ya utalii kupitia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo ipo mkoani humo.

Ameongeza kuwa Uongozi wa Wilaya tayari umejipanga kwa kuupokea mradi huo na wameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mkandarasi huyo kwa kumpatia eneo la kuchimba mchanga na kokoto za ujenzi.

Naye, Meneja wa Uwanja wa ndege wa Musoma, Mohammed Bakari, amesema kuwa uwanja huo utajengwa na Kampuni ya kikandarasi ya Beijing kutoka China na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.

Amefafanua kuwa Mkandarasi huyo tayari ameshawasilisha vifaa vyake katika eneo la mradi kwa ajili ya kuanza rasmi ujenzi huo, na kusisitiza kuwa ujenzi wa uwanja huo unasimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mkoa wa Mara.Hakuna kama Samia, View attachment 2029306
Angeuacha tu. Wenyeji wa mkoa wa Mara hawathamini mkoa wao ndiyo maana hata mwl aliongoza miaka 24 na akauacha kama mnavyouona.

Pia walikuwa viongozi kibao wa kitaifa lakini hakuna chochote walichokifanya. Mwingine aliishia kujisifia kula vichwa vya watu na kukata mauno.
 

BILIONI 35 KUJENGA UWANJA WA NDEGE MUSOMA KUMUENZI BABA WA TAIFA KWA VITENDO,​



3-25.jpg

Huu ni muonekano wa baadhi ya vifaa vya ujenzi vya mkandarasi Beijing kutoka nchini China ambavyo vinatarajiwa kutumika katika kazi za maboresho ya uwanja wa ndege wa Musoma sehemu aliyozaliwa muasisi wa Taifa hili,

Serikali ya Rais Samia Suluhu imesema inatarajia kutumia kiasi cha TZS 35BL ili kuboresha uwanja wa ndege wa Musoma,

Maboresho hayo ni pamoja na kuweka lami na kuongeza urefu wa uwanja huo ili kuruhusu ndege kubwa na ndogo kuweza kutua.

Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Khalfani Haule, amesema kuwa mradi huo ukikamilika utarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Musoma na pia kuchochea biashara ya utalii kupitia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo ipo mkoani humo.

Ameongeza kuwa Uongozi wa Wilaya tayari umejipanga kwa kuupokea mradi huo na wameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mkandarasi huyo kwa kumpatia eneo la kuchimba mchanga na kokoto za ujenzi.

Naye, Meneja wa Uwanja wa ndege wa Musoma, Mohammed Bakari, amesema kuwa uwanja huo utajengwa na Kampuni ya kikandarasi ya Beijing kutoka China na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.

Amefafanua kuwa Mkandarasi huyo tayari ameshawasilisha vifaa vyake katika eneo la mradi kwa ajili ya kuanza rasmi ujenzi huo, na kusisitiza kuwa ujenzi wa uwanja huo unasimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mkoa wa Mara.Hakuna kama Samia, View attachment 2029306
Pesa za kuanza ujenzi wa uwanja wa Musoma, Msalato, Mbeya, Geita (Chato) na Mtwara zilitengwa katiba Bajeti ya mwaka 2017 au 2018 hivi. Process ya Ujenzi inaendelea kwa miaka kama minne au mitano hivi, na mpaka sasa viwanja vyote havijakamilika sawasawa, ingawa kile cha mbeya nadhani kimetangulia kufuatia na cha Chato au Msalato.
Mkuu sami huo uwanja kaja kukamilisha tu mradi umeanza enzi za jiwe maan ata fidia watu wamelipwa wakat wake
Utakuwa na nguvu sana kubishana na CM 1774858 katika swala lolote linalohusu Samia! Account hiyo imefunguliwa miezi sita tu iliyopita ila tayari ina posts zaidi 2200 ambapo 98% ya posts zote hizo ni kuhusu Samia.
 
Safi sana Mama Samia. Kale kauwanja kalikuwa kanatia aibu. Na itasaidia Sana mkoa wa Mara kiuchumi kupitia utalii hususani mbuga ya Serengeti. Mtalii akishashuka atafika kirahisi na kuingia Serengeti kupitia lango la Lamadi au Mugumu kwenye hifadhi wanyama za Grumeti au Ikoma. Pia itakuwa ni short cut ya kwenda Mkoa wa Simiyu kwa wilaya za Busega na Bariadi ambayo ndii makao makuu ya mkoa.
 
Uwanja huu ulihitaji ukarabati siku nyingi naujua. Msiingize siasa kwenye hili sio kumpaka Mwl Nyerere mafuta kwa mgongo wa chupa. Musoma walihitaji huu uwanja siku nyingi kwanza wapo karibu zaidi na mbuga ya Wanyama ya Serengeti kuliko Mwanza na Arusha. Hoteli za kitalii zilitakiwa zijengwe Musoma sio Mwanza wala Arusha tu. Serikali iitazame Musoma kama sehemu ya utalii sio eti Nyerere acheni siasa kwenye vitu hivi. Nisieleweke vibaya kuwa nampuuza Mwalimu hapana nilimuheshimu na naheshimu legacy zake.
 
Uwanja huu ulihitaji ukarabati siku nyingi naujua. Msiingize siasa kwenye hili sio kumpaka Mwl Nyerere mafuta kwa mgongo wa chupa. Musoma walihitaji huu uwanja siku nyingi kwanza wapo karibu zaidi na mbuga ya Wanyama ya Serengeti kuliko Mwanza na Arusha. Hoteli za kitalii zilitakiwa zijengwe Musoma sio Mwanza wala Arusha tu. Serikali iitazame Musoma kama sehemu ya utalii sio eti Nyerere acheni siasa kwenye vitu hivi. Nisieleweke vibaya kuwa nampuuza Mwalimu hapana nilimuheshimu na naheshimu legacy zake.
Sio vitu vya kulazimisha kujenga uwanja wa kimataifa Chato na kuanzisha mbuga ya wanyama kwa nguvu na wanyama wenyewe sijui wapo au walishavuka mpaka kwenda Rwanda? Tutumie hela za wananchi kwa umakini sio kutafutia kiki za kisiasa hata Mwalimu asingetaka hizi kauli.
 

BILIONI 35 KUJENGA UWANJA WA NDEGE MUSOMA KUMUENZI BABA WA TAIFA KWA VITENDO​

3-25.jpg
Huu ni muonekano wa baadhi ya vifaa vya ujenzi vya mkandarasi Beijing kutoka nchini China ambavyo vinatarajiwa kutumika katika kazi za maboresho ya uwanja wa ndege wa Musoma sehemu aliyozaliwa muasisi wa Taifa hili,

Serikali ya Rais Samia Suluhu imesema inatarajia kutumia kiasi cha TZS 35BL ili kuboresha uwanja wa ndege wa Musoma,

Maboresho hayo ni pamoja na kuweka lami na kuongeza urefu wa uwanja huo ili kuruhusu ndege kubwa na ndogo kuweza kutua.

Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Khalfani Haule, amesema kuwa mradi huo ukikamilika utarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Musoma na pia kuchochea biashara ya utalii kupitia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo ipo mkoani humo.

Ameongeza kuwa Uongozi wa Wilaya tayari umejipanga kwa kuupokea mradi huo na wameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mkandarasi huyo kwa kumpatia eneo la kuchimba mchanga na kokoto za ujenzi.

Naye, Meneja wa Uwanja wa ndege wa Musoma, Mohammed Bakari, amesema kuwa uwanja huo utajengwa na Kampuni ya kikandarasi ya Beijing kutoka China na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.

Amefafanua kuwa Mkandarasi huyo tayari ameshawasilisha vifaa vyake katika eneo la mradi kwa ajili ya kuanza rasmi ujenzi huo, na kusisitiza kuwa ujenzi wa uwanja huo unasimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mkoa wa Mara.Hakuna kama Samia,
Unajenga uwanja wa ndege kumuenzi Mwalimu? Sio kuhudumia wananchi na biashara zao?

Amandla....
 
Back
Top Bottom