Rais Samia atoa TZS 35BL Ujenzi wa Musoma Airport kumuenzi Baba wa Taifa

Rais Samia atoa TZS 35BL Ujenzi wa Musoma Airport kumuenzi Baba wa Taifa

Cheap!
Kumuenzi Mwalimu Nyerere kiuhalisia ni kumaliza Bwawa la Nyerere hilo lilikuwa ni wazo lake na kuhamia Dodoma, Nyerere alianzisha Mji Mkuu mpya wa Dodoma.

Yote mawili Bwawa la Nyerere na Dodoma Samia anayapiga vita, kama si kwa maneno basi kwa vitendo, angalau kulingana na matendo ya watendaji wake.
Mengine yote usanii tu.
Bwawa la Nyerere halikuwemo katika mipango yake. Environmental Impact Assessment iliposema halina tija akaliweka pembeni. Kama ambavyo walivyofanya marais watatu waliomfuata.

Amandla...
 
Bwawa la Nyerere halikuwemo katika mipango yake. Environmental Impact Assessment iliposema halina tija akaliweka pembeni. Kama ambavyo walivyofanya marais watatu waliomfuata.

Amandla...
Nani huyo?
 

BILIONI 35 KUJENGA UWANJA WA NDEGE MUSOMA KUMUENZI BABA WA TAIFA KWA VITENDO​

3-25.jpg
Huu ni muonekano wa baadhi ya vifaa vya ujenzi vya mkandarasi Beijing kutoka nchini China ambavyo vinatarajiwa kutumika katika kazi za maboresho ya uwanja wa ndege wa Musoma sehemu aliyozaliwa muasisi wa Taifa hili,

Serikali ya Rais Samia Suluhu imesema inatarajia kutumia kiasi cha TZS 35BL ili kuboresha uwanja wa ndege wa Musoma,

Maboresho hayo ni pamoja na kuweka lami na kuongeza urefu wa uwanja huo ili kuruhusu ndege kubwa na ndogo kuweza kutua.

Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Khalfani Haule, amesema kuwa mradi huo ukikamilika utarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Musoma na pia kuchochea biashara ya utalii kupitia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo ipo mkoani humo.

Ameongeza kuwa Uongozi wa Wilaya tayari umejipanga kwa kuupokea mradi huo na wameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mkandarasi huyo kwa kumpatia eneo la kuchimba mchanga na kokoto za ujenzi.

Naye, Meneja wa Uwanja wa ndege wa Musoma, Mohammed Bakari, amesema kuwa uwanja huo utajengwa na Kampuni ya kikandarasi ya Beijing kutoka China na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.

Amefafanua kuwa Mkandarasi huyo tayari ameshawasilisha vifaa vyake katika eneo la mradi kwa ajili ya kuanza rasmi ujenzi huo, na kusisitiza kuwa ujenzi wa uwanja huo unasimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mkoa wa Mara.Hakuna kama Samia,
Halafu atakuaa anatua hapo? Vipi wa Chato ushaisha phase II?

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Nchi haina dira, viongozi wanajenga miradi isiyo na tija kisa kufurahishana
 
anataka kujenga uwanja wa kuanikia mahindi, na mtama au? sijaelewa
 
Kwa kuendeleza na kuufanyia maboresho uwanja huu nakupongeza maana, nikirudisha kumbukumbu zangu nyuma alipofariki Nyerere ndege nyingi zilishindwa kutua katika kiwanja kile hakika utakuwa umeacha alama kwa wana Mara na Wana musoma kwa ujumla.

Kuhusu kile chuo kilichopelekwa butiama sijajua kwanini hadi sasa hawajaanza fanya udahili
 
Hii mradi kanda ya ziwa tu,,mikoa ya mbeya iringa njombe songea ccm wanawaona mapimbi sana
Huu ni muda wa kuifuta ccm mikoa ya nyanda za juu
Nyanda za juu nyie sio watanzania halisi sijajua kwanini hamkuangukia kwenye nchi za jirani zetu
 
Tanzania kamwe hatutaendelea hivi karibuni ikiwa hatuna mwelekeo wala dira katika uongozi wa nchi. Kila rais ajaye anabuni mambo yake. Baya zaidi ni mambo haya ya kujitakia sifa. Uwanja wa ndege ni huduma/kitega uchumi, haujengwi kwa sababu ya kmuenzi mtu, yeyote. Sidhani kama kuna mtaala wowote uliofanywa juu uwanja huo utarudisha vipi pesa za watoa kodi. Inaelekea pesa za Watanzania zaamuliwa na mhumuko mmoja tu na mapenzi ya mtu! Nchi itaendelea vipi hivyo?
Natoa mfano wa Rwanda: kwa miaka 20 tu iliyopita Rwanda imepiga hatua kubwa sana ya kuigwa. Bila shaka sababu kuu ni kuwa kuna mwelekeo, dira na uongozi usobadilika badilika kama kinyonga.
Pili: Kwa nini kajiwanja kama haka kajengwe na Wachina? Jamani. Inadhi sana. Si muagize vyombo tu msivyonavyo? Mainjinia chungu nzima wapo. Walieni tu nusu ya mnavyowalipa Wachina watafanya kazi zaidi ya Wachina. Mbona Waafrika hatujiamini hivi?
 
SERIKALI NDIO IMETOA FEDHA NA SIO SAMIA.

HAJATOA KWENYE AKAUNTI BINAFSI BALI KITOKA HAZINA YA JMT [emoji1241]
 

BILIONI 35 KUJENGA UWANJA WA NDEGE MUSOMA KUMUENZI BABA WA TAIFA KWA VITENDO​

3-25.jpg
Huu ni muonekano wa baadhi ya vifaa vya ujenzi vya mkandarasi Beijing kutoka nchini China ambavyo vinatarajiwa kutumika katika kazi za maboresho ya uwanja wa ndege wa Musoma sehemu aliyozaliwa muasisi wa Taifa hili.

Serikali ya Rais Samia Suluhu imesema inatarajia kutumia kiasi cha TZS 35BL ili kuboresha uwanja wa ndege wa Musoma,

Maboresho hayo ni pamoja na kuweka lami na kuongeza urefu wa uwanja huo ili kuruhusu ndege kubwa na ndogo kuweza kutua.

Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Khalfani Haule, amesema kuwa mradi huo ukikamilika utarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Musoma na pia kuchochea biashara ya utalii kupitia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo ipo mkoani humo.

Ameongeza kuwa Uongozi wa Wilaya tayari umejipanga kwa kuupokea mradi huo na wameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mkandarasi huyo kwa kumpatia eneo la kuchimba mchanga na kokoto za ujenzi.

Naye, Meneja wa Uwanja wa ndege wa Musoma, Mohammed Bakari, amesema kuwa uwanja huo utajengwa na Kampuni ya kikandarasi ya Beijing kutoka China na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.

Amefafanua kuwa Mkandarasi huyo tayari ameshawasilisha vifaa vyake katika eneo la mradi kwa ajili ya kuanza rasmi ujenzi huo, na kusisitiza kuwa ujenzi wa uwanja huo unasimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mkoa wa Mara.Hakuna kama Samia,
Najua vijana wengi wa sasa hamjui . Miaka ya nyuma kuna kiwanja cha ndege cha kimataifa kilitakiwa kujengwa sehemu moja inaitwa Nyansurura. Baada ya Nyerere kuondoka madarakani mpango huo ukafanyika hadi leo. Ilikuwa kumuenzi vizuri ilikuwa kujenga huo kuliko ukarabati wa huo.
 
Najua vijana wengi wa sasa hamjui . Miaka ya nyuma kuna kiwanja cha ndege cha kimataifa kilitakiwa kujengwa sehemu moja inaitwa Nyansurura. Baada ya Nyerere kuondoka madarakani mpango huo ukafanyika hadi leo. Ilikuwa kumuenzi vizuri ilikuwa kujenga huo kuliko ukarabati wa huo.
Uwanja unajengwa sio kukarabatiwa, Palikuwa na vumbi tu pale
 

BILIONI 35 KUJENGA UWANJA WA NDEGE MUSOMA KUMUENZI BABA WA TAIFA KWA VITENDO​

3-25.jpg
Huu ni muonekano wa baadhi ya vifaa vya ujenzi vya mkandarasi Beijing kutoka nchini China ambavyo vinatarajiwa kutumika katika kazi za maboresho ya uwanja wa ndege wa Musoma sehemu aliyozaliwa muasisi wa Taifa hili.

Serikali ya Rais Samia Suluhu imesema inatarajia kutumia kiasi cha TZS 35BL ili kuboresha uwanja wa ndege wa Musoma,

Maboresho hayo ni pamoja na kuweka lami na kuongeza urefu wa uwanja huo ili kuruhusu ndege kubwa na ndogo kuweza kutua.

Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Khalfani Haule, amesema kuwa mradi huo ukikamilika utarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Musoma na pia kuchochea biashara ya utalii kupitia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo ipo mkoani humo.

Ameongeza kuwa Uongozi wa Wilaya tayari umejipanga kwa kuupokea mradi huo na wameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mkandarasi huyo kwa kumpatia eneo la kuchimba mchanga na kokoto za ujenzi.

Naye, Meneja wa Uwanja wa ndege wa Musoma, Mohammed Bakari, amesema kuwa uwanja huo utajengwa na Kampuni ya kikandarasi ya Beijing kutoka China na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.

Amefafanua kuwa Mkandarasi huyo tayari ameshawasilisha vifaa vyake katika eneo la mradi kwa ajili ya kuanza rasmi ujenzi huo, na kusisitiza kuwa ujenzi wa uwanja huo unasimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mkoa wa Mara.Hakuna kama Samia,
Huyu Samia ni tajiri sana kumbe.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom