EvilSpirit
JF-Expert Member
- Jun 15, 2017
- 10,576
- 16,644
Nimesheshangazwa mno ujinga unauita ukweli hizo salamu alizozituma unazoziita nzito zina kila ngapi ndio maana nakuita mjingaMimi siyo chawa bali ni msema kweli.
Nakuandalia kitita hicho cha wewe kulipia ili upewe U platinum na kuendelea kujitawala humu jukwaani kama mbayuwaiDr Restart umemuelewa Lucas?
Acha uchonganishi wako hapa wewe na kusubiri mkono udondoke kama fisi fanyavyo.utasindikiza mpaka MlangoniNimecheka sana.
Nilikuambia utapigwa maneno tu.
RubbishNdugu zangu Watanzania,
Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hasssan ametuma salamu nzito za pongezi kwa Mheshimiwa Cyril Ramaphosa ,kwa kuchaguliwa kwake kwa kishindoo kwa muhula wa pili kama Rais wa Taifa hilo.
Salamu hizo zimetolewa na Rais wetu kupitia mtandao wa Twitter,ambapo amempongeza sana kwa imani kubwa aliyopewa ya kuendelea kuliongoza Taifa la Afrika kusini,lakini pia Rais wetu ameahidi kuendelea kushirikiana naye na Taifa la Afrika kusini na kuendeleza Historia yetu ya kindugu na ya muda mrefu.
Mheshimiwa Ramaphosa ameshinda Urais huo baada ya kupata kura karibu 283 na kumshinda mgombea wa chama cha EFF kinachoongozwa na Mhessimiwa Julius Malema aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa vijana wa chama cha ANC kabla ya kutimuliwa kwenye chama hicho.Na kuunda chama chake cha Economic Freedom Fighters. Ambapo kwa sasa chama chake kilipata kura 9% na kuzidiwa na chama cha Mheshimiwa Zuma kilichoanzishwa miezi michache tu iliyopita kilichopata 15%.
Lakini pia uchaguzi huu umeshuhudia ANC ikiporomoka vibaya sana katika Historia ya uchaguzi wa Taifa hilo na kushindwa kufikisha 50% ya kura. Jambo lililopelekea ANC kufanya mazungumzo na chama cha DA kilichopata 22% ya kura zote.
Naamini ANC na viongozi wake watakuja haraka sana Tanzania kujifunza kwa CCM naamna ya kurejesha imani ya wapiga kura kilio wapoteza na waliokinyima kura. Kikubwa ANC inatakiwa ijifunze kwa CCM kuhakikisha kuwa kinakuwa karibu ya wananchi wake, kuwasikiliza kero zao na kuwapatia majibu,kuwa na sera zenye kuleta matumaini kwa watu hasa kundi la vijana ambalo ndio kundi kubwa.
Kwa kuhakikisha kuwa kundi hili linapewa kipaombele ya kisera,kibajeti na kifursa,kama ambavyo CCM imekuwa ikifanya hapa Nchini kwa kutoa kipaombele kwa vijana,kwa kuwapatia ajira,mikopo pamoja na kuwawezesha kwa namna tofauti tofauti. ndio sababu vijana wameendelea kuiamini na kuipigia CCM kura kila uchaguzi.
Lakini pia ni lazima ANC ni lazima ijifunze kwa CCM kuwa na sera zinazoendana na mahitaji ya wakati na zenye kugusa kila kundi na maisha yao,kutumia rasilimali zake zote kujenga miundombinu na miradi itakayotoa fursa za ajira kwa vijana ,pamoja na kuwajengea matumaini hai wananchi wake.ambapo mtu akiamka awe na matumaini ya kupata walau milo mitatu kwa siku, uhakika wa kupata matibabu mtu akiugua,uhakika wa kupata Elimu kijana akifaulu,uhakika wa kupata ajira akimaliza chuo kikuu au kujiajiri katika mazingira salama na rafiki,uhakika wa usalama kwa shughuli zake,uhakika wa watu hasa vijana kujiona fahari kuzaliwa Afrika kusini kama ilivyo kwa watanzania kufurahia kuzaliwa hapa Nchini.
Kazi iendelee,Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Wewe tulizana na elfu saba yako.Acha uchonganishi wako hapa wewe na kusubiri mkono udondoke kama fisi fanyavyo.utasindikiza mpaka Mlangoni
Embu niambie kwanini wananchi wamechagua na kukipatia kura chama cha Democratic Alliance? Kwamba wao hawaifahamu historia ya Taifa lao? Kwanini wasikipe EFF cha Malema au kile cha Zuma cha wapigania uhuru? Tambua kuwa wananchi wamevuka mstari wa ubaguzi na kuangalia chama chenye sera na ajenda zenye kugusa maisha yao ya kila siku. Kuna faida gani ya kung'ang'ania mtu anayekuumiza ,kukutesa,kukunyonya na kukuangamiza? Muache kidogo na kukaa naye mbali kidogo ili ajuwe kuwa hufurahii matendo yake .akijisahihisha na kujirekebisha utamrudia baadaye.Ungalijua DA ni chama cha akinanani usingesifia hili. Unaingia katika kuiongoza nchi na wale watesi wenu wa hapo awali halafu unajidai kuiongoza nchi kwa kipindi kingine.
Hata sisi hapa Tanganyika tuliteswa na Wakoloni lakini hawa Wakoloni weusi wa CCM ndio wametutesa zaidi.Ungalijua DA ni chama cha akinanani usingesifia hili. Unaingia katika kuiongoza nchi na wale watesi wenu wa hapo awali halafu unajidai kuiongoza nchi kwa kipindi kingine.
Safi sana. Embu angalia sasa ulivyoandika kwa ufupi na fasaha.Acha uvivu na papala zako hapa.kioi ambacho hujaelewa hapo .taarifa ni kuwa Rais Samia kampongeza Mheshimiwa Ramaphosa kwa kuchaguliwa kwake Awamu ya pili.na na kuahidi kuendelea kushirikiana naye kuendeleza undugu na ushirikiano wetu wa kihistoria.
Mimi nilishasema kuwa naandika kwa aya ili kila mmoja asome mpaka pale uwezo wake unapoishia kiakili.Safi sana. Embu angalia sasa ulivyoandika kwa ufupi na fasaha.
Ndiyo hivyo ukitakiwa kuandika.
Umenena vyema. Hata hapa Peru tujiulize kama kunavfaida gani kung'ang'snia hawa watesi wetu? Muda utaongea.Embu niambie kwanini wananchi wamechagua na kukipatia kura chama cha Democratic Alliance? Kwamba wao hawaifahamu historia ya Taifa lao? Kwanini wasikipe EFF cha Malema au kile cha Zuma cha wapigania uhuru? Tambua kuwa wananchi wamevuka mstari wa ubaguzi na kuangalia chama chenye sera na ajenda zenye kugusa maisha yao ya kila siku. Kuna faida gani ya kung'ang'ania mtu anayekuumiza ,kukutesa,kukunyonya na kukuangamiza? Muache kidogo na kukaa naye mbali kidogo ili ajuwe kuwa hufurahii matendo yake .akijisahihisha na kujirekebisha utamrudia baadaye.
500k ndio sh ngap?Lucas mbona umenikimbia kule kwenye uzi!? Nilipie 500k niwe platinum member...!🤸
500,000500k ndio sh ngap?
Kumbe, huo u platinum unasaidia nini ?500,000
Status tu! Sidhani kama kuna cha muhimu zaidiKumbe, huo u platinum unasaidia nini ?
😁😁Status tu! Sidhani kama kuna cha muhimu zaidi