Rais Samia Atunukiwa Tuzo Mapambano Dhidi ya Dawa za Kulevya

Hii zawadi anastahili ila maelezo yawe kinyume chake. Hata yeye anajua.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametunikuwa tuzo ya Kutambua mchango wake kwenye mapambano dhidi ya dawa za Kulevya nchini.

Tuzo hiyo imekabidhiwa kwake na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyeiwasilisha kwa niaba ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA).

Rais Samia amepewa tuzo hiyo katika maadhimisho ya kitaifa ya kupiga vita matumizi na biashara ya dawa hizo duniani ambayo kitaifa yamefanyika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha leo Jumapili Juni 25, 2023.
 
Nadhani Tanzania itabidi tuje na Tuzo ya Kutoa Tuzo....

Yaani nani anaongoza kwa Kutoa Tuzo...

Utakuta Taasisi ya kusaidia wakulima badala ya kujikita kwenye uchunguzi wa kuwapunguzia wakulima gharama au kuja na mbolea bora wana-brainstorm ni nani wa kumpa Tuzo na ni vipi mpewaji ata-reciprocate kuwapa fadhila....

Hizo pesa za kuandaa Tuzo kingekwenda kwenye Trenches kusaidia hicho ambacho mpewaje anapewa kwa so called amekifanya
 
bashite si ilikuwa tuzo ya kunyang'anya watu magari na pesa, ulitaka naye apewe?
 
Makonda akirudi kwenye madaraka nitaamini hii story inayotrend kuwa ni kweli
 
Aahaaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…